Wednesday, May 23, 2012

MADIWANI WAWASHIKIA WATENDAJI


 RORYA.


MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Mkoani Mara wamemtuhumu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Rorya, Daniel Chacha kutumia fedha vibaya zinazotolewa na Halmashauri kwenda katika vituo vinavyotoa huduma ya afya kwa ajili ya kununua vifaa,dawa na mahitaji mengine huku akidaiwa kutofikisha baadhi ya vifaa kwenye vituo.

Hayo yalibainishwa katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika jana ambapo Madiwani walisema kuwa kuna baadhi ya wakuu wa idara wamekuwa wakitumia vibaya fedha za Serikali ambapo walisema kuwa kuna fedha ambazo zilitolewa kwa ajili ya miradi ya maendeleo lakini hazitumiki ipasavyo.

Diwani wa kata ya Kyango’mbe Emanuel Manyama,(Matongwe) CCM alisema kuwa kuna kiasi cha fedha Milioni 20 zilitengwa kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Bitiryo lakini fedha zilizoingizwa kwenye akaunti si kiwango  kamili kilichotolewa na Halmashauri.

“Kuna ndume tatu ambazo ni tatizo kwenye Halmashauri DMO,DT na Mhandisi wa maji hawa watu ni wala fedha kijiji cha Bitiryo zilitengwa  Milioni 20  kwa ajili ya ujenzi cha kushangaza fedha zilizoingizwa kwenye akaunti ya kijiji ni Milioni 17 tu Milioni 3 hazionekani  zimebaki Halmashauri lakini hapa kwenye kablasha naambiwa milioni 20 ziliingizwa kwenye akaunti ya kijiji na zimetumika kujenga zahanati na wakati ni Milioni 17 zilizowekwa kwenye akaunti naomba nielezwe hizo pesa zingine zimekwenda wapi na kwanini hazikuwekwa kwenye akaunti”alisema Manyama.

Diwani wa viti maalumu Tarafa ya Nyancha Pendo Odero CCM  aliongeza kwa kusema kuwa Mganga mkuu Chacha anatuhumiwa kwa kutofikisha fedha za vifaa na dawa kwenye baadhi ya vituo vya afya nakwamba baada ya kufahamu tuhuma hizo alianza kuwahamasisha wanafunzi kumfichia siri ya kutofika kwa fedha za vifaa.

“DMO kala pesa za Halmashauri za kununua vifaa na hata dawa zilizotolewa kusambazwa vituoni hazijafika baada ya yeye kugundua mambo yameharibika alichukuwa gari kwenda kuwahamasisha watumishi na kuwadanganya waseme pesa na vifaa vimefika lakini mipango yake ikavunjika akiwa safarini taarifa zikafika kwa mkurugenzi na Mwenyekiti wa Halimashauri wakazyuia gari na kumtaka astishe zoezi hilo”alisema Odero.

Diwani wa kata ya Mirare Peter Ayoyi( CCM),alilalamikia Madiwani kutopatiwa vitambulisho vya Bima ya afya  licha ya kuwa tayali walishatoa fedha za malipo ya vitambulisho.

“DMO atueleze hatima ya vitambulisho vyetu vya bima ya afya Madiwani tumeshalipa pesa 3,000 kwa kila Diwani ambapo 3,000 zingine kwa kila Diwani,  Halmashauri inachangia jumla kila Diwani ni 6,000 tumetoa lakini hatujaletewa vitambulisho na hivi karibuni nimeenda Bima ya afya Mwanza wakasema hawajapokea fedha za Madiwani kutoka Rorya DMO tuambie pesa zetu umezipeleka wapi.”alisema Ayoyi.

Hata hivyo Mganga Mkuu Daniel Chacha alikwepa kujibu baadhi ya maswali huku maswali mengine aliyojibu kudaiwa kutowaridhisha Madiwani ambapo kwa upande wa vitambulisho vya Bima ya afya  alisema kuwa vitambulisho vimekataliwa kwa madai kuwa hakuna mchango wowote uliowasilishwa  kwa ajili ya kupatiwa huduma hiyo ya vitambulisho.

Madiwani hao hawakuishia kwa Mganga Mkuu pia walimvaa Mweka Hazina wa Halmashauri,Caiser Ninalwo  na kumtuhumu kushindwa kusimamia fedha zikiwamo asilimia 20 inayotolewa na Halmashauri kwenda katika vijiji ambapo walimlalamika kuwa kumekuwa na upungufu wa fedha zinazotolewa kwenda kwenye vijiji huku vijiji vingine vikidaiwa kutofikiwa na fedha .

“Miongoni mwa Madiwani waliolalamika  kutolewa kwa fedha kidogo kwenye vijiji ni Diwani wa kata ya Ikoma Laurent Adriano (CCM) Diwani wa kata ya Koryo Peter Sarungi (CCM) Diwani kata ya Kitembe Thomas Patrick( Chadema) Diwani wa kata ya Kigunga Magesa Magige (CCM).

“Kuna fedha inayotolewa na Halmashauri asilimia 20 kwenda kwenye vijiji lakini kila kwaka fedha zinapungua vijiji 80 vinatakiwa kupa asilimia hiyo mwaka juzi zilitolewa Sh. 613000,mwaka jana zikatolewa tena Sh.430,000, ambapo mwaka huu zimetolewa Sh. 100,000, kiasi hicho ni kidogo hasa ukizingatia serikali imetupatia ruzuku ya zaidi ya Milioni 300 na  kuna vijiji vina akaunti havikuingiziwa fedha  na kuna vijiji havina akaunti fedha zinakwenda wapi?alihoji Sarungi.

Madiwani hao waliomba kupatiwa Nyaraka za fedha zinazotolewa ili kujua na kuthibitisha  kiasi cha fedha zinazokwenda kwenye vijiji kila mwaka mbapo hata hivyo Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Rorya Andreas Madundo alikubali ombi lao na kukubali kutoa nyaraka za fedha zinazotolewa kwa manufaa ya vijiji.

Wakati huo huo madiwani hao wa halmashauri wamemlalamika Mhandishi wa Maji Emmanuel Masanja kwa kutokamika kwa visam vya majia ambpo walisema kuwa kuna fedha zilizotumika katika uchimbaji wa visima lakini hadi sasa visima hivyo havitoi maji.

Naye Diwani wa kata ya kisumwa, Amwolo  Malaki  (NCCR) alisema kuwa jumla ya Sh. Milioni 80 zilitolewa kufufua mradi wa maji katika kijiji cha Malasibora na Nyanchabakenye na kwamba fedha za ujenzi huo zimepotea bila kuwa na manufaa.

“Visima havitoi maji na mashine ni mbovu haifanyi kazi na mkandarasi alipewa Milioni 40 lakini hakuna kisima ambapo kimeishakamilika na ikatangazwa zabuni kwa mkandarasi mwingine na yeye akapewa Milioni 40  akanunua mashine ambayo nayo haikufanya kazi, fedha zimekwisha na hatujui fedha zingine tutapata wapi, wananchi wanaendelea kupata kero ya maji” Alisema Malaki.

Aliongeza “Zaidi ya mika mitatu an nusu maji hayapatikani kamati zmeudwa kufatia lakini hatua zozote zilizochukuliwa madiwani wenzangu kwa machafu haya na kwa kuzingatia kanuni naomba mniunge mkono baraza lijeuke kuwa kamati tuwajadili hawa watu DMO, DT, na Mhandishi wa Maji tumechoka na utendaji wao mbovu kwani kila baraza tunazungumzia mambo yale yale yasiyotekelezwa?Alisema.

Hata hivyo kutokana na majibu yaliyotolewa na wakuu hao wa Idara hizo tatu hayakuweza kuwaridhisha madiwani hali iliyolazimu baraza hilo kugeuka na kukwa kamati ili kuwajadili kwa kina.

No comments:

Post a Comment