JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI.
Waziri wa Nishati na Madini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo amekula chakula cha pamoja na wapiga kura wake katika kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo karne nyingi zilizopita katika kata ya Nyakatende Wilaya ya Musoma Vijini.
Mbunge huyo ambaye aliambatana na familia yake na rafiki zake kutoka Ujerumani walisali katika kanisa la Menonite la kata uya Nyakatende kabla ya kwenda katika kijiji cha Kamuguruki ambapo pia alisali na kupata chakula cha pamoja.
Hii ni mara ya kwanza kwa Mbunge kula chakula cha pamoja na wananchi hao tangu achaguliwe kuwa Mbunge, pia tangia kupatikana kwa Uhuru wa nchi hii.
No comments:
Post a Comment