Wednesday, May 16, 2012

VIONGOZI WA VITONGOJI, TARAFA NA KATA WAPATA MSASA



VIONGOZI wa Tarafa,Kata vijijiji na Vitongoji wa Wilaya ya Rorya wamepata Mafunzo juu ya Utawala Bora na uwajibika , ulinzi shirikishi na rushwa katika eneo lao la kazi.

Akitoa mafunzo hayo ya siku mbili yaliyofanyika katika kijiji cha Sudi Tarafa ya Mirare Wilayani humo, Afisa Utumishi wa Wilaya hiyo, Sebastian Masanja  aliwataka viongozi hao kuwatumikia wananchi wao na kuhakikisha wanatoa taarifa za mapato na matumizi kwa wananchi kwenye mikutano mikuu ya vijiji WDC na taarifa zote na michango ya wananchi,tozo, wahisani,Halmashauri na Serikali kuu.

Alisema kuwa upo udhaifu wa kutofanya vikao ambao unasababisha kuwepo kwa ugomvi hasa wa ardhi na kutokusanya ushuru kwa maduka na migahawa iliyopo katika vijiji hivyo.

Aliwataka viongozi hao kuweka utaratibu wa kuwajibishana kati ya viongozi wa kuchaguliwa na wananchi pamoja na watumishi wa Umma.

Aidha aliwataka viongozi hao kuwa mfano wa kuigwa kwa kuwa na mashamba ya mfano, miradi midogo midogo ya kuwawezesha kujikimu katika familia zao kama ufugaji wa kuku, bata na mbuzi ili wananchi waige mfano wao, kwani kwa kufnaya hivyo itawasababisha kuondokana na umasikini.
Pia amewahimiza kuachana na mila potofu ya kuridhi wajane kwani kwa kufanya hivyo ni kuongeza ongezeko la waathirika wengi wa Ugonjwa wa Ukimwi ukizingatia kuwa Wilaya ya Rorya ndiyo yenye maambukizi makubwa kiwilaya.

Aidha aliwataka kusaidia kampeni mbalimbali za kitaifa mfao, kupima VVU, chanjo za watoto, panga uzazi, kuwa na choo bora, kuchemsha maji ya kunywa, kunawa mikono kwa sabuni, kuwa waaminifu katika mapenzi na kuacha vitenndo vya uzinzi, kujitolea kwenye shughuli za maendeleo, kuvaa mavazi yenye heshima, kuazisha vikundi yva ulinzi shirikishi jamii na kupiga vita rushwa.

Akitoa mada juu ya ulinzi shirikishi,Mkaguzi Msaidizi wa jeshi la polisi, Antony kahema aliwataka viongozi hao kuacha tabia ya kujichukuliwa mamlaka na kuwanyanyasa wananchi kwa mamlaka waliyopewa na badala yake wawafikishe katika mikono ya sheria.

“Nashangaa wapo baadhi ya watendaji wa kata na vitongoji na vijiji wamekuwa wakiwanyanyasa wanachi aidha kwa kuwapiga na kuwafungia masaa 24 katika ofisi zao wale wanaosaidikiwa kuwa na tuhuma, hili ni kosa kwani kazi yenu ni kuwasiliana na jeshi letu ili hatua za kisheria zichukuliwe na si kuwapiga hadi kusababisha maumivu makali.”Alisema Mahema.

Aliwataka kuwa na utii wa sheria pasipo kuwa na shuruti na si kiongozi kuhamasisha vurugu na kuongoza wananchi kupiga mtu hadi kufa, kwani kwa kufanya hivyo kunasabisha  kutoweka kwa usalama.
Aliwataka pia kuondokana na dhana ya kumwona polisi na kumwogopa bali ashirikiane nae kutatua nini matatizo ya uhalifu katika Tarafa zao pamoja na kushirikisha jamii ili kupata ukweli wa jambo Fulani.

Aidha Kamanda wa Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Wilaya ya Rorya, kebero Kassimu aliwataka viongozi  hao kusaidia katika mapambano dhidi ya Rushwa na si wao kuwa kichocheo cha kupokea Rushwa.


Katika kikao hicho yaliwekwa maazimio yao ikiwa pamoja na kuweka sheria ndogo ndogo, kutoa taarifa ya mapato na matumizi, Baraza la ardhi la kata litoe taarifa ya maendeleo  kila baada ya miezi mitatu  kwenye Baraza la maendeleo la kata, kutenga eneo la misitu, kuibua vyanzo vya mapato, kutenga hekali za mazao ya chakula kwa kila kaya na kuhamasisha wakazi ujenzi wa vyoo bora.


No comments:

Post a Comment