Tuesday, December 27, 2016

Wabunge nyumbani kwa hayati, Baba wa Taifa.


Baadhi wa wabunge wakiwa katika picha ya pamoja kwa hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere mara baada ya kumaliza kikao chao cha kwanza cha kila mwaka kujadili maendeleo ya Mkoa wa Mara.

MUHONGO AJA NA MIRADI MIPYA JIMBONI KWAKE.




MBUNGE wa Jimbo la Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Madini amewapatia mradi wa Sungura, Kuku na mradi wa kilimo cha mchaichai wananchi wa jimbo lake ambao utawakwamua kiuchumi na kuwa na maendeleo endelevu na kuepuka umasikini uliokidhiri miongoni mwao.
Akitambulisha kampuni ya kubuni na kutengeneza kazi za kujiajiri nchini Tanzania, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo (TBCC), Elibariki Mchau alisema kuwa yuko tayari kuanza mafunzo kwa wajasiriamlai wadogo walio katika vikundi ili waweze kuanza ufugaji mapema na kujipatia pato ambapo Mbunge huyo aliamua kutoa mbegu za sungura na mbegu za mchaichai kwa viukundi vitakavyokuwa tayari kupokea mradi huo.

Ame kuwa mradi huo ni mradi wa biashara ambao unatoa ajira na kipato kikubwa na endelevu hivyo wanapaswa watatoa mafunzo hayo na mbinu za kuendesha miradi hiyo na usimamizibora ili kuhakikisha mkulima anazalisha kwa tija na kpata fadi kubwa zaidi ambapo pia kwa upande wa masoko wao watawaletea soko na kabla ya hapo watatoa mikataba ambao utamuhakikishia huduma bora mkulima na mfugaji.
Aidha akizungumzia juu ya mkojo wa mnyama huyo alisema kuwa mkojo wake ni kiwatilifu kwa ajili ya kupambana na wadudu wahribifu wa mazao ya kilimo na ni kiwatilifu kisichoo na kemikali ambapo kinyesi chake ni mbolea iliyo bora kwa mazao hasa mboga mboga na huisha udongo haraka na kurejesha uoto wa asili haraka.

Kwa upande mwingine nyama yake ni bora ambayo uaazwa kwa kilo moja sh.8,000, ambapo sungura mmoja anao uwezo wa kuzalisha sungura kati ya 60-100 kwa mwaka endapo atatuzwa vizuri na atampatia mfugaji kiasi cha sh. Milioni 1.4 – Milioni 2.4 na kwa kuwa ufugaji huu hufanywa kwa jozi yenye sungura jike 6 na dume moja, hivyo mfugaji atajipatia kipato cha Sh Milioni 8.6 hadi Milioni 14.4 kwa jozi moja kwa mwaka kama pato ghafi.
Kuhusu mradi wa kuku aina ya (super solomony), mradi huo utahusisha kumfuga kuku ambaye anatoa mazao ya kuku wa aina tatu, akiwemo kuku wa nyama(broiler), kuku wa kienyeji ajili ya supu na kupika pia mayai yenye kiini cha njano(yellow-york) ambayo pia hutotolewa.

Akizungumzia kuhusu mradi wa kilimo cha mchai chai, Afisa Utafiti wa kampuni hiyo, Selemani Boko alisema kuwa ekari moja ya mchai chai mbichi kwa ajili ya mafuta hutoa mavuno ya majani kilo 4,000 na majani makavu yaliyokaushwa kwa jua kilo 700, na ekari kwa moja kwa shamba moja litavunwa kwa misimu mitatu yenye mavuno 11 kwa mpando mmoja na kutoa faidi ya sh Milioni 4.8 kwa mwaka.
Katika mkutano wa hadhara wananchi wa kata hiyo walipiga nderemo, vigeregere na vifijo na kuupokea mradi huo ambapo wasio na vikundi vilisisajiliwa kuamua kukaa wakiongozwa na viongozi wao kuunda vikundi vya miradi hiyo, ambapo pia madiwani waliupokea mradi kwa kila kata ambapo kata zilizoko kwenye mwambao wa ziwa wamepewa mradi wa kilimo cha mchai chai na kata zingine ufugaji wa Sungura ambazo, baadhi ya kata ni Bwasi, Lusoli, Mugango, Bukumi-Busekela, Bukima, lifulifu,Nyakatende,Tegeruka na Nyegina

Aidha maamuzi ya fedha za mfuko wa jimbo pia yalifanyika katika kata hiyo,katika mkutano wa hadhara ambao pia uliwashirikisha madiwani wa halmashauri ya Musoma na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Vicent Naano kwa pamoja waliamua fedha za mfuko wa jimbo zinunue mbegu na mashine ya kukamua mafuta ya Alizeti.

Fedha za mfuko wa jimbo kiasi cha Sh. Milioni 38,347 zitanunua mbegu za Muhogo (Vipando) zipatazo 532,000 katika vijiji 68 yenye thamani ya Sh. Milioni 16, ambapo sh. Milioni 21.9 zitanunua mashine ndogo za kukamua mafuta ya Alizeti ambazo zitafugwa katika ofisi ya kata kwa afisa kilimo kila kata.

NYUMBANI KWA HAYATI MWALIMU NYERERE KUFANYIKA VIKAO VYA WABUNGE.





WABUNGE wa Mkoa wa Mara wakiwemo, wabunge wa afrika Mashariki wameamua kufanya kikoa cha kujadili maendeleo ya Mkoa nyumbani kwa hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere Mwitongo kijijini Butiama wilaya ya Butiama Mkoa wa Mara, kila mwaka ili kumuenzi Baba wa Taifa.

Kikao hicho kilifanyika siku ya sikukuu ya zawadi ya kuzaliwa Yesu kristo nyumbani Mwitongo kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika ukumbi uliondaliwa kwa ajili ya mazungumzo ambacho kilikuwa kinaongozwa na mwenyekiti wao ambaye ni Waziri wa Nishati na Madini Pro. Sospeter Muhongo.

Wabunge hao walisema umefika muda muafaka wa kuungana kwa pamoja na kuacha itikadi za vyama vya siasa pembeni ili kuweza kusimamia na kuendeleza shughuli za maendeleo kwa vitendo ili wananchi waondokane na umaskini na kujikwamua kiuchumi na mkoa huo uweze kusonga mbele .

Mbunge wa Jimbo la Mwibara Kangi Lugola akitoa maazimio yaliyoazimiwa kwa niaba wabunge hao alisema masuala waliyoweka kipaumbele ni pamoja na kusimamia vizuri kwa kushirikiana na serikasa hali yake sio nzuri na kuhakikisha hakuna mwananchi ambaye atakufa kwa njaa.
Aidha vipaumbele vingine vilikuwa ni ujenzi wa hospitali ya Kwangwa ambayo itaitwa Kwangwa hospital ya rufaa ambayo imetengewa Sh Bilioni 5.5 ambayo imepekezwa imalizike katika awamu hii ya uongozi wa Rais John Magufuli.

Aidha wabunge hao waliitaka Wizara ya Mali asili na Utalii kutenga uzio kwa ajili ya kutenganisha hifadhi ya Mbuga ya Serengeti na wananchi, ambapo wanyama aina ya Tembo wamekuwa wakivamia mashamba na kuhatarisha maisha wanadamu na kusabaisha njaa kali kwa wananchi.

Kuhusu michezo walisema kuwa michezo ni ajira, hivyo timu ya polisi Mara ambayo iko nyuma kimechezo itaimarisha ikiwa pamoja na michezo mingine kama riadha ambayo historia yake ya kuwa wakimbiaji kutoka Mkoa wa Mara imefutika.




Sunday, December 25, 2016

ASKOFU MSONGANZILA AHIMIZA AMANI.



JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI.


Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma Michael Msonganzila amewataka wananchi kuwa na Amani ambayo kila binadamu anapaswa kuenenda nayo kwani ukikosa amani hutaweza kupata nafasi ya kufanya shughuli za maendeleo.

Yameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya jimbo la Katoliki Dayosisi ya Musoma, kuwa kutokuwa na binadamu anapaswa kumpenda mwenzake kwa kujijengea moyo wa kusameheana,kupatana,kunyenyekeana katika uajibikaji wa shughuli za kijamii.

‘’Mwaka 2008 nilikuja kufanya kazi kama mtumishi katika kuhudumia wananchi wa Mkoa wa Mara katika shughuli mbalimbali za wananchi kwa kutoa elimu na malezi ili waweze kuwa tegemeo la nchi na lengo likiwa kudumisha Amani, ambaponimeweza kufanya juhudi katika miaka minane na kuhakikisha amani inapatikana katika Mkoa wa Mara,ambapo mapigano ya koo za waryachori na waryanchonka katika wilaya ya Tarime yamekwisha’’ Alisema Msonganzila.


Amesema wao kama taasisi ya dini wanaanzisha darasa maalum Nyegina Sekondari kwa mabinti wanaokimbia ukeketaji majumbani kwao ambapo watasoma kwa muda wa mwaka mmoja ikiwa ni kupigwa msasa kisha wataanza masomo kama kawaida.

Amesema kwa kufanya hivyo mabinti hao watakuwa mabalozi wazuri kwa wenzao na katika kijiji wanachotoka hivyo kusaidia kuepuka majanga kama ukeketaji.



Amesema kuna uwezekano wa wananchi kukumbwa na uhaba wa ukosefu wa chakula kutokana na hali ya hewa na mabadiliko ya tabia ya nchi hivyo ametoa wito kwa wananchi hususani wilaya ya Tarime kuacha tabia ya kuuza chakula nchini Kenya kwani, Serikali imekuwa ikigharamika tena kununua chakula nchini Kenya ambacho wananchi wa Tarime ukiuza.

Kuhusu mwenendo wa utendaji kazi wa Serikali ya awamu ya tano Askofu huyo alisema kuwa mwelekeo wa serikali kwa sasa umekuwa ni mtetezi wa haki kwa wananchi wanyonge ingawa wengine hawafurahii hali hiyo kutokana na kuzibiwa mianya huku mizizi ya rushwa ikithibitiwa kwa kiasi kikubwa.

MBUNGE WA JIMBO LA MUSOMA VIJIJIJI AWAASA WAUMINI WA KANISA LA MENNONITE.



MUSOMA.
MBUNGE wa Jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amewataka Waumini wa kanisa la Mennonite kata ya Nyakatende vijiji vya Nyakatende na Kamuguruki, kuachana na tabia za ugomvi bali wapendane ,waungane na kudumisha Amani kwa mujibu wa Imani ya Kikristo.

Mbunge huyo ambaye alijumuika na waumini wa kanisa hilo kusherehekea sikukuu ya kuzaliwa Yesu kristo karne nyingi zilizopita alisema kuwa si jambo jema kuendeleza ugomvi bali wawe pamoja kwa kuwa na upendo kama Yesu alivyokuwa hapa duniani.

Aliwataka kuachana na malumbano yasiyo na misingi bali wawe kitu kimoja na kufanya shughuli za maendeleo, hususani ujenzi wa shule, zahanati, nyumba za walimu na makanisa.

Aidha Mbunge huyo alimwagiza msaidizi wake kwa kanda ya Nyanja, Juma Shaban kufanya tathimini ya gharama za mahitaji ya ujenzi wa kanisa la Menonite la vijiji vya Nyakatende na Nyasurula .

Akiwa katika kijiji cha Kamuguruki alisema kuwa katika jimbo zima kuna upungufu wa vyumba vya madarasa shule za msingi na Sekondari vipatavyo 748, ambapo tayari makotena ya saruji na mabati yameagizwa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba hivyo.

Aidha amekabidhi vifaa vipatavyo 10 vya umeme wa jua vitavyotumika kwa ajili ya mwanga na kuchaji simu kwa ajili ya majaribio, ambapo mara baada kujaribishwa timu ya wataalamu kutoka korea watakuja kutoa elimu kwa vijana waliomaliza kidato cha Nne wa jimbo hilo kufundishwa ili waweze kupata utaalamu na ujuzi wa kuvitengeneza ambapo watajipatia kipato kutokana na uuzwaji wa vifaa hivyo kwa kila kifaa kiasi cha Sh.15,0000.

Akitoa ibada kwa waumini hao, Askofu wa Kanisa la Menonite, Dayosisi ya Mara na Mwanza(mstaafu), Jairo Onyengo aliwataka vijana wanawake na wanaume kutumia ujana wao vizuri,kwa kumkumbaka bikira Maria ambaye alipata ujauzito kwa njia ya roho Mtakatifu.

‘’Ni vijana wangapi na mabinti kwa sasa ambao unaweza kushuhudia kama bikira, na ndiyo maana ugonjwa wa Ukimwi unaendelea kuwepo kutokana na maadili yasiyo mpendeza mwenyezi Mungu,..Utii ni bora kama mafuta ya beberu aliongeza Askofu huyo.

Alisema sikukuu hii ni maalumu kwa kuomba na kumshukuru Mungu na si ilivyo sasa kwa walio wengi wakifanya mkesha kwa uasheretari kwenye madangulo wakiutafuta ukimwi na kulewa pombe na hata katika sikukuu yenyewe,bali Yesu alikuja kutukomboa ili tutubu na kuepukana na maovu.

WAZIRI wa Nishati na Madini ala chakula na wapiga kura wake.

JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI.


Waziri wa Nishati na Madini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo amekula chakula cha pamoja na wapiga kura wake katika kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo karne nyingi zilizopita katika kata ya Nyakatende Wilaya ya Musoma Vijini.


Mbunge huyo ambaye aliambatana na familia yake na rafiki zake kutoka Ujerumani walisali katika kanisa la Menonite la kata uya Nyakatende kabla ya kwenda katika kijiji cha Kamuguruki ambapo pia alisali na kupata chakula cha pamoja.



Hii ni mara ya kwanza kwa Mbunge kula chakula cha pamoja na wananchi hao tangu achaguliwe kuwa Mbunge, pia tangia kupatikana kwa Uhuru wa nchi hii.

Wednesday, December 14, 2016

WAIGIZAJI FILAMU MKOA WA MARA WANOLEWA.

WIZARA ya habari, utamaduni, sanaa na Michezo kupitia bodi ya Filamu Tanzania imetoa mafunzo kwa waigizaji wa filamu Mkoa wa Mara ya kuwajengea uwezo waigizaji wa filamu ili waweze kuendesha kazi zao kwa ufanisi zaidi.

Akifungua warsha hiyo ya siku tatu katika Shule ya Sekondari ya Mara, Kaimu katibu Mkuu, Wizara ya habari,Utamaduni, sanaa na michezo, Nuru Milao aliwataka kutumia mafunzo hayo kwa weredi mkubwa ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi na kuutangaza Mkoa wa Mara na vivutio vyake.

Alisema kuwa mafunzo hayo yatawajengea uwezo wadau hao ili waweze kuongeza pato lao na Taifa kwa ujumla kwa kuwa wakifanikiwa wataweza kulipa kodi ya maendeleo kwa Taifa lao.

Akitoa salamu za kumkaribisha mgeni, Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu, Joyce Fissoo alisema kuwa inashangaza kuona kuwa wachezaji wa filamu wengi wao nchini Tanzania wanaonyesha filamu za mapenzi peke yake bila kufanya utafiti wa kina na wakati kuna vivutio vingi vizuri nchini hapa ambavyo wanapaswa kuvionyesha katika filamu zao wawapo kazini.

Alisema kuwa kazi nyingi zinakataliwa kuruka hewani kutokana na mahudhuhi mabaya kwa mtanzania, ambayo kifamilia ambayo hayajengi bali kubomoa, kazi ambazo amesema kuwa huwa hawaruhusu kazi hizo zitolewa kwenye luninga.
“Kunataka kutambua kazi zenu kama zina ubora, hatutaki kuzuia, nia yetu ni kujenga ili kuwajengea uwezo nyie, ambapo mwaka jana filamu zipatazo 55 zilifanyiwa marekebisho” alisema Fissoo.

Naye Rais wa Shirikisho la filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba aliwataka waigizaj kufanya kazi kwa kujituma bila wasiwasi wa kuibia kazi zao, na kwamba Serikali imetoa fursa na haki ya kulinda kazi zao ili kila msanii aweze kuneemeka kupitia kazi yake.

Akitoa mada katika warsha hiyo, Mkufunzi kutoka Chuo Kikuu Dar es Salaam, Richard Ndunguru, alisema kuwa wasanii wanapaswa kuwa na uandishi wa Script iliyo bora ambayo inalenga uwe na wazo au msukumo ambao ndio msingi unaoweza kumjenga muandaaji na kwamba hadithi yake inapagwa katika mfumo wa namba ambapo mada zipatazo 11 zitazungumzwa.