MUSOMA.
JUMLA ya noti bandia zipatazo 16 za Sh 10,000 na Sh. 5,000 zipatazo 12 zimekamatwa katika Manispaa ya Mji wa Musoma.
Akizungumza na Mwandishi wa habari hii ofisini kwake Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP), Mkoa wa Mara, Robert Boaz alisema tukio hilo limetokea Agosti 24 mwaka huu katika mtaa wa Jamatini majira ya saa 2 usiku katika Super Market ya Msendo wakati mteja akinunua vocha ya Sh.5,000.
Alisema baada ya kuugundua si noti halali alipiga simu kwa askari wa doria na kumkamata mtuhumiwa aliyemtaja kuwa Mashaka Samson, mkazi wa Musoma Mjini mtaa wa Karume.
Kamanda Boaz alisema noti hizo zilikuwa na namba tofauti tofauti ambapo noti zipatazo nane za Sh.5,000 zilikuwa na namba aina moja AA 084 598 na nne zikiwa na namba ADO 845 927, noti za 10,000 zilikuwa nne , tatu zikiwa na namba BB 0315203 na moja ikiwa na namba BC 031 5209.
Mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani kujibu mashitaka.
No comments:
Post a Comment