MUSOMA.
WAMILIKI wa Filamu Tanzania wamepewa siku 90 za marekebisho ya filamu zao vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Agizo hilo limetolewa mbele ya Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharibu Bilal na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na michezo, Dk. Emmanuel Nchimbi, wakati wa uzinduzi wa kanuni za sheria ya filamu na Michezo ya kuigiza za mwaka 2011 zilizofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji wa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Alisema zipo filamu nchini Tanzania ambazo hazina maadili kwa watanzania na ni hatari kwa vizazi vijavyo.
Aliongeza kuwa Serikali baada ya kutumia Sheria ya picha za sinema(Ordinance Cap 230) kwa takribani miaka 46 iliona kuna umuhimu wa kuwa na sheria inayoilenga mazingira na hali halisi ya kitanzania,hivyo ikaona umuhimu wa kutunga Sheria mpya, yaani Sheria ya Filamu na Michezo ya Kuigiza Na.4 ya mwaka 1976 yenye ni ya kuulinda utamaduni wa kitanzania na kuhakikisha Watanzania wanapata hurudani stahiki zinazofuata taratibu zilizowekwa na zinazozingatia maadili.
Akizindua kanuni hizo, Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Bilal alisema kuwa alisema Serikali inadhamini na kutambua mchango unaotokana na tasnia ya filamu,ambapo Rais Jakaya Kikwete wakati anahutubia Bunge alizungumzia dhamira yake ya dhati katika kuimarisha tasnia hiyo ya filamu.
Pia serikali kupitia bajeti yake ya mwaka 2009/2010. Ilitoa unafuu kwa kupunguza kodi katika uingizaji wa vifaa kama kamera kwa ajili ya kutrngrnrza filamu ili kuwapatia ajira wasanii wa tasnia hiyo na hatimaye waweze kuchangia na kukuza Uchumi,sanjali na kuandaa sera, Sheria na miongozi inayosimamia tasnia hiyo.
Alisema kuwa kanuni hizo zilizozinduliwa zinawakumbusha wadau wa Filamu na michezo ya kuigiza kwamba tasnia hiyo inasimiwa na Sheria na kwamba hamna budi kuhakikisha filamu na Michezo ya kuigiza zinazotengenezwa nchini nza zinazoingizwa toka nje ya nchi zinawiana na mila, desturi na maadili ya Tanzania.
“Lakini nikiri pia zipo filamu na michezo ya kuigiza ambazo kwa kweli zinalinda maadili, zinatangaza nchi yetu na zinatoa pato kwa wasanii, lakini ni chache sana,na kazi nyingi za filamu na michezo ya kuigiza hziwanufaishi kw akiwango stahili,wasanii wa tasnia hio wala kuliingizia Taifa pato stahiki,hivyo wadau wa filamu hawana budi kuhakikisha kazi zao zina viwango vya hali ya juu na zinachangia katika kumkomboa na kumpa msanii pato stahuki na zinachangia pato la Taifa” Alisema Gharibu.
Aidha akitoa mfano wa nchi ya Marekani, Makamu wa Rais,Dk. Mohammed Gharibu Bilal alisema wasanii wa nchi hiyo wanachangia pato la Taifa kwa fani za muziki na filamu kwa kiasi kikubwa,ambapo India iko katika kundi la nchi zinazoendelea.
Tasnia ya Filamu na Televisheni huiingizia zaidi ya Dola Bilion 6.1 na imetoa jumla ya ajira 571,000 mwaka 2008,huko Uingereza ikiingiza zaidi ya paundi 4.5 Bilioni takribani Sh. trioni 9 katika uchumi wa nchi hiyo,hata Tanzania inawezekana endapo fursa zilizopo zitatumika vizuri.
Aidha amemwagiza Wzairi huska kuhakiksiha inaimarisha Bodi kuu ya filamu, Bodi za Mikoa na Wilaya kw akushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), na kuhakikisha kanuni zilizozinduliwa zinawafikai wahusika wote na kupanga namna ya kuzitekeleza mapema ili zitoe matokeo chanya katika jamii na Taifa kwa ujumla.
Uzinduzi huo ulihudhuriw na viongozi mbalimbali wa Serikali, akiwemo, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fennella Mukangara, Mkuu wa Mkoa wa Mra John Tupa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Sethi Kamuhanda, Mwenyekiti wa Bodi ya filamu, Rose Sahoye na watumishi wa Wizara na Asasi zake.