Tuesday, March 12, 2013

MKUU WA WILAYA YA BUTIAMA NA USALAMA

BUTIAMA MARA,



 Mkuu wa Wilaya ya Butiama,Angeline Mabula  amesema kuwa hali ya Ulinzi na Usalama katika Wilaya hiyo imeimarika tofauti na hapo awali ambapo ilikubwa na matukio ya mauaji ya kutisha.

Alikuwa akizungumza na Waandishi  kutoka vyombo mbalimbali vya  habari vya Radio, Magazeti na Luninga juu ya mafaniko ya awamu ya nne katika Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi kwa kipindi cha mwaka 2005-2012


Kwa siku za hivi karibuni, Wilaya ilikumbwa na wimbi la mauaji yanayohusishwa na imani za kishirikina, Serikali imechukua kila tahadhari kuhakikisha kwamba mauaji hayatokei tena,elimu imeendelea kutolewa, ili kuhimiza ulinzi shirikishi ambao utakuwa suluhisho la tatizo la mauaji”Alisema Mabula. 

Alisema kuwa historia inaonyesha kwamba, mbali na mauaji yatokanayo na ugomvi wa koo, wizi wa mifugo na ugomvi/migogoro ya ardhi mauaji ya sasa ya kuchinja watu hayakuwahi kutokea, yameibuka tu kwa udanganyifu  wa watu kutaka kujipatia utajiri wa haraka haraka.

Serikali inafanya kila linalowezekana kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wahalifu wa aina zote, kwa kuwafichua na kuwafikisha mbele ya vyombo vya dola ili kulinda raia wake na mali zao. 
Aidha Wilaya ina vituo 10 vya polisi Buhemba, Bisumwa, Bukima, Suguti, Kiagata, Kyabakari, Kigera etuma, Butiama, Saragana na Tegeruka.

Aliongeza kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua katika kuwahimiza na kuwaelewesha wananchi kuwa ulinzi wao na mali zao uko mikononi mwa wananchi wenyewe wakishirikiana na Polisi, dhana ya Polisi jamii na ulinzi shirikishi inaendelea kuhimizwa.


Wilaya imeweka mpango madhubuti wa  kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa vijana au wanamgambo waliokwishapitia mafunzo ili kuimarisha ulinzi na Usalama katika maeneo yao na kuwatahadharisha kutojichukulia sheria mikononi.


Amewataka vijana na akinamama kuunda vikundi ili wapewe vitendea kazi ambavyo vitawasaidia katika kazi zao za ujasiliamali na kwamba jumla ya Sh. Milioni 90 zimetegwa kwa aili ya kuwawezesha vijana na akina mama ,ambapo kati ya hizo Milioni 45 ni za Vijana na Milioni 45 ni za vikundi vya akina mama ambapo watapewa vitendea kazi watakapokuwa wamejisajili.


Aidha vikundi 4 vya wajasiliamali vilipewa mikopo yenye thamani ya Sh. 180,000,000 kutoka mfuko wa wajasiliamali unaofadhiliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Vikundi vilivyopewa fedha ni Mwangaza SACCOS Buhemba Tshs. 80,000,000, Imani Bwai (Kiriba) Shs. 31,000,000 na Mwamucha SACCOS (Mugango) Tshs. 30,000,000




Katika kipindi cha miezi sita halmashauri imeweza kusimamia vizuri fedha zilizopatikana katika vyanzo mbalimbali kwa ajili ya kugharamia matumizi ya mishahara, matumizi mengineyo na miradi ya maendeleo.  Pia Ruzuku ya Serikali imeongezeka kutoka Sh.571,556,000 mwaka 2005 hadi Sh.975,426,302  mwaka 2012 sawa na 59%.




No comments:

Post a Comment