Wednesday, May 16, 2012

WAKUU WA WILAYA WAAPISHWA,SMG 3 NA RISASI 430 ZAKAMATA




WAKUU wapya wa Wilaya Mkoa wa Mara jana waliapishwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa tayari kwa kuanza kazi, iliyofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji wa Mkoa wa Mara, uliopo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa.


 Baada ya kuapishwa kwa Wakuu hao wapya wa Wilaya kwa pamoja walikwenda katika ofisi za CCM Mkoa kuweka saini katika kitabu cha wageni jambo ambalo ni mara ya kwanza kufanya hivyo,tofauti na awali kwa kwenda kila mmoja kwa muda wake na siku tofauti.

Shamra  Shamra za kuwaapisha Wakuu hao wapya zilitia fola, kwa wananchi na viongozi mbalimbali waliofurika katika ukumbi huo, jambo ambalo pia liliwashangaza baadhi ya viongozi na kwamba halijawahi kutokea.

Sherehe hizo zilianza kwa dua kutoka katika viongozi wa madhehebu ya dini ya kiislamu na kikrsito ambapo Shehe Mkuu wa Waisalamu Mkoa Shehe Magehe aliomba dua, akifuatiwa na Askofu Mkuu wa  Wakatoliki, Mhashamu Msonganzila.

Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka Wakuu hao wa Wilaya kuwajibika  kwa kufanya kazi kwa uadilifu, uchapa kazi, kuwa na moyo wa kujituma, maono na kuacha alama kama kumbukumbu zao waachapo madaraka na kuwahudumia wananchi  ipasavyo kwani Rais Jakaya Kikwete amewaamini wao.

Alisema kuwa kuna changamoto zinaukabilia Mkoa wa Mara hasa kwa ulinzi na usalama japokuwa bado kuna matukio yanayofanyika lakini yanadhibitiwa haraka.

Alisema kuwa kuna baadhi ya watu kutoka mikoa na Wilaya zinazopakana na nchi jirani wanaingia katika Mkoa wakiwa na silaha na risasi ambapo jumla ya risasi zipatazo 430 na SMG tatu zilikamatwa katika Wilaya za Tarime na Serengeti na kubaini watuhumiwa hao ni wakazi wa Kigoma.

Alizitaja changamoto zingine zinazoukabili Mkoa wa Mara, pamoja na kuwa na rasilimali za kutosha wananchi wake bado ni masikini ambapo Mkoa huku chini ya kiwango cha kitaifa,   kuvushwa  kwa magendo katika Wilaya ya Tarime kwenda nchi jirani ya Kenya na ajira kwa vijana.


“ Kuhusu ajira wapo vijana  ambao hawataki kujishughulisha na huwa vijiwe  asubuhi , hii ni changamoto kubwa, huku kukiwa na fursa nyingi za Mkoa kwa wao kujishughulisha, kuwepo wazi kwa maeneo ya kilimo, huku ardhi ikiwa na rutuba ya kutosha” Alisema Tuppa.


Aliwataka Wakuu hao wapya kushughulikia changamoto hizo kwa pamoja kwa kushirikiana na wadua mbalimbali wa maendeleo wa Mkoa wa Mara.

Walioapishwa majina yao na sehemu zao za kazi zikiwa kwenye mabano ni ni Joshua Chacha Mirumbe(Bunda), Angelina Mabula (Butiama), Jackson Msome( Musoma), Alias Goroe( Rorya), Capt. Mstaafu James Yamungu (Serengeti) na John Henjewele( Tarime).



Viongozi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa walihudhuria sherehe hizo wakiwemo pia viongozi wa vyama vingine vya siasa.

No comments:

Post a Comment