Friday, May 11, 2012


VIONGOZI  wa Halmashauri za Mkoa wa Mara wamepeana mbinu  na changamoto za kukabiliana na wimbi la kutowasili  katika vituo vyao vya kazi ,watumishi wa  halmashauri na  jinsi ya kuwasidia  katika vitu vyao vya kazi wanapotakiwa kazini.


Katika kongamono hilo la siku lililofanyika Mkoani hapa viongozi hao wameazimia kuweka jitihada za kuweka vivutio kwa ajili ya kuwapata na kuwabakiza(retention) watumishi  wapya na waliopo na kuboresha  utendaji kazi mahala pa kazi .


Akisoma hotuba kabla ya ufunguzi  wa kongamano hilo,Afisa rasilimali watu wa Taasisi ya Benjamini William Mkapa HIV/AIDS,issuja kilian alisema kuwa Taasisi imeona ni vyema Halmashauri zikajadili mafanikio na changamoto ili kuweka mikakati ya uboreshaji na kubadilishana mbinu mbalimbali.


Alisema kuwa Taasisi imepanga kujenga nyumba 10 za watumishi na kuajiri watumishi wa afya katika Wilaya za serengeti, Tarime na Bunda katika mwaka 2013/2014.


Akifungua kongamano hilo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Buhanda Kichinda alisema kuwa Rasilimali watu ni nguzo muhimu katika utekelezaji wa mipango ya kazi ambayo inalengakuboresha huduma mbalimbalui za jamii ikiwemo huduma muhimu ya afya kwa watanzania wote.

Aliongeza kuwa kuna upungufu mkubwa wa rasilimali watu na kwamba kunahitaji jitihada za mikakati ya madhubuti kwa ngazi zote ili kuhakikisha wanapatikana watumishi wanaokidhi mahitaji na wenye ari ya utendaji kazi.


Alisema kuwa kongamano hilo limeandaliwa katika wakati muafaka kwani halmashauri zinajitayarisha kutekeleza mpango kabambe itakayopitishwa ya mwaka 2012/2013 pia kupokea watumishi wapya kazini.
Aidha Halmashauri ziliwasilisha taarifa pamoja na mikakati inayohusu menejimenti ya rasilimali watu katika Halmashuri kwa kushirikiana na ofisi ya Raisi Menejimenti ya utumishi wa Umma na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuhakikisha inapata idadi inayokidhi ya rasilimali watu katika sekta ya Afya.


Taasisi ya Benjamini William Mkapa HIV/AIDS kwa kushirikina na Shirika la kimataifa la intra Healh Intenational, inatekeleza shughuli mbalimbali katika halmashuri za Wilaya, zikiwemo kutoa mafunzo ya menejiment ya Rasilimali watu,maadili katika sekta ya afya kwa timu za uendeshaji za shughuli za sekta ya afya, uhasiashaji wa ajira katika sekta ya afya na ajira za mikataba kwa watumishi na waalimu wa afya.


Wilaya ya Serengeti imejiwekea mkakati wa kujenga nyumba tatu za watumishi na kutoa motisha kwa wafanyakazi bora waliokaa kazini kwa mika 25 mfululizo na utumishi uliotukuka huku Wilaya zingine kama Rorya ikilalmikia madiwani kutotumia utaratibu wa kupima mtumishi( Opras) na watumishi kubadilishiwa vituo kabla ya kuwasili katika kituo chake kipya, huku Wilaya ya Tarime ikilamikia ucheleweshwaji wa majibu ya watumishi walioomba kazi baada ya kustaafu kutoka Wizarani wa Afya.

No comments:

Post a Comment