SERENGETI
Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori(TAWIRI)
Dk.Simon Mduma amesema kuwa tishio la kutoweka Mbwa Mwitu katika hifadhi ya Serengeti
kutokana na magonjwa mbalimbali ya mbwa litatoweka kwani tayari wamepata chanjo
ili kuweza kumaliza magonjwa yanayosababisha kutoweka kwa Mbwa Mwitu.
Mbwa hao
waliochukuliwa eneo la Loliondo wamefugwa katika Hifadhi ya Taifa (TANAPA) kwa
miezi mitatu hili likiwa ni kundi la pili lenye mbwamwitu 15 ambapo kundi la
kwanza lilitolewa Agosti 30 mwaka huu likiwa na mbwamwitu 11 waliachiwa ndani
ya hifadhi hiyo mwaka 1980 na kulikuwepo Mbwa
Mwitu wapatao 500.
Aidha Mbwamwitu
wapatao 15 ambao walikuwa wamefugwa katika eneo la Nyamuma ndani ya hifadhi
hiyo kwa ajili ya juhudi za kuwarudisha wanyama hao ambao walitopotea miaka ya
1990 wanaendelea vizuri.
Kukosekana
kwa wanyama hao ndani ya hifadhi hiyo kumesababisha kukosekana kwa kivutio
kingine muhimu ambapo watalii wanahitaji kuwaona.
Alitoa pongezi
kwa mashirika mbalimbal ikiwemo ofisi ya
Rais,ambayo ilichangia Sh. M.30 kwa ajili ya mradi wa mbwa mwitu kwani imesaidia kuongeza kivutio muhimu.
Alisema kuwa
kuna changamoto ambazo wanakabiliana nazo ikiwa ni pamoja mashirika mengi
kutofadhili mradi huo ambapo kwa sasa kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom
ndio pekee iliyotoa ufadhili wa zaidi ya milioni 450.
Kutokana na
kuruhusiwa kwa mbwamwitu hao sasa imeongezeka na kufanya idadi ya wanyama hao
kufikia 26 ndani ya TANAPA ambapo Agosti 30 mwaka huu waliachiwa 11.
Hivi karibuni
Rais Jakaya Kikwete aliagiza Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI)
kuhakikisha Mbwamwitu waliofunguliwa katika mbuga ya Serengeti wanakuwa salama muda
wote ili wasitoweke tena.
No comments:
Post a Comment