Thursday, May 31, 2012
SAKATA LA KUMKATAA DC TARIME LAGONGA MWAMBA
SAKATA LA KUMKATAA DC TARIME LAGONGA MWAMBA
TARIME.
SAKATA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya Tarime Mkoani Mara la
kumkataa na kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete kumwondoa Ukuu wa Wilaya,
Mkuu wa Wilaya John Henjewele limeingia sura mpya baada ya madiwani
kugawanyika wengine wakitaka aondolewe na huku wengine wakiomba apewe
muda wa kujibu tuhuma zinazomkabili.
Licha ya kuwa kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichopita Mei 08
2012 madiwani wa CCM pamoja na wa kambi ya upinzani waliungana pamoja
kujenga hoja ya kutaka Henjewele kuondolewaTarime,kwenye kikao
kilichofanyika Mei 30 ambapo baada ya hoja hiyo kugusiwa na madiwani
toka kambi ya upinzani iliwagawa madiwani ambapo madiwani toka CCM
waliwageuka wale wa Chadema.
Kwa hali hiyo Madiwani wakambi ya upinzani walijikuta wanaingia wakati
mugumu walipojaribu kukumbushia msimamo wao wa maazimio ya kikao
kilichopita ambapo madiwani wote kwa pamoja walikuwa na kauli moja ya
kumkataa Henjewele,CHADEMA walijikuta CCM wanawageuka kwa madai kuwa
hoja hiyo haikuja kwa wakati mwafaka.
Kufuatia utata huo ambao ulisababisha kikao kuonyesha hali ya
kutokalika na malumbano ya kwa baadhi ya madiwani hasa wa kambi ya
upinzani huku wakitishia kususia kikao na kujigeuza kuwa kamati hali
ambayo ilimlazimu, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Fidelis Lumato
kusoma kanuni namba 17 yenye kumpat fursa Mwenyekiti kumwondoa Diwani
yeyote anaye leta fujo ndani ya kikao kwa kumtaja kwa jina ili
achukuliwe hatua ikiwa ni pamoja na kutolewa nje ya kikao na
kutohudhuria vikao vitatu mfululizo katika baraza hilo, hali iliyo
leta utulivu nakuendelea na kikao.
Sagara alilazimika kuwa mkali baada ya kanuni kusomwa kuwa anaye kiuka
utaratibu na kuvuruga kikao lazima awajibishwe kwa mjibu wa kanuni
ambapo sagara alitishia madiwani mawili toka kambi ya upinzani kutoka
nje ya kikao kwa kuwa wanaonekana kuvuruga kikao baada ya hapo Diwani
Mang'enyi Ryoba toka kata ya Nyanungu(Chadema) kuwatetea wenzake
kuwa awasamehe ilikuendelea na kikao na kwamba ni changamoto kwao,
ambapo Mwenyekiti aliridhia ombi hilo na kuwasamehe ili kuendelea na
kikao.
Aidha kwa kuhitimisha mjadala huo ulioleta utata huku baadhi ya
madiwani toka kambi ya upinzani wakisimama bila ruksa ya Mwenyekiti
midhili ya nyumbu, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Amosi Sagara
aliwataka Madiwani kufuata utaratibu kwa kuunda kamati itakayo kwenda
kwa Mkuu wa Mkoa John Tuppa ili wapate majibu kuhusiana na maazimio
ya kikao kilicho pita .
Awali Madiwani hao waligomea kikao kilichopita kwa kumtuhumu Mkuu wa
wilaya John Henjewele kuwa ameshindwa kuondoa kizuizi cha polisi
kilichopo kijiji cha Magena kwa madai kuwa hakina msaada wowote na
wananchi.
kikao hicho kilihusu ripoti ya ukaguzi wa hesabu za Serikali na
kupitia miradi ya mwaka wa fedha ya mwaka 2010/2011.
TARIME.
SAKATA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya Tarime Mkoani Mara la
kumkataa na kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete kumwondoa Ukuu wa Wilaya,
Mkuu wa Wilaya John Henjewele limeingia sura mpya baada ya madiwani
kugawanyika wengine wakitaka aondolewe na huku wengine wakiomba apewe
muda wa kujibu tuhuma zinazomkabili.
Licha ya kuwa kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichopita Mei 08
2012 madiwani wa CCM pamoja na wa kambi ya upinzani waliungana pamoja
kujenga hoja ya kutaka Henjewele kuondolewaTarime,kwenye kikao
kilichofanyika Mei 30 ambapo baada ya hoja hiyo kugusiwa na madiwani
toka kambi ya upinzani iliwagawa madiwani ambapo madiwani toka CCM
waliwageuka wale wa Chadema.
Kwa hali hiyo Madiwani wakambi ya upinzani walijikuta wanaingia wakati
mugumu walipojaribu kukumbushia msimamo wao wa maazimio ya kikao
kilichopita ambapo madiwani wote kwa pamoja walikuwa na kauli moja ya
kumkataa Henjewele,CHADEMA walijikuta CCM wanawageuka kwa madai kuwa
hoja hiyo haikuja kwa wakati mwafaka.
Kufuatia utata huo ambao ulisababisha kikao kuonyesha hali ya
kutokalika na malumbano ya kwa baadhi ya madiwani hasa wa kambi ya
upinzani huku wakitishia kususia kikao na kujigeuza kuwa kamati hali
ambayo ilimlazimu, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Fidelis Lumato
kusoma kanuni namba 17 yenye kumpat fursa Mwenyekiti kumwondoa Diwani
yeyote anaye leta fujo ndani ya kikao kwa kumtaja kwa jina ili
achukuliwe hatua ikiwa ni pamoja na kutolewa nje ya kikao na
kutohudhuria vikao vitatu mfululizo katika baraza hilo, hali iliyo
leta utulivu nakuendelea na kikao.
Sagara alilazimika kuwa mkali baada ya kanuni kusomwa kuwa anaye kiuka
utaratibu na kuvuruga kikao lazima awajibishwe kwa mjibu wa kanuni
ambapo sagara alitishia madiwani mawili toka kambi ya upinzani kutoka
nje ya kikao kwa kuwa wanaonekana kuvuruga kikao baada ya hapo Diwani
Mang'enyi Ryoba toka kata ya Nyanungu(Chadema) kuwatetea wenzake
kuwa awasamehe ilikuendelea na kikao na kwamba ni changamoto kwao,
ambapo Mwenyekiti aliridhia ombi hilo na kuwasamehe ili kuendelea na
kikao.
Aidha kwa kuhitimisha mjadala huo ulioleta utata huku baadhi ya
madiwani toka kambi ya upinzani wakisimama bila ruksa ya Mwenyekiti
midhili ya nyumbu, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Amosi Sagara
aliwataka Madiwani kufuata utaratibu kwa kuunda kamati itakayo kwenda
kwa Mkuu wa Mkoa John Tuppa ili wapate majibu kuhusiana na maazimio
ya kikao kilicho pita .
Awali Madiwani hao waligomea kikao kilichopita kwa kumtuhumu Mkuu wa
wilaya John Henjewele kuwa ameshindwa kuondoa kizuizi cha polisi
kilichopo kijiji cha Magena kwa madai kuwa hakina msaada wowote na
wananchi.
kikao hicho kilihusu ripoti ya ukaguzi wa hesabu za Serikali na
kupitia miradi ya mwaka wa fedha ya mwaka 2010/2011.
HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME YATAKIWA KUONGEZA VYANZO VYA MAPATO
HALMASHAURI ya Wilaya ya Tarime Mkoa wa Mara, imetakiwa
kuongeza vyanzo vyake vya mapato ili iweze kujitosheleza yenyewe katika sehemu
kubwa ya matumizi si ya kutegemea ruzuku toka serikalini.
Akiwasilisha taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali (CAG) kuhusu taarifa ya fedha za halmashauri ya Wilaya ya Tarime
kwa mwaka wa fedha uliouishia Juni 30 2011 Mkaguzi Mkazi Msaidizi Mkoa wa Mara,
Deogratius Waijaha alisema kuwa asilimia 91.4 ya halmshauri inategemea ruzuku
kuu, hivyo lazima ianzishe na kubuni mipango ya kuifanya ijitegemee na sio
kutegemea ruzuku kutoka Serikali kuu.
Waijaha alisema kuwa mapato ya ndani ambayo ni Sh. Bilioni
1,503,489,981 ni madogo sana
ukilinganisha na ruzuku inayopewa halmashauri kutoka Serikali kuu ya kiasi cha
Sh. Bilioni 20, 960, 601,198.
Kwa upande wa matumizi ya kawaida alisema kuwa halmashauri
ilitumia kiasi ch Sh. 17,604,608,018 kwa matumizi ya kawaida wakati ambapo mapato
yake ya kawaida yalikuwa Sh. Bilioni
18,238,072,617 ikionyesha kwamba kulikuwa na Balance ya Sh. 633,
464,599.
Mkaguzi huyo alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2010/2011
halmashauri ilikusanya Jumla ya Sh. 1,503,489,981 kutoka katika vyanzo vyake
ukilinganisha na bajeti yake ya Sh. 1,263,405,000 na kusababisha makusanyo
zaidi ya Sh. 240,084,981 yakiwa sawa na asilimia 19.
Maeneo ya faini na tozo yalibajetiwa kukusanya kiasi cha Sh.
583,405,00 lakini kiasi kilichokusanya
kilikuwa Sh. 549,769, 083 ikiwa na upungufu wa Sh. 33,635, 916 sawa na 5.8 ambapo kodi ya ndani
ilibajetiwa kiasi cha Sh. 680,000,000 lakini kiasi kilichokusanywa kilikuwa na
Sh. 868,036,449 ikiwa ni ongezeko zaidi
ya Sh. 188, 036,449 ikiwa ni sawa na asilimia 27.7
Mkaguzi Waijaha alisema kuwa halmashauri imepata hati
inayoridhisha ambapo aliipongeza kwa kusimamia vyema rasilimali na fedha za
halmashauri na kwamba hali ya fedha ya halmashauri hadi Juni 30 2011 na kwamba
matokeo ya utendaji na mapato halisi kwa mwaka ulioishia inawiana na viwango
vya kimataifa vya uandaaji wa hesabu za fedha kwa sekta ya Umma.
Pia alisema katika manunuzi yenye jumla ya Sh. 32,050,000
yaliyokusanywa kupitia programu ya maendeleo ya kilimo (ASDP) yalikiuka kanuni Na.
49 ya manunuzi ya umma ya mwaka 2005 kwa kununua vifaa huska katika kiasi
kidogo kidogo kupitia hati mbalimbali za malipo badala ya kufuata taratibu za
Zabuni kama ilivyokuwa ikihitajika na
kanuni husika.
Tuesday, May 29, 2012
WANANCHI WATAKIWA KUJUA SHERIA YA PAROLE
MUSOMA
WANANCHI wa Mkoa wa
Mara, wametakiwa kufahamu utaratibu wa kisheria wa wafugwa wenye kifungo kirefu
wanaoonyesha mwenendo mzuri wa kurekebika wawapo Magereza (PAROLE), na kumaliza
kifungo chao wakiwa nje ya gereza na si kuwakataa.
Hayo yalisemwa Mei 29 Mwaka huu katika uzinduzi wa Bodi ya Parole, Afisa
Mwandamizi Afisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Buhacha Kichinda alipokuwa anazindua
bodi hiyo yenye jukumu la kupitia majalada ya wafugwa wenye nidhamu wawapo
katika vifungo vyao magerezani.
Alisema hiyo ni changamoto kubwa inayowakabili wafugwa
wanaoachiwa kwa sheria ya Parole kukataliwa na wananchi wanapotakiwa kumalizia
kifungo chao wakiwa majumbani mwao, jambo ambalo lilikuwa kikwazo kwa utekelezaji
wa sheria hiyo.
Aliongeza kuwa elimu inahitaji kwa wananchi juu ya umuhimu
wa Parole kwa kushirikiana na viongozi wa Serikali ili wananchi waweze
kushirikiana nao kwani wamekuwa tayari wamehakikiwa kuwa wana tabia hivyo na
wengi kujishughulisha katika majukumu
mbalimbali ya ujenzi wa Taifa kwa kujishughulisha na kilimo, ufugaji, uvuvi
na biashara ndogo ndogo.
Ameitaka bodi hiyo kufanya kazi za uchunguzi wa majalada kwa
kina ili wafugwa hao wanapokuwa na kifungo cha nje wasifanye uhalifu tena na
kusababisha kutoaminiwa kwa bodi.
Awali akisoma taarifa ya Parole, Mkuu wa Magereza Mkoa (RPO), Melchadus Mwendwa alisema kuwa
ofisi yake imekuwa na changamoto mbalimbali za kufuatilia taarifa muhimu za
kukamilisha majalada ya wafugwa wanaopekezwa kuachiliwa ikiwa ni pamoja na
upatikanaji wa nakala za hukumu toka Mahakamani,taarifa za uhalifu za awali
toka jeshi la polisi,ufinyu wa bajeti na uelewa mdogo wa Sheria ya Parole kwa
viongozi wa vijiji/mitaa anapochagua kuishi mfugwa.
Alisema kuwa kati ya wafugwa 268 wafugwa 10 tu waliovunja masharti wengi wao
wakitenda makosa mengine ya jinai na kuwalazimu kurudishwa gerezani kwa mujibu
wa sheria na wafugwa wapatao 40
wakiendelea na vifungo vyao chini ya utaratibu wa Parole wakiwa katika mitaa na
vijiji walipochagua kuishi na wafugwa
wapatao 219 tayari wamemaliza vifungo vyao chini ya utaratibu huo.
Sheria ya Bodi ya Parole N0. 25/1994 na marekebisho yake No.
5/2002, kanuni za bodi ya Parole No. GN 563/1997 vilianza kutumika mwaka 1999
na kwa mujibu wa kifungu cha 3(3) cha Sheria ya Bodi za Parole kinaidhinisha
ziundwe Bodi za Parole Mikoa ambayo kwa Mkoa wa Mara zilizinduliwa Mei 29
ambayo kazi zake ni kupitia kila jalada
la mfugwa lenye vielelezo vinavyojitajika toka sehemu mbalimbali,
aliyependekezwa kuachiliwa kwa Parole na kuthibitisha viwango vya sifa za
mfugwa ili akubalike.
Aidha kati ya majalada ya wafugwa wapatao 321 yaliyopekezwa
na Bodi ya Parole Mkoa wa Mara tangu utaratibu huo uanzishwe ni majalada 22 tu
ambayo bado yapo kwenye Bodi ya Parole Taifa yanayofanyiwa mchakato wa
kuyapeleka kwa Waziri huska ili ayatolee uamuzi idadi ambayo hairidhishi.
Wednesday, May 23, 2012
DC TARIME ADAIWA KULIDHALALISHA KANISA
Dinna Maningo, Tarime.
MCHUNGAJI wa Kanisa la
Pentecostal Evangelistic Fellowship Africa(PEFA) Tawi la Gonsarara Kijiji cha
Kewanja Kata ya Kemambo-Nyamongo Wilayani Tarime Elia Magutu amewataka viongozi
wa Serikali kutumia hekima na kauli za busara pindi wanapohutubia wananchi
kupitia mikutano ya hadhara.
Kauli hiyo imekuja baada ya
mchungaji Magutu kudai kuwa hivi karibuni May 3 Mkuu wa Wilaya John
Henjewele akiwa anahutubia wananchi wa kitongoji cha Gonsarara kijiji cha
Kewanja alidaiwa kulikashifu kanisa na kusema kuwa kanisa la PEFA halipo
kihalali bali limeibuka na kuanzishwa kwa lengo la kufanyiwa tathimini ya
malipo katika zoezi linaloendeshwa na
mgodi wa Dhahabu wa North Mara unaoendelea na tathimini kwa ajili ya
kuwahamisha wananchi wanaoishi jirani na mgodi wa dhahabu kitongoji cha
Gonsarara.
“Ilikuwa tarehe 3 May Mkuu wa Wilaya Henjewele akiwa katika
mkutano wa hadhara Gonsarara akiwa anazungumzia tathimini alisema kuwa kuna
watu wamekuja kutoka Mwanza na
kujenga nyumba ili nao wafanyiwe tathimini na mgodi wakati
anaendelea na maongezi alisema kuna Kanisa limeibuka la kitapeli lisilojulikana
na limetegeshwa ili nalo lifanyiwe tathimini ya malipo kauli hiyo ilitushangaza
kwa sababu katika hicho kitongoji kuna kanisa moja tu ambalo ni kanisa la
PEFA moja kwa moja ndilo alilokuwa
analilenga”alisema Magutu.
Mchungaji Magutu alikanusha
madai ya Mkuu wa Wilaya Henjewele la kuibuka kwa kanisa ambapo alisema kwa
kuonyesha vielelezo mbalimbali kuwa kanisa hilo lipo kwa muda mlefu tangu mwaka 1996 na
kwamba kauli hiyo ni kulizalalisha kanisa.
“Hili kanisa halijajengwa leo
limeanzishwa toka mwaka 1996 wakati huo tukiwa tunasali shuleni
Nyabigena-Kewanja ilipofika mwaka 2002 tukanunua eneo Gonsarara tukajenga
nyumba ya nyasi kulingana na uwezo mdogo tuliokuwa nao wakati huo tukaendelea
kusali likiwa linaongozwa na mzee wa kanisa aitwae Dishon Ghati baadae
tukajenga nyumba ya bati na sasa tunaendelea na ukarabati na kanisa ambalo hadi
sasa lina zaidi ya waumini 100”alisema Mchungaji.
Mchungaji huyo alisema kuwa
amesikitishwa na kauli hiyo ya Dc Henjewele na kumtaka aliombe radhi kanisa kwa
madai kuwa amelidhalalisha na kulikasfu hadharani bila kujua kwa undani
historia ya kanisa hilo
la PEFA.
“Kama Dc alikuwa na mashaka
na kanisa alipaswa afike kanisani aonane na uongozi wa kanisa tumweleze
historia ya kanisa siyo kuongea hadhalani kitu asichokijua,kanisa lipo kwenye
eneo halali tunamuomba achunguze kwa undani zaidi na hatuna sababu yoyote ya
kuhamishwa na wala hatujaomba mgodi utuamishe kama mgodi umeona kanisa lipo
jirani na mgodi na kunahaja ya kuamishwa kwa shuguli zao ni maamuzi yao
wenyewe”alisema
Aliongeza” Sisis hatuna
taarifa yoyote wala barua kuwa mgodi unataka kufanya tathimini kanisa na
kuliamisha na itambulike kuwa kanisa la PEFA
ni taasisi inayotambulika lina haki ya kujiendesha kikanisa,kuboreshwa
kwa kanisa Dc anasema tunafanya hivyo kwa ajili ya malipo ya kuhamishwa! Je
toka tathimini imeanza ni kanisa lipi ambalo limefanyiwa tathimini? Hakuna.
Mchungaji Magutu alisema kuwa
kutokana na kauli ya Dc Henjewele huwenda ikaathili waumini kwa kudhani kuwa halikuwa kanisa bali lipo
kwa ajili ya kutafuta masalahi binafsi ambapo pia aliwataka waumini kuendelea
kusali na kumtumikia Mungu nakwamba wasikatishwe tamaa na kauli ya Henjewele.
Mwenyekiti wa kanisa la PEFA
Wilaya ya Mashariki Tarime Mchungaji Samson Msabi alithibitisha kuwepo kwa
uhalali wa kanisa hilo
ambapo alisema aliliweka wakfu mwaka 2008.
Pia Mwenyekiti wa Kijiji cha
Kewanja ambako ndiko kuliko na kanisa hilo
Tanzania Omtima( Chadema) alithibitisha kuwepo kwa kanisa ambapo alisema
analitambua kutokana na kuwepo kijijini kwake kwa muda mlefu.
Mkuu Wa Wilaya ya Tarime John
Henjewele alipoelezwa tuhuma hizo dhidi yake alikili kuwepo kwa kanisa hilo
nakusema siyo kanisa halali nakwamba
limeibuka na kutegeshwa kwa lengo la kufanyiwa tathimini na mgodi na kwamba
ameliona hilo kanisa kwa macho yake ambalo alisema halijui jina la kanisa
kwakuwa kanisa hilo halijaandikwa jina.
MADIWANI WAWASHIKIA WATENDAJI
RORYA.
MADIWANI wa Halmashauri ya
Wilaya ya Rorya Mkoani Mara wamemtuhumu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya
Rorya, Daniel Chacha kutumia fedha vibaya zinazotolewa na Halmashauri kwenda
katika vituo vinavyotoa huduma ya afya kwa ajili ya kununua vifaa,dawa na
mahitaji mengine huku akidaiwa kutofikisha baadhi ya vifaa kwenye vituo.
Hayo yalibainishwa katika
kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika jana ambapo Madiwani walisema kuwa
kuna baadhi ya wakuu wa idara wamekuwa wakitumia vibaya fedha za Serikali
ambapo walisema kuwa kuna fedha ambazo zilitolewa kwa ajili ya miradi ya
maendeleo lakini hazitumiki ipasavyo.
Diwani wa kata ya Kyango’mbe
Emanuel Manyama,(Matongwe) CCM alisema kuwa kuna kiasi cha fedha Milioni 20
zilitengwa kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Bitiryo lakini fedha
zilizoingizwa kwenye akaunti si kiwango
kamili kilichotolewa na Halmashauri.
“Kuna ndume tatu ambazo ni
tatizo kwenye Halmashauri DMO,DT na Mhandisi wa maji hawa watu ni wala fedha
kijiji cha Bitiryo zilitengwa Milioni
20 kwa ajili ya ujenzi cha kushangaza
fedha zilizoingizwa kwenye akaunti ya kijiji ni Milioni 17 tu Milioni 3
hazionekani zimebaki Halmashauri lakini
hapa kwenye kablasha naambiwa milioni 20 ziliingizwa kwenye akaunti ya kijiji
na zimetumika kujenga zahanati na wakati ni Milioni 17 zilizowekwa kwenye
akaunti naomba nielezwe hizo pesa zingine zimekwenda wapi na kwanini
hazikuwekwa kwenye akaunti”alisema Manyama.
Diwani wa viti maalumu Tarafa
ya Nyancha Pendo Odero CCM aliongeza kwa
kusema kuwa Mganga mkuu Chacha anatuhumiwa kwa kutofikisha fedha za vifaa na
dawa kwenye baadhi ya vituo vya afya nakwamba baada ya kufahamu tuhuma hizo alianza
kuwahamasisha wanafunzi kumfichia siri ya kutofika kwa fedha za vifaa.
“DMO kala pesa za Halmashauri
za kununua vifaa na hata dawa zilizotolewa kusambazwa vituoni hazijafika baada
ya yeye kugundua mambo yameharibika alichukuwa gari kwenda kuwahamasisha
watumishi na kuwadanganya waseme pesa na vifaa vimefika lakini mipango yake
ikavunjika akiwa safarini taarifa zikafika kwa mkurugenzi na Mwenyekiti wa
Halimashauri wakazyuia gari na kumtaka astishe zoezi hilo”alisema Odero.
Diwani wa kata ya Mirare
Peter Ayoyi( CCM),alilalamikia Madiwani kutopatiwa vitambulisho vya Bima ya
afya licha ya kuwa tayali walishatoa
fedha za malipo ya vitambulisho.
“DMO atueleze hatima ya
vitambulisho vyetu vya bima ya afya Madiwani tumeshalipa pesa 3,000 kwa kila
Diwani ambapo 3,000 zingine kwa kila Diwani,
Halmashauri inachangia jumla kila Diwani ni 6,000 tumetoa lakini
hatujaletewa vitambulisho na hivi karibuni nimeenda Bima ya afya Mwanza
wakasema hawajapokea fedha za Madiwani kutoka Rorya DMO tuambie pesa zetu
umezipeleka wapi.”alisema Ayoyi.
Hata hivyo Mganga Mkuu Daniel
Chacha alikwepa kujibu baadhi ya maswali huku maswali mengine aliyojibu kudaiwa
kutowaridhisha Madiwani ambapo kwa upande wa vitambulisho vya Bima ya afya alisema kuwa vitambulisho vimekataliwa kwa
madai kuwa hakuna mchango wowote uliowasilishwa
kwa ajili ya kupatiwa huduma hiyo ya vitambulisho.
Madiwani hao hawakuishia kwa
Mganga Mkuu pia walimvaa Mweka Hazina wa Halmashauri,Caiser Ninalwo na kumtuhumu kushindwa kusimamia fedha
zikiwamo asilimia 20 inayotolewa na Halmashauri kwenda katika vijiji ambapo
walimlalamika kuwa kumekuwa na upungufu wa fedha zinazotolewa kwenda kwenye
vijiji huku vijiji vingine vikidaiwa kutofikiwa na fedha .
“Miongoni mwa Madiwani
waliolalamika kutolewa kwa fedha kidogo
kwenye vijiji ni Diwani wa kata ya Ikoma Laurent Adriano (CCM) Diwani wa kata
ya Koryo Peter Sarungi (CCM) Diwani kata ya Kitembe Thomas Patrick( Chadema) Diwani
wa kata ya Kigunga Magesa Magige (CCM).
“Kuna fedha inayotolewa na
Halmashauri asilimia 20 kwenda kwenye vijiji lakini kila kwaka fedha zinapungua
vijiji 80 vinatakiwa kupa asilimia hiyo mwaka juzi zilitolewa Sh. 613000,mwaka jana zikatolewa tena Sh.430,000, ambapo mwaka huu zimetolewa Sh. 100,000, kiasi hicho ni kidogo hasa ukizingatia serikali imetupatia ruzuku ya
zaidi ya Milioni 300 na kuna vijiji vina
akaunti havikuingiziwa fedha na kuna
vijiji havina akaunti fedha zinakwenda wapi?alihoji Sarungi.
Madiwani hao waliomba
kupatiwa Nyaraka za fedha zinazotolewa ili kujua na kuthibitisha kiasi cha fedha zinazokwenda kwenye vijiji
kila mwaka mbapo hata hivyo Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Rorya
Andreas Madundo alikubali ombi lao na kukubali kutoa nyaraka za fedha
zinazotolewa kwa manufaa ya vijiji.
Wakati huo huo madiwani hao
wa halmashauri wamemlalamika Mhandishi wa Maji Emmanuel Masanja kwa kutokamika
kwa visam vya majia ambpo walisema kuwa kuna fedha zilizotumika katika uchimbaji
wa visima lakini hadi sasa visima hivyo havitoi maji.
Naye Diwani wa kata ya
kisumwa, Amwolo Malaki (NCCR) alisema kuwa jumla ya Sh. Milioni 80
zilitolewa kufufua mradi wa maji katika kijiji cha Malasibora na Nyanchabakenye
na kwamba fedha za ujenzi huo zimepotea bila kuwa na manufaa.
“Visima havitoi maji na
mashine ni mbovu haifanyi kazi na mkandarasi alipewa Milioni 40 lakini hakuna
kisima ambapo kimeishakamilika na ikatangazwa zabuni kwa mkandarasi mwingine na
yeye akapewa Milioni 40 akanunua mashine
ambayo nayo haikufanya kazi, fedha zimekwisha na hatujui fedha zingine tutapata
wapi, wananchi wanaendelea kupata kero ya maji” Alisema Malaki.
Aliongeza “Zaidi ya mika mitatu
an nusu maji hayapatikani kamati zmeudwa kufatia lakini hatua zozote
zilizochukuliwa madiwani wenzangu kwa machafu haya na kwa kuzingatia kanuni
naomba mniunge mkono baraza lijeuke kuwa kamati tuwajadili hawa watu DMO, DT,
na Mhandishi wa Maji tumechoka na utendaji wao mbovu kwani kila baraza
tunazungumzia mambo yale yale yasiyotekelezwa?Alisema.
Hata hivyo kutokana na majibu
yaliyotolewa na wakuu hao wa Idara hizo tatu hayakuweza kuwaridhisha madiwani
hali iliyolazimu baraza hilo
kugeuka na kukwa kamati ili kuwajadili kwa kina.
Monday, May 21, 2012
SIASA CHAFU ZAANZA WILAYA YA RORYA
Watangaza nia ya Uenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya wameaanza
kutumia mbinu za kuhujumiana wao kwa wao huku wakitumia baadhi ya vyombo vya
habari kuchafuana.
Akizungumza na Mwandishi wa habari hii ofisini kwake, Katibu
Mwenezi wa CCM Wilaya ya Rorya Samueli kiboye alisema kuwa mmoja ya mgombea
ambaye hakutaka kutaja kutaja jina lake
alisema ameanza kutumia
vibaya vyombo vy ahabari kwa kukiuka taalumu hiyo.
Alisema kuwa kuna moja ya gazeti la kila siku si Uhuru,limetoa habari kuwa amemkatisha masomo
mwanafunzi na kumfanyisha kazi za nyumbani, huku binti huyo akinusha habari
hizo kuwa yeye aliamua kuondoka nyumbani kwao kutokana vipigo vya mara kwa mara
kutoka kwa Baba Mzazi kumkatisha masomo na
kumlazimsha kuolewa na ndipo
binti huyo alipoamua kutafuta kazi za nyumbani.
“Baada ya Mama yangu mzazi, Wankuru Joseph kufarikia Mwaka
2008,nilibahatika kuchaguliwa na kujiunga na Shule ya Sekondari Nyandoto-Tarime
kidato cha kwanza mwaka 2009, hadi cha Tatu sikuwahi kulipiwa ada na mzazi, walimu
wakamwandikia barua ya kumtaka alipe ada na wito wa kumwita shuleni lakini
hakufanya hivyo, nikafukuzwa shuleni na akaniambia kuolewa nilipokataa
alinipiga sana na Kunifukuza alisema Angelina.
Aliongeza kuwa baada ya kufukuzwa na baba yake alitafuta
sehemu ya kuishi na kumpata msamalia mwenye ambaye ni Mke wa Katibu Mwenezi wa
CCM Wilaya na kumwambia matatizo yake na kuamua kuishi hapa hadi sasa.
Alisema kuwa hiyo ni hujuma kutoka na watangaza nia wenzake kudurufu
( Photocopy) kwa habari iliyotolewa na kuisambaza katika vijiji ili wananchi waisome
kwa nia kum dhoofisha kisiasa.
Aidha amewataka waandishi wa habari kutumia taaluma yao ya kuandika habari
sahihi na kwamba wasitumike kwa lengo la masilahi ya mtu binafsi.
Fomu za kugombea
nafasi mbalimbali za uongozi kwa ngazi ya Wilaya na Mkoa zitaanza kuchukuliwa Juni
2 Mwaka huu, ambapo mpaka sasa miongoni mwa wagombea wa kiti cha Uenyekiti
Wilaya ya Rorya ni Samuel kiboye (Namba
tatu), Razaro Akuku, Jamoko Kateti na Yoda Ambonya.
Wednesday, May 16, 2012
WAKUU WA WILAYA WAAPISHWA,SMG 3 NA RISASI 430 ZAKAMATA
WAKUU wapya wa Wilaya Mkoa wa Mara jana waliapishwa rasmi na
Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa tayari kwa kuanza kazi, iliyofanyika katika
Ukumbi wa Uwekezaji wa Mkoa wa Mara, uliopo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
Baada ya kuapishwa
kwa Wakuu hao wapya wa Wilaya kwa pamoja walikwenda katika ofisi za CCM Mkoa
kuweka saini katika kitabu cha wageni jambo ambalo ni mara ya kwanza kufanya hivyo,tofauti
na awali kwa kwenda kila mmoja kwa muda wake na siku tofauti.
Shamra Shamra za
kuwaapisha Wakuu hao wapya zilitia fola, kwa wananchi na viongozi mbalimbali waliofurika
katika ukumbi huo, jambo ambalo pia liliwashangaza baadhi ya viongozi na kwamba
halijawahi kutokea.
Sherehe hizo zilianza kwa dua kutoka katika viongozi wa
madhehebu ya dini ya kiislamu na kikrsito ambapo Shehe Mkuu wa Waisalamu Mkoa
Shehe Magehe aliomba dua, akifuatiwa na Askofu Mkuu wa Wakatoliki, Mhashamu Msonganzila.
Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka Wakuu hao wa Wilaya
kuwajibika kwa kufanya kazi kwa
uadilifu, uchapa kazi, kuwa na moyo wa kujituma, maono na kuacha alama kama
kumbukumbu zao waachapo madaraka na kuwahudumia wananchi ipasavyo kwani Rais Jakaya Kikwete amewaamini
wao.
Alisema kuwa kuna changamoto zinaukabilia Mkoa wa Mara hasa
kwa ulinzi na usalama japokuwa bado kuna matukio yanayofanyika lakini yanadhibitiwa
haraka.
Alisema kuwa kuna baadhi ya watu kutoka mikoa na Wilaya
zinazopakana na nchi jirani wanaingia katika Mkoa wakiwa na silaha na risasi
ambapo jumla ya risasi zipatazo 430 na SMG tatu zilikamatwa katika Wilaya za
Tarime na Serengeti na kubaini watuhumiwa hao ni wakazi wa Kigoma.
Alizitaja changamoto zingine zinazoukabili Mkoa wa Mara,
pamoja na kuwa na rasilimali za kutosha wananchi wake bado ni masikini ambapo
Mkoa huku chini ya kiwango cha kitaifa, kuvushwa kwa magendo katika Wilaya ya Tarime kwenda
nchi jirani ya Kenya na ajira kwa vijana.
“ Kuhusu ajira wapo vijana ambao hawataki kujishughulisha na huwa vijiwe asubuhi , hii ni changamoto kubwa, huku
kukiwa na fursa nyingi za Mkoa kwa wao kujishughulisha, kuwepo wazi kwa maeneo
ya kilimo, huku ardhi ikiwa na rutuba ya kutosha” Alisema Tuppa.
Aliwataka Wakuu hao wapya kushughulikia changamoto hizo kwa
pamoja kwa kushirikiana na wadua mbalimbali wa maendeleo wa Mkoa wa Mara.
Walioapishwa majina yao na sehemu zao za kazi zikiwa kwenye
mabano ni ni Joshua Chacha Mirumbe(Bunda), Angelina Mabula (Butiama), Jackson Msome(
Musoma), Alias Goroe( Rorya), Capt. Mstaafu James Yamungu (Serengeti) na John
Henjewele( Tarime).
Viongozi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa walihudhuria sherehe
hizo wakiwemo pia viongozi wa vyama vingine vya siasa.
VIONGOZI WA VITONGOJI, TARAFA NA KATA WAPATA MSASA
VIONGOZI wa Tarafa,Kata vijijiji na Vitongoji wa Wilaya ya
Rorya wamepata Mafunzo juu ya Utawala Bora na uwajibika , ulinzi shirikishi na
rushwa katika eneo lao la kazi.
Akitoa mafunzo hayo ya siku mbili yaliyofanyika katika
kijiji cha Sudi Tarafa ya Mirare Wilayani humo, Afisa Utumishi wa Wilaya hiyo,
Sebastian Masanja aliwataka viongozi hao
kuwatumikia wananchi wao na kuhakikisha wanatoa taarifa za mapato na matumizi
kwa wananchi kwenye mikutano mikuu ya vijiji WDC na taarifa zote na michango ya
wananchi,tozo, wahisani,Halmashauri na Serikali kuu.
Alisema kuwa upo udhaifu wa kutofanya vikao ambao unasababisha
kuwepo kwa ugomvi hasa wa ardhi na kutokusanya ushuru kwa maduka na migahawa
iliyopo katika vijiji hivyo.
Aliwataka viongozi hao kuweka utaratibu wa kuwajibishana
kati ya viongozi wa kuchaguliwa na wananchi pamoja na watumishi wa Umma.
Aidha aliwataka viongozi hao kuwa mfano wa kuigwa kwa kuwa
na mashamba ya mfano, miradi midogo midogo ya kuwawezesha kujikimu katika
familia zao kama ufugaji wa kuku, bata na mbuzi ili wananchi waige mfano wao,
kwani kwa kufnaya hivyo itawasababisha kuondokana na umasikini.
Pia amewahimiza kuachana na mila potofu ya kuridhi wajane
kwani kwa kufanya hivyo ni kuongeza ongezeko la waathirika wengi wa Ugonjwa wa
Ukimwi ukizingatia kuwa Wilaya ya Rorya ndiyo yenye maambukizi makubwa
kiwilaya.
Aidha aliwataka kusaidia kampeni mbalimbali za kitaifa mfao,
kupima VVU, chanjo za watoto, panga uzazi, kuwa na choo bora, kuchemsha maji ya
kunywa, kunawa mikono kwa sabuni, kuwa waaminifu katika mapenzi na kuacha
vitenndo vya uzinzi, kujitolea kwenye shughuli za maendeleo, kuvaa mavazi yenye
heshima, kuazisha vikundi yva ulinzi shirikishi jamii na kupiga vita rushwa.
Akitoa mada juu ya ulinzi shirikishi,Mkaguzi Msaidizi wa
jeshi la polisi, Antony kahema aliwataka viongozi hao kuacha tabia ya
kujichukuliwa mamlaka na kuwanyanyasa wananchi kwa mamlaka waliyopewa na badala
yake wawafikishe katika mikono ya sheria.
“Nashangaa wapo baadhi ya watendaji wa kata na vitongoji na
vijiji wamekuwa wakiwanyanyasa wanachi aidha kwa kuwapiga na kuwafungia masaa
24 katika ofisi zao wale wanaosaidikiwa kuwa na tuhuma, hili ni kosa kwani kazi
yenu ni kuwasiliana na jeshi letu ili hatua za kisheria zichukuliwe na si
kuwapiga hadi kusababisha maumivu makali.”Alisema Mahema.
Aliwataka kuwa na utii wa sheria pasipo kuwa na shuruti na
si kiongozi kuhamasisha vurugu na kuongoza wananchi kupiga mtu hadi kufa, kwani
kwa kufanya hivyo kunasabisha kutoweka
kwa usalama.
Aliwataka pia kuondokana na dhana ya kumwona polisi na
kumwogopa bali ashirikiane nae kutatua nini matatizo ya uhalifu katika Tarafa
zao pamoja na kushirikisha jamii ili kupata ukweli wa jambo Fulani.
Aidha Kamanda wa Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU),
Wilaya ya Rorya, kebero Kassimu aliwataka viongozi hao kusaidia katika mapambano dhidi ya Rushwa
na si wao kuwa kichocheo cha kupokea Rushwa.
Katika kikao hicho yaliwekwa maazimio yao ikiwa pamoja na
kuweka sheria ndogo ndogo, kutoa taarifa ya mapato na matumizi, Baraza la ardhi
la kata litoe taarifa ya maendeleo kila
baada ya miezi mitatu kwenye Baraza la
maendeleo la kata, kutenga eneo la misitu, kuibua vyanzo vya mapato, kutenga
hekali za mazao ya chakula kwa kila kaya na kuhamasisha wakazi ujenzi wa vyoo
bora.
Friday, May 11, 2012
VIONGOZI wa
Halmashauri za Mkoa wa Mara wamepeana mbinu na changamoto za kukabiliana na wimbi la kutowasili
katika vituo vyao vya kazi ,watumishi wa halmashauri na jinsi ya kuwasidia katika vitu vyao vya kazi wanapotakiwa kazini.
Katika kongamono hilo la siku lililofanyika Mkoani hapa
viongozi hao wameazimia kuweka jitihada za kuweka vivutio kwa ajili ya kuwapata
na kuwabakiza(retention) watumishi wapya
na waliopo na kuboresha utendaji kazi
mahala pa kazi .
Akisoma hotuba kabla ya ufunguzi wa kongamano hilo,Afisa rasilimali watu wa Taasisi
ya Benjamini William Mkapa HIV/AIDS,issuja kilian alisema kuwa Taasisi imeona
ni vyema Halmashauri zikajadili mafanikio na changamoto ili kuweka mikakati ya
uboreshaji na kubadilishana mbinu mbalimbali.
Alisema kuwa Taasisi imepanga kujenga nyumba 10 za watumishi
na kuajiri watumishi wa afya katika Wilaya za serengeti, Tarime na Bunda katika
mwaka 2013/2014.
Akifungua kongamano hilo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa,
Buhanda Kichinda alisema kuwa Rasilimali watu ni nguzo muhimu katika
utekelezaji wa mipango ya kazi ambayo inalengakuboresha huduma mbalimbalui za
jamii ikiwemo huduma muhimu ya afya kwa watanzania wote.
Aliongeza kuwa kuna upungufu mkubwa wa rasilimali watu na
kwamba kunahitaji jitihada za mikakati ya madhubuti kwa ngazi zote ili
kuhakikisha wanapatikana watumishi wanaokidhi mahitaji na wenye ari ya utendaji
kazi.
Alisema kuwa kongamano hilo limeandaliwa katika wakati
muafaka kwani halmashauri zinajitayarisha kutekeleza mpango kabambe itakayopitishwa
ya mwaka 2012/2013 pia kupokea watumishi wapya kazini.
Aidha Halmashauri ziliwasilisha taarifa pamoja na mikakati
inayohusu menejimenti ya rasilimali watu katika Halmashuri kwa kushirikiana na
ofisi ya Raisi Menejimenti ya utumishi wa Umma na Wizara ya Afya na Ustawi wa
Jamii kuhakikisha inapata idadi inayokidhi ya rasilimali watu katika sekta ya
Afya.
Taasisi ya Benjamini William Mkapa HIV/AIDS kwa kushirikina
na Shirika la kimataifa la intra Healh Intenational, inatekeleza shughuli
mbalimbali katika halmashuri za Wilaya, zikiwemo kutoa mafunzo ya menejiment ya
Rasilimali watu,maadili katika sekta ya afya kwa timu za uendeshaji za shughuli
za sekta ya afya, uhasiashaji wa ajira katika sekta ya afya na ajira za
mikataba kwa watumishi na waalimu wa afya.
Wilaya ya Serengeti imejiwekea mkakati wa kujenga nyumba
tatu za watumishi na kutoa motisha kwa wafanyakazi bora waliokaa kazini kwa
mika 25 mfululizo na utumishi uliotukuka huku Wilaya zingine kama Rorya
ikilalmikia madiwani kutotumia utaratibu wa kupima mtumishi( Opras) na
watumishi kubadilishiwa vituo kabla ya kuwasili katika kituo chake kipya, huku
Wilaya ya Tarime ikilamikia ucheleweshwaji wa majibu ya watumishi walioomba
kazi baada ya kustaafu kutoka Wizarani wa Afya.
Subscribe to:
Posts (Atom)