Saturday, March 16, 2013

WANANCHI WANAOZUNGUKA MGODI WA NORTH MARA KUPEWA FIDIA


TARIME.

KUFUATIA kuundwa kwa kikosi kazi (Task Force) kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuchunguza uthamini fidia ya wakazi wanaozunguka mgodi wa Dhahabu wa North Mara,wananchi hao sasa watapatiwa ufumbuzi wa tatizo hilo.

Hayo yamesema na Afisa Mthamini Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mwenyekiti wa Kikosi kazi hicho, Adam Yusuf alipokuwa akijibu hoja ya Diwani wa kata ya Mbogi,Wilaya ya Tarime Mkoa wa Mara  Sylivester Nyankomo,katika kikao cha Baraza la Madiwani, kuhusu fidia utatuzi wa mgogoro wa Mgodi na wananchi wanaozungumka katika eneo hilo.


Katika hatua nyingine Diwani huyo pia alikishtumu Kikosi kazi hicho kwa kutoa taarifa isiyo na sahihi wala uthibitisho kutoka kwa mwekezaji,jambo ambalo lilizua mgogoro katika kikao hicho na madiwani kuitaka taarifa hiyo iandikwe na kuwekewe sahihi ndipo ijadiliwe.



Akisoma taarifa hiyo mbele ya baraza la madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Tarime,katika kikao cha dharula cha kupokea taarifa ya  vikao kati ya kikosi kazi cha kushughulikia masuala ya uthamini na fidia, Katibu wa kikosi kazi, Jeremiah  Minja alisema kuwa ni lengo la Serikali kuona kuwa matatizo yaliyojitokeza katika mgodi wa Noth Mara yanapatiwa ufumbuzi wa kudumu na kumwezesha mwekezaji kuendelea na shughuli zake kama kawaida huku haki stahili za wananachi wa ardhi wanaozunguka mgdo huo zikizingatiwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.

Aidha ni azam ya Serikali ni  kuona kuwa amani na Utulivu na mahusiano mema kati ya Mgodi na wananchi wanaozunguka Mgodi huo vinadumishwa na ndiyo maana ikaazimia kiudwe kikosi kazi kitakachojumisha wataalamu na maafisa kutoka katika taasisi mbalimbali za Serikali kusimamia utatuzi wa matatizo hayo.

Alisema kuwa matatizo yaliyojitokeza katika maeneo ya vijiji vinavyozunguka mgodi ni pamoja na wanachi ambao maeneo yao yalifanyiwa uthamini lakini bado hawako tayari kuchukua malipo yao,waliofanyiwa uthamini lakini hawako tayari kuondoka,waliopokea sehemu ya malipo nab ado wako katika maeneo yaliyofanyiwa uthamini,waliofanyiwa uthamini wakachukua malipo yao yote na kuwaendelea kukaa na kuendeleza maeneo ambayo yalifanyiwa uthamini ambapo kuna wengine hawako tayari kuona maeneo yao yakifanyiwa uthamini.


Wiki iliyopita katika kikao cha Baraza la Madiwani  wakati wa kutambulisha kikosi kazi hicho, Baraza liliagiza kikosi hicho kwenda katika vijiji vya Kewanja, Nyangoto na Nyakunguru na Baraza lipewe matokeo ya vikao hivyo kabla ya zoezi rasmi la uthamini na uhakika kuanza katika maeneo husika.
Alisema kuwa baada ya kikao cha halamshauri ya Kijiji cha Kewanja kulitolewa hoja na kujdiliwaambapo iliagizwa Uthamini ufanyike ndani ya wiki mbili,ambapo kikosi hicho kilifanya kazi hiyo kama kilivyoagizwa lakini dosari iijitokeza katika kijiji cha Nyangoto ambao hawakuwa tayari kuzungumza wala  kushirikia katika zoezi hilo hadi hapo Mgodi utakapotoa kesi yao Mahakamani na ndipo kipagwe kikao kingine na uongozi wa mgodi uwepo ili kuzungumza nao.


Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Amos Sagara aliiomba Wizara ya Nishati na Madini ,Baraza la Mazingira (NEMC), wao pia waunde kikosi kazi kingine kwa ajili ya kuchunguza matatizo yanayowakabili wakazi wanaozunguka mgodi huo kwani maisha yao yako hatarini kwa kuwa maji machafu  ya kusafishia dhahabu yanaathiri afya ya watanzania hao ambao hawana hatia.

Aidha alikiomba kikosi kazi hicho kuzunguka kwa vijiji vyote vinavyozunguka Mgodi huo ili kujua matatizo yao ingawaje nayo yanafafa na ya vijiji hivyo, vijiji ambavyo ‘Task Force’ imetakiwa kwenda na kurudisha  mrejesho ni pamoja na Kerende, Nyamwaga, Matongo,  na Genkuru.


Akizungumza katika Kikao  hicho, Meneja wa Mgodi huo,Champman Gerry alitoa shukrani kwa Serikali kuunda timu hiyo ili kuja kutatua matatizo  kwamba amesikia akilalamikiwa  kuwa walikuwa hawalipwi fidia kwa mujibu wa sheria,na kwamba atazingatia utaratibu atakaopewa na kwamba ataufuata   ili kuondoa kabisa matatizo yaliyopo baina yao na wananchi.



No comments:

Post a Comment