Saturday, October 8, 2011

MASWALI YA MAMA MARIA NYERERE

YAFUATAYO NI MASWALI YA KUMUULIZA MAMA MARIA NYERERE:

1-Oktoba 14 mwaka huu, Tanzania itaadhimisha miaka 12 tangu kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Unapenda kuwaeleza nini
Watanzania kuhusu siku hii.

2- Unadhani inatosha kwa watanzania kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa kuwasha mwenge Butiama ama kuandaa makongamano?

3- Binafsi unayaonaje maisha bila ya kuwa na Mwalimu Nyerere?

4- Ni changamoto zipi ulizowahi kukumbana nazo ukiwa mke wa rais?

5-Unadhani ni kwa nini Mwalimu Nyerere aliwalea watoto wake sawa na watoto wengine wa Kitanzania wakati ambapo
kwa madaraka aliyokuwa nayo, angeweza kuwapeleka nje kusoma ama wangeishi kifahari sana?

6-Ni kwa nini Mwalimu Nyerere hakujihusisha kabisa na biashara ama kujilimbikizia mali katika kipindi chote
alichokuwa madarakani hadi alipostaafu urais?

7- Ni kwa nini wewe binafsi katika kipindi chote cha uongozi wa Mwalimu Nyerere hukutaka kuanzisha taasisi ya mke wa
rais kama ilivyo kwa wake wengine wa marais duniani?

8- Ni kitu gani kilichowahi kumchukiza sana Mwalimu Nyerere katika maisha yake?

9-Na ni kipi ambacho kiliwahi kumfurahisha, iwe akiwa madarakani au hata baada ya kustaafu?

10-Wewe binafsi ni tukio lipi, ambalo liliwahi kukuhuzunisha katika maisha yako? Na tukio lipi liliwahi kukufurahisha?

11-Tanzania inaelekea kutimiza miaka 50 ya uhuru. Wapo wanasiasa wanaobeza kwamba hakuna chochote
kilichofanyika kuiletea nchi maendeleo. Unasemaje kuhusu kauli hizi?

12- Una maoni gani kuhusu siasa ya vyama vingi hapa nchini? Unadhani vinaisaidia serikali katika kuendesha mambo yake
ama vinaweza kuhatarisha amani, umoja na mshikamano miongoni mwa watanzania?

13- Nini maoni yano kuhusu matukio ya vurugu, ambayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara wakati wa chaguzi
ndogo za ubunge na udiwani?

14- Tanzania imetoa wanawake wengi katika ngazi za uongozi, kitaifa na kimataifa. Unadhani wakati wa Tanzania kuwa
na rais mwanamke umewadia?

15- Unatoa mwito gani kwa wanawake wa Tanzania, hasa wale waliojitosa katika masuala ya siasa ama kupewa
nafasi za juu za uongozi?

No comments:

Post a Comment