Saturday, March 2, 2013

MBEGU YA MAHINDI KUTOKA KENYA INA UGONJWA

TARIME.


Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Mkoani Mara  imetoa tahadhari kwa
wananchi wa Kata ya Nyamwaga kutokana na mbegu mbaya  ya mahindi yenye
ugonjwa wa michirizi ya Mahindi yanapofikia kiwango cha kukomaa
iliyosambazwa kutoka Kenya na wakulima kuinunua kutokana na kuuzwa kwa
bei nafuu  kutoitumia.





Diwani wa Kata ya Nyamwaga ,Joseph Nyagala alitoa taarifa kutoka katani
kwake juu ya ugonjwa uliopo wa mahindi kupata michirizi.


“ugonjwa huo unakuwa hivi unapanda mahindi vizuri yakifikia hatua ya
kubeba muhindi  ganda la juu linakauka kana kwamba mahindi yamekomaa
ukivuna unakutana na aidha gunzi ama michirizi iliyopo kwenye mahindi
ambayo hayana chochote,hii ni hatari sana,mbegu za mahindi hayo yanauzwa
Sh.5000,ambapo mbegu bora ya SIDICO ni Sh. 9,000.Alisema Nyagala.



Mkuu wa Mkoa wa Mara John Tuppa alisema ugonjwa huo kwa sasa umefika Wilaya ya Bunda,ametoa tahadhari wananchi kutonunua mbegu hiyo,ambapo ameagiza wakulima kuyachoma,njaa kali itaukumba Mkoa huu.


No comments:

Post a Comment