Saturday, March 2, 2013

HATIHATI YA KIFO CHA CHADEMA YAINGIA TARIME-MUSOMA

TARIME NA MUSOMA.

BAADHI ya wanachama wa  Chama cha Demokrasi na Maendeleo CHADEMA wamefunga ofisi ya Wilaya iliyoko Mjini Tarime Mkoa wa Mara kwa mabanzi  yaliyopigwa kwa misumari kwa muda wa siku tatu.

 

Wanachama wa Chama  cha Demokrasia  na Maendeleo Chadema Wilayani Tarime wamesikitishwa  kwa kitendo cha  Ofisi ya Chama Wilaya   kufungwa  kwa muda wa siku 3 hadi sasa ambapo mpaka jana mbanzi hayo yalitolewa na kuacha kufuri pekee ambapo baadhi yao walitaka kusikiana mapanga lakini hawakufanya hivyo.


Wanachama walisema kuwa kitendo cha kufungwa ofisi ya chama Wilaya kimewafanya wao wasipate huduma za kichama  na kwamba kitendo hicho cha kufunga ofisi kitarudisha nyuma chama kutokana na viongozi kutokuwa kioo kwa wanachama wake.

Mjumbe mmoja  wa chama hicho mkazi wa Nyamisangura ambaye hakutaka jina lake kutajwa alisema kuwa  sababu ya kufungwa kwa ofisi imekuja baada ya Kaimu Mwenyekiti wa Chadema Wilaya Lucas Ngoto kusimamishwa  uongozi na kamati Tendaji jambo ambalo  alikuafikiwa na baadhi ya wananchama na kuibua mgogoro mkubwa ambao umewafanya baadhi yao kugawanyika makundi.

Mjumbe huyo aliongeza kuwa  kwa sasa kunampasuko mkubwa ndani ya chama cha Chadema ambapo tayari kuna makundi mawili yanayodaiwa kuwa kundi moja ni la Mwenyekiti wa Vijana Taifa John Heche  na kundi la George Waitara ambao wanadaiwa   kuwa wapo mbioni na wanajipanga kugombea Ubunge uchaguzi 2015 kutoka ndani ya chama hicho.

“Sababu ya kufungwa kwa ofisi ni baada ya  Kaimu Mwenyekiti wa chama Wilaya  Lucas Ngoto kusimamishwa uongozi ambapo sababu hatuzijui na ieleweke kuwa ndani ya chama kuna makundi mawili haya makundi hayaelewani kati ya kundi la Heche na Waitara sasa huyu Kaimu  yeye yuko kundi la Waitara  kundi la Heche halimtaki jambo ambalo lilisababisha watu wa kundi la  La Waitara  kufunga Ofisi kwa mabanzi na kugonga misumari,kama tunataka kunusuru chama  hawa watu wasipewe nafasi za kugombea Ubunge watauwa chama yote haya ni kwa sababu ya kujitengenezea mazingira mazuri ya uchaguzi ujao”alisema Mjumbe mmoja.

Dominic Manyama Mkazi wa Mtaa wa Starehe alisema kuwa makundi yanayoendelea ndani ya chama  ni dalili ya Chama hicho kushindwa uchaguzi wa mwaka 2015  kwa madai kuwa Chama hicho kimekuwa kikiaminiwa na wananchi walio wengi na kuendelea kuwepo kwa makundi kutawafanya watu kutokuwa na imani ya Chama hicho.

Wanachama  wamewataka viongozi wa Kitaifa kufika Tarime kutatuwa mgogoro ili kukinusuru chama na kwamba vinginevyo baadhi ya wanachama watakihama chama hicho kwa kuwa kina mgogoro mkubwa wa kimadaraka na kuwa kufunga ofisi  inaleta picha mbaya kwa wanachama na watu wengine.

Kaimu Mwenyekiti wa Chadema Wilaya, Lucas Ngoto  alipohojiwa nini sababu ya yeye kusimamishwa uongozi na kuwepo kwa  makundi ndani ya chama na wakati uchaguzi ukingali bado alisema kwa sasa hawezi kuongea chochote na kuahidi kutoa taarifa baada ya siku tatu.

Katibu Mwenezi wa chama cha Chadema Wilaya Marwa Maruri  alisema kuwa  leo wanatarajia kukaa kikao cha Chama na kwamba taarifa kamili ataitoa  kesho juu ya maamuzi yatakayo kuwa yamepatikana kutokana na kikao  hicho.

Inasemekana kuwa,Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe anatarajiwa kufika siku yoyote kusuluhisha mgogoro huo huku ofisi kwa sasa ikiwa imefugwa kwa kufuri  na kungo'oa mabanzi yaliyokuwa yamepigiliwa na misumari.

Mjini Musoma Meya wa Manispaa hiyo,Alex kisurura alinusurika kung'olewa na madiwani wenzake kwa kile kinachodaiwa kuwa ni ubadhilifu wa fedha. 

No comments:

Post a Comment