Monday, May 21, 2012

SIASA CHAFU ZAANZA WILAYA YA RORYA


Watangaza nia ya Uenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya wameaanza kutumia mbinu za kuhujumiana wao kwa wao huku wakitumia baadhi ya vyombo vya habari kuchafuana.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hii ofisini kwake, Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Rorya Samueli kiboye alisema kuwa mmoja ya mgombea ambaye hakutaka kutaja kutaja jina lake alisema ameanza kutumia vibaya vyombo vy ahabari kwa kukiuka taalumu hiyo.

Alisema kuwa kuna moja ya gazeti la kila siku si  Uhuru,limetoa habari kuwa amemkatisha masomo mwanafunzi na kumfanyisha kazi za nyumbani, huku binti huyo akinusha habari hizo kuwa yeye aliamua kuondoka nyumbani kwao kutokana vipigo vya mara kwa mara kutoka kwa Baba Mzazi kumkatisha masomo na  kumlazimsha  kuolewa na ndipo binti huyo alipoamua kutafuta kazi za nyumbani.

“Baada ya Mama yangu mzazi, Wankuru Joseph kufarikia Mwaka 2008,nilibahatika kuchaguliwa na kujiunga na Shule ya Sekondari Nyandoto-Tarime kidato cha kwanza mwaka 2009, hadi cha Tatu sikuwahi kulipiwa ada na mzazi, walimu wakamwandikia barua ya kumtaka alipe ada na wito wa kumwita shuleni lakini hakufanya hivyo, nikafukuzwa shuleni na akaniambia kuolewa nilipokataa alinipiga sana na Kunifukuza alisema Angelina.

Aliongeza kuwa baada ya kufukuzwa na baba yake alitafuta sehemu ya kuishi na kumpata msamalia mwenye ambaye ni Mke wa Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya na kumwambia matatizo yake na kuamua kuishi hapa hadi sasa.

Alisema kuwa hiyo ni hujuma kutoka na watangaza nia wenzake kudurufu ( Photocopy) kwa habari iliyotolewa na kuisambaza katika vijiji ili wananchi waisome kwa nia kum dhoofisha kisiasa.

Aidha amewataka waandishi wa habari kutumia taaluma yao ya kuandika habari sahihi na kwamba wasitumike kwa lengo la masilahi ya mtu binafsi.

Fomu za  kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwa ngazi ya Wilaya na Mkoa zitaanza kuchukuliwa Juni 2 Mwaka huu, ambapo mpaka sasa miongoni mwa wagombea wa kiti cha Uenyekiti Wilaya ya Rorya ni Samuel  kiboye (Namba tatu), Razaro Akuku, Jamoko Kateti na Yoda Ambonya.

No comments:

Post a Comment