MUSOMA.
MTOTO Mchanga wa jinsia ya kike anayekadiriwa kuwa wa wiki mbili ,Agosti 25 ameokotwa akiwa ametupwa kwenye korongo katika Mtaa wa Mtakuja na Zanzibar, kata ya Mwisenge,kikiwa kimetupwa na mtu asiyejulikana.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Kamishina Msiadizi wa Polisi (ACP),Robert Boaz alisema kuwa mtoto huyo amegunduliwa na watoto wa shule ya Msingi wa Tatu Issa (32) walipokuwa wakipita kwenye korongo hilo wakielekea shuleni na ndipo waliporudi nyumbani kumpatia taarifa Mama yao.
Alisema Mama huyo alimkuta mtoto huto akiwa mtupu na alikuwa hai ,ndiopo alipotoa taarifa kwa Polisi,mtoto huyo amehifadhiwa katika hospitali ya Mkoa wa Mara iliyoko katika Manispaa ya Musoma.
Aidha ametoa wito kwa watu ambao wanahisi kuna mama alikuwa mjazito na hana ujauzito watoe taarifa kituo cha Polisi ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.
Katika tukio jingine lililotokea katika wilaya ya Bunda, majira ya saa 10 jioni stend ya Mabasi, mtoto mchanga wa jinsia ya kiume wa Chausiku Kelaryo( 21), mwenye umri wa wiki moja na nusu ameibiwa.
Alisema Chausiku alimwachia Mama mmoja asiyemfahamu kumshikia ili akanunue mboga sokoni, kutoka sokoni akakuta mama huyo ametoweka na mwanae.
Ametoa wito kwa wakazi wa Wilaya hiyo kama kutakuwa na utata juu mama huyo na kwamba hakuwa na ujauzito watoe taaifa kituo cha Polisi ili hatua dhidi ya mama huyo zichukuliwe.
No comments:
Post a Comment