Saturday, October 22, 2011

KAMPUNI YA SIMU TANZANIA YAHUJUMIWA.

MUSOMA.



KAMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL) Mkoa wa Mara imehujumiwa kwa kukatiwa mikongo ya simu yenye urefu wa Mita 4,000 na wananchi wasio wema na kusababisha hasara kubwa ya Mamilioni ya fedha kwa kipindi cha miezi sita.

Akizungumza kwa masikitiko makubwa na Mwandishi wa habari hii ofisini kwake wakati wa mahojiano, Meneja wa kampuni hiyo, Richard Augustine alisema ingawaje kampuni inajitahidi kutoa huduma nzuri kwa wakazi wa Mji wa Musoma na Tarimr lakini inakubiliwa na changamoto mbalimbali.

Alisema kwa sasa wakazi wa kata za Bweri machinjioni na Rwamlimi na Wilani Tarime ambao wanakosa huduma hiyo muhimu majumbani kwao kutokana na tatizo hilo ambalo limeipatia kampuni hasara ya kiasi cha Sh Milioni 50.

Aliongeza kuwa ukaratabati wa miundo mbinu ya kupitisha maji, barabara imekata baadhi ya mikongo maeneo ya kiwanda cha Nguo cha Mutex suala ambalo linashughulikiwa ili kiwanda hicho kiweze kuendelea kupata huduma.

“Suala hili la ukarabati wa barabara na upitishaji maji ni lazima tuwe tunashirikiana ili kuepuka gharama zingine zisizo za lazima, pia suala la ushirikiano baina ya vyombo vya dola na kampuni yetu ni jambo la msingi sana ili kuhakikisha vitendo vya namna hii vinatokemea,kwani wahujumu hawa wanafahamika na wengine tumekuwa tukiwakamata na ni wezi sugu wanafahamika”Alisema Richard.

Akizungumzia kuhusu kutanua wigo wa mtandao alisema kampuni ina mkakati huo kwani kwa sasa huduma ya simu ya mkononi ya TTCL Mobile haifiki maeneo mengi ukilinganisha na kampuni zingine, sanjali na mtandao wa Broad band ambao kwa sasa watumiaji wengi wamekuwa wakifahidika nayo.

Akizungumzia juu ya kupanda kwa gharama za umeme alisema gharama zimekuwa kubwa kulinganisha na awali ambapo huduma hiyo ilikuwa ikipatikana,haipungui japo kuwa kuna mgao na kwa maeneo mengine yameathiri utendaji kwa kampuni hiyo, kutokana na matumizi makubwa ya mafuta kwenye generator, huku Ankara pia zikipanda.



“Nilifikiri gharama zitapungua kutokana na mgao wa umeme,lakini cha ajabu tumekuwa tukitumia mafuta kwa wengi tukijua Ankara za Tanesco zitapungua lakini imekuwa kinyume zinakwenda sambamba” Alisema Richard kwa mshangao.


No comments:

Post a Comment