Tuesday, May 29, 2012

WANANCHI WATAKIWA KUJUA SHERIA YA PAROLE


MUSOMA

WANANCHI wa Mkoa wa Mara, wametakiwa kufahamu utaratibu wa kisheria wa wafugwa wenye kifungo kirefu wanaoonyesha mwenendo mzuri wa kurekebika wawapo Magereza (PAROLE), na kumaliza kifungo chao wakiwa  nje  ya gereza na si kuwakataa.


Hayo yalisemwa Mei 29 Mwaka huu katika uzinduzi wa Bodi ya Parole, Afisa Mwandamizi Afisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Buhacha Kichinda alipokuwa anazindua bodi hiyo yenye jukumu la kupitia majalada ya wafugwa wenye nidhamu wawapo katika vifungo vyao magerezani.

Alisema hiyo ni changamoto kubwa inayowakabili wafugwa wanaoachiwa kwa sheria ya Parole kukataliwa na wananchi wanapotakiwa kumalizia kifungo chao wakiwa majumbani mwao, jambo ambalo lilikuwa kikwazo kwa utekelezaji wa sheria hiyo.


Aliongeza kuwa elimu inahitaji kwa wananchi juu ya umuhimu wa Parole kwa kushirikiana na viongozi wa Serikali ili wananchi waweze kushirikiana nao kwani wamekuwa tayari wamehakikiwa kuwa wana tabia hivyo na wengi  kujishughulisha katika majukumu mbalimbali ya ujenzi wa Taifa kwa kujishughulisha na kilimo, ufugaji, uvuvi na  biashara ndogo ndogo.


Ameitaka bodi hiyo kufanya kazi za uchunguzi wa majalada kwa kina ili wafugwa hao wanapokuwa na kifungo cha nje wasifanye uhalifu tena na kusababisha kutoaminiwa kwa bodi.


Awali akisoma taarifa ya Parole, Mkuu wa Magereza  Mkoa (RPO), Melchadus Mwendwa alisema kuwa ofisi yake imekuwa na changamoto mbalimbali za kufuatilia taarifa muhimu za kukamilisha majalada ya wafugwa wanaopekezwa kuachiliwa ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa nakala za hukumu toka Mahakamani,taarifa za uhalifu za awali toka jeshi la polisi,ufinyu wa bajeti na uelewa mdogo wa Sheria ya Parole kwa viongozi wa vijiji/mitaa anapochagua kuishi mfugwa.

Alisema kuwa kati ya wafugwa 268  wafugwa 10 tu waliovunja masharti wengi wao wakitenda makosa mengine ya jinai na kuwalazimu kurudishwa gerezani kwa mujibu wa sheria na  wafugwa wapatao 40 wakiendelea na vifungo vyao chini ya utaratibu wa Parole wakiwa katika mitaa na vijiji walipochagua kuishi  na wafugwa wapatao 219 tayari wamemaliza vifungo vyao chini ya utaratibu huo.

Sheria ya Bodi ya Parole N0. 25/1994 na marekebisho yake No. 5/2002, kanuni za bodi ya Parole No. GN 563/1997 vilianza kutumika mwaka 1999 na kwa mujibu wa kifungu cha 3(3) cha Sheria ya Bodi za Parole kinaidhinisha ziundwe Bodi za Parole Mikoa ambayo kwa Mkoa wa Mara zilizinduliwa Mei 29 ambayo kazi  zake ni kupitia kila jalada la mfugwa lenye vielelezo vinavyojitajika toka sehemu mbalimbali, aliyependekezwa kuachiliwa kwa Parole na kuthibitisha viwango vya sifa za mfugwa ili akubalike.


Aidha kati ya majalada ya wafugwa wapatao 321 yaliyopekezwa na Bodi ya Parole Mkoa wa Mara tangu utaratibu huo uanzishwe ni majalada 22 tu ambayo bado yapo kwenye Bodi ya Parole Taifa yanayofanyiwa mchakato wa kuyapeleka kwa Waziri huska ili ayatolee uamuzi  idadi ambayo hairidhishi.

No comments:

Post a Comment