Saturday, March 16, 2013

WANANCHI WANAOZUNGUKA MGODI WA NORTH MARA KUPEWA FIDIA


TARIME.

KUFUATIA kuundwa kwa kikosi kazi (Task Force) kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuchunguza uthamini fidia ya wakazi wanaozunguka mgodi wa Dhahabu wa North Mara,wananchi hao sasa watapatiwa ufumbuzi wa tatizo hilo.

Hayo yamesema na Afisa Mthamini Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mwenyekiti wa Kikosi kazi hicho, Adam Yusuf alipokuwa akijibu hoja ya Diwani wa kata ya Mbogi,Wilaya ya Tarime Mkoa wa Mara  Sylivester Nyankomo,katika kikao cha Baraza la Madiwani, kuhusu fidia utatuzi wa mgogoro wa Mgodi na wananchi wanaozungumka katika eneo hilo.


Katika hatua nyingine Diwani huyo pia alikishtumu Kikosi kazi hicho kwa kutoa taarifa isiyo na sahihi wala uthibitisho kutoka kwa mwekezaji,jambo ambalo lilizua mgogoro katika kikao hicho na madiwani kuitaka taarifa hiyo iandikwe na kuwekewe sahihi ndipo ijadiliwe.



Akisoma taarifa hiyo mbele ya baraza la madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Tarime,katika kikao cha dharula cha kupokea taarifa ya  vikao kati ya kikosi kazi cha kushughulikia masuala ya uthamini na fidia, Katibu wa kikosi kazi, Jeremiah  Minja alisema kuwa ni lengo la Serikali kuona kuwa matatizo yaliyojitokeza katika mgodi wa Noth Mara yanapatiwa ufumbuzi wa kudumu na kumwezesha mwekezaji kuendelea na shughuli zake kama kawaida huku haki stahili za wananachi wa ardhi wanaozunguka mgdo huo zikizingatiwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.

Aidha ni azam ya Serikali ni  kuona kuwa amani na Utulivu na mahusiano mema kati ya Mgodi na wananchi wanaozunguka Mgodi huo vinadumishwa na ndiyo maana ikaazimia kiudwe kikosi kazi kitakachojumisha wataalamu na maafisa kutoka katika taasisi mbalimbali za Serikali kusimamia utatuzi wa matatizo hayo.

Alisema kuwa matatizo yaliyojitokeza katika maeneo ya vijiji vinavyozunguka mgodi ni pamoja na wanachi ambao maeneo yao yalifanyiwa uthamini lakini bado hawako tayari kuchukua malipo yao,waliofanyiwa uthamini lakini hawako tayari kuondoka,waliopokea sehemu ya malipo nab ado wako katika maeneo yaliyofanyiwa uthamini,waliofanyiwa uthamini wakachukua malipo yao yote na kuwaendelea kukaa na kuendeleza maeneo ambayo yalifanyiwa uthamini ambapo kuna wengine hawako tayari kuona maeneo yao yakifanyiwa uthamini.


Wiki iliyopita katika kikao cha Baraza la Madiwani  wakati wa kutambulisha kikosi kazi hicho, Baraza liliagiza kikosi hicho kwenda katika vijiji vya Kewanja, Nyangoto na Nyakunguru na Baraza lipewe matokeo ya vikao hivyo kabla ya zoezi rasmi la uthamini na uhakika kuanza katika maeneo husika.
Alisema kuwa baada ya kikao cha halamshauri ya Kijiji cha Kewanja kulitolewa hoja na kujdiliwaambapo iliagizwa Uthamini ufanyike ndani ya wiki mbili,ambapo kikosi hicho kilifanya kazi hiyo kama kilivyoagizwa lakini dosari iijitokeza katika kijiji cha Nyangoto ambao hawakuwa tayari kuzungumza wala  kushirikia katika zoezi hilo hadi hapo Mgodi utakapotoa kesi yao Mahakamani na ndipo kipagwe kikao kingine na uongozi wa mgodi uwepo ili kuzungumza nao.


Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Amos Sagara aliiomba Wizara ya Nishati na Madini ,Baraza la Mazingira (NEMC), wao pia waunde kikosi kazi kingine kwa ajili ya kuchunguza matatizo yanayowakabili wakazi wanaozunguka mgodi huo kwani maisha yao yako hatarini kwa kuwa maji machafu  ya kusafishia dhahabu yanaathiri afya ya watanzania hao ambao hawana hatia.

Aidha alikiomba kikosi kazi hicho kuzunguka kwa vijiji vyote vinavyozunguka Mgodi huo ili kujua matatizo yao ingawaje nayo yanafafa na ya vijiji hivyo, vijiji ambavyo ‘Task Force’ imetakiwa kwenda na kurudisha  mrejesho ni pamoja na Kerende, Nyamwaga, Matongo,  na Genkuru.


Akizungumza katika Kikao  hicho, Meneja wa Mgodi huo,Champman Gerry alitoa shukrani kwa Serikali kuunda timu hiyo ili kuja kutatua matatizo  kwamba amesikia akilalamikiwa  kuwa walikuwa hawalipwi fidia kwa mujibu wa sheria,na kwamba atazingatia utaratibu atakaopewa na kwamba ataufuata   ili kuondoa kabisa matatizo yaliyopo baina yao na wananchi.



Tuesday, March 12, 2013

MKUU WA WILAYA YA BUTIAMA NA USALAMA

BUTIAMA MARA,



 Mkuu wa Wilaya ya Butiama,Angeline Mabula  amesema kuwa hali ya Ulinzi na Usalama katika Wilaya hiyo imeimarika tofauti na hapo awali ambapo ilikubwa na matukio ya mauaji ya kutisha.

Alikuwa akizungumza na Waandishi  kutoka vyombo mbalimbali vya  habari vya Radio, Magazeti na Luninga juu ya mafaniko ya awamu ya nne katika Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi kwa kipindi cha mwaka 2005-2012


Kwa siku za hivi karibuni, Wilaya ilikumbwa na wimbi la mauaji yanayohusishwa na imani za kishirikina, Serikali imechukua kila tahadhari kuhakikisha kwamba mauaji hayatokei tena,elimu imeendelea kutolewa, ili kuhimiza ulinzi shirikishi ambao utakuwa suluhisho la tatizo la mauaji”Alisema Mabula. 

Alisema kuwa historia inaonyesha kwamba, mbali na mauaji yatokanayo na ugomvi wa koo, wizi wa mifugo na ugomvi/migogoro ya ardhi mauaji ya sasa ya kuchinja watu hayakuwahi kutokea, yameibuka tu kwa udanganyifu  wa watu kutaka kujipatia utajiri wa haraka haraka.

Serikali inafanya kila linalowezekana kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wahalifu wa aina zote, kwa kuwafichua na kuwafikisha mbele ya vyombo vya dola ili kulinda raia wake na mali zao. 
Aidha Wilaya ina vituo 10 vya polisi Buhemba, Bisumwa, Bukima, Suguti, Kiagata, Kyabakari, Kigera etuma, Butiama, Saragana na Tegeruka.

Aliongeza kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua katika kuwahimiza na kuwaelewesha wananchi kuwa ulinzi wao na mali zao uko mikononi mwa wananchi wenyewe wakishirikiana na Polisi, dhana ya Polisi jamii na ulinzi shirikishi inaendelea kuhimizwa.


Wilaya imeweka mpango madhubuti wa  kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa vijana au wanamgambo waliokwishapitia mafunzo ili kuimarisha ulinzi na Usalama katika maeneo yao na kuwatahadharisha kutojichukulia sheria mikononi.


Amewataka vijana na akinamama kuunda vikundi ili wapewe vitendea kazi ambavyo vitawasaidia katika kazi zao za ujasiliamali na kwamba jumla ya Sh. Milioni 90 zimetegwa kwa aili ya kuwawezesha vijana na akina mama ,ambapo kati ya hizo Milioni 45 ni za Vijana na Milioni 45 ni za vikundi vya akina mama ambapo watapewa vitendea kazi watakapokuwa wamejisajili.


Aidha vikundi 4 vya wajasiliamali vilipewa mikopo yenye thamani ya Sh. 180,000,000 kutoka mfuko wa wajasiliamali unaofadhiliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Vikundi vilivyopewa fedha ni Mwangaza SACCOS Buhemba Tshs. 80,000,000, Imani Bwai (Kiriba) Shs. 31,000,000 na Mwamucha SACCOS (Mugango) Tshs. 30,000,000




Katika kipindi cha miezi sita halmashauri imeweza kusimamia vizuri fedha zilizopatikana katika vyanzo mbalimbali kwa ajili ya kugharamia matumizi ya mishahara, matumizi mengineyo na miradi ya maendeleo.  Pia Ruzuku ya Serikali imeongezeka kutoka Sh.571,556,000 mwaka 2005 hadi Sh.975,426,302  mwaka 2012 sawa na 59%.




Monday, March 4, 2013

MAGUFULI AWAPONGEZA CHADEMA KUTEKELEZA ILANI



MUSOMA.


WAZIRI wa Ujenzi Barabara na Viwanja vya Ndege,Dk.John Magufuli amekipongeza Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kwa kutekeleza Ilani ya CCM.

Aliyasema hayo jana wakati  akimkaribisha Makamu wa Rais Dk.Mohamed Gharib Bilal wakati wa  kuzindua ukarabati wa barabara  ya Nyanguge-Musoma inayopakana na mpaka wa Mikoa ya Simiyu na Mara,sherehe zilizofanyika katika kijiji cha Mmazami, Wilaya ya Butiama.

Alisema kuwa ushiriki wa Meya wa Manispaa ya Musoma (CHADEMA), Alex Kisurura  unaonyesha dhahiri kuwa anatekeza vyema ilani ya Chama cha Mapinduzi, na kusimamia vyema ujenzi wa barabara za Manispaa kwa fedha ambayo ni ya Serikali inayoongozwa na CCM.

“Serikali hii inaongozwa na Chama cha Mapinduzi,haina ubaguzi wowote,kwani  imetoa fedha jumla y a sh. Milioni 496 za ujenzi wa barabara zake na kati ya hizo  tayari wamepewa sh. Milioni 341 inaonyesha Meya huyu, Alex Kisurura  ana mwili wa CHADEMA lakini  moyo ni wa CCM tumpongeza”alisema magufuli huku akishangiliwa na wananchi.

Aliongeza kuwa “Tunawajengea barabara,km 2 kwa watembea kwa miguu na pikipiki upande wa kulia na kushoto,kama wanataka kuandamana waandamane sana ila waachie nafasi za magari kupita huku wakijua kuwa barabara hiyo imejengwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi”alisema Magufuli.

Alisema katika kuhakikisha mtandao wa barabara za lami  zinajengwa na kwamba  fedha nyingi zimetolewa katika Wilaya za Mkoa wa Mara, ambapo alitoa pongezi kwa  Serikali  ya awamu ya nne kwa jitihada zake katika kuhakikisha Mkoa wa Mara unapata maendeleo.

Wilaya zilizotengewa  fedha  ni pamoja na Serengeti Sh. Milioni 57.6, Musoma Milioni 496,Bunda Sh. Milioni 975,Butiama Sh. Milioni 334,halmashauri ya Wilaya ya Musoma Sh. Milioni 519 ,Wilaya ya Rorya Sh. Milioni 977 na Wilaya ya Tarime Sh. Milioni 854.

Aidha amelitaka Shirika la Umeme Tanesco kutoa kibanda chake ili kupisha upanuzi wa barabara ambapo hawatalipwa fidia yoyote.

Makamu wa Rais yuko ziarani Mkoa wa Mara,ambapo leo atafanya uzinduzi kivuko cha Mv.Musoma kinachofanya safari zake kutoka Musoma kwenda Kinesi Wilaya ya Rorya ambacho pia nia hadi za Rais Jakaya Kikwete kuleta kivuko kipya ili kupunguza hadha kwa wananchi.

Pia amekutana na viongozi wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Mara katika ukumbi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa.

Saturday, March 2, 2013

TENDER






PRIME MINISTER’S OFFICE
REGIONAL ADMINISTRATION AND LOCAL GOVERNMENT
RORYA DISTRICT COUNCIL
(All references should be made to the District Executive Director)

THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR,     P.O.BOX  250,                                        TARIME



 
Mara Region
 Tel     Phone Number: + 255 732 985742,     Fax Number:  + 255  732 985742               E - mail: dedrorya@yahoo.com







E






 
683E07AB
REF NO. HWR/ LGA/068/18/w/2012/2013/                     Date: 01/02/2013

NAME OF PROJECT: WATER SECTOR DEVELOPMENT PROGRAMME (WSDP)
(Rural Water Supply and Sanitation Programme Component) RWSSP
IFB TITLE:    CONSTRUCTION OF PIPED WATER SUPPLY SYSTEM AND CIVIL WORKS FOR KINESI, RANDA AND UTEGI VILLLAGES,
IFB NUMBER: TENDER No. LGA/068/16/W/2012/2013/1-3

1.      This Invitation for Bids follows the General Procurement Notice for this Project which appeared in Development Business, Issue no. WB 320-696/07 dated  January 2007

2.      The Rorya District Council has received financing from Development Partners towards the cost of Construction of Piped water supply System and Civil works for Kinesi, Randa and Utegi Villages in Rorya District council and intends to apply part of the portion of the funds to cover eligible payments under the contract for which this invitation for Bid is issued.


3.      The Rorya District Council now invites sealed bids from eligible and qualified contractors to carry out Construction of Piped water supply  System and Civil works for Kinesi, Randa and Utegi Village in Rorya District council in three (3) separate Lot whereby each Lot are independently in  biding and evaluation processes as follows:






Lot Number and name
Major works
Eligibility
CONSTRUCTION OF PIPED WATER SUPPLY SYSTEM AND CIVIL WORKS FOR KINESI VILLLAGE
IFB NUMBER: TENDER No. LGA/068/16/W/2012/2013/1
1.Kinesi  village wss sub project
i)                    Construction of Ferro cement tank for RWH (5m3), 1m3 water jar and Pour Flush Latrines for boys and girls (1 block), and provision of  2 Sim tanks of 3m3 each. Intake works from Lake Victoria
ii)                  Supply materials and construction of a sump well, power house and a fence
iii)                Supply and installation of pumping unit (a submersible pump) and submersible electrical motor of 30kW with associated fittings, switch gears gad jets
iv)                Supply pipes and fittings  and construction intake pipe line of 150mm diameter,505m long (with stainless steel pipes)
v)                  Supply pipes and fittings and construction of rising main pipe 150mm diameter, 3305m long.
vi)                Supply pipes and fittings and construction of distribution network consisting of 13,730m pipe line of different pipe sizes and classes, 26 water points(single tapped) and one cattle trough
vii)              Supply materials and construction of 4 storage tanks of total capacity of 500m3(225m3 &135m3 on ground and 90m3 and 45m3 on 6m raised above the ground level)
viii)            Extend power supply line from nearest transformer to the pump house
ix)                Construction of Ferro cement tank for RWH (5m3) and 1m3 water jar
x)                  Construction of Pour Flush Latrines for boys and girls (1 block), and provision of  2 Sim tanks of 3m3 each.




CRB Class IV and above  (Civil)




CONSTRUCTION OF PIPED WATER SUPPLY SYSTEM AND CIVIL WORKS FOR RANDA VILLLAGES
IFB NUMBER: TENDER No. LGA/068/16/W/2012/2013/2

2. Randa village wss sub project
i)          Supply and install 2 submersible pump units (electrically submersible pumps and motors), fittings, switch gears and gad jets.
ii)        Supply and install 1 electrically surface motor pump, fittings, switch gears and gad jets.
iii)      Construction of  on ground Sump well – 5m3 at the booster station
iv)      Installation of internal electricity in the power house and external electricity from the nearest transformer and Pump/power house and  fence
v)        Supply pipes and fittings and construction of rising main pipeline 50 mm diameter (63HDPE PN 10), 1,750m long (booster station), rising main pipeline 43.7mm diameter (50HDPE PN 10), 30m long (from 2boreholes to booster station) and distribution network consisting of 14,272m pipe line, 11 water points double tapped
vi)      Supply materials and construction of a storage tank of capacity 45m3 on ground level and 5hand pumps development
vii)    Nyabing’erere natural spring improvement, fencing off the spring source, construction of 2 DPs (double taps) and construction of a cattle trough.
viii)  Rain water harvesting systems construction(5m3 ferro cement tank, 1m3 water jar), Pour Flush toilets with 2 Sim Tanks(3m3 each) for rain water harvesting
ix)      Surveying, drilling, test pumping and development of one (1) additional borehole.








CRB Class V and above (Civil)
CONSTRUCTION OF PIPED WATER SUPPLY SYSTEM AND CIVIL WORKS FOR  UTEGI VILLLAGES
IFB NUMBER: TENDER No. LGA/068/16/W/2012/2013/3

3. Utegi village wss sub project
i) Supply and install 3 submersible pump units (electrically submersible pumps and motors), fittings, switch gears and gad jets.
ii) Supply and install 1 electrically surface motor pump, fittings, switch gears and gad jets and On ground Sump well – 5m3 at the booster station.
iii) Installation of internal electricity in the power house and external electricity from the nearest transformer and Construction of Pump/power house and  fence
iv) Supply pipes and fittings and construction of rising main pipeline 50 mm diameter (63HDPE PN 10), 2,000m long (booster),  rising main pipeline 43.7mm diameter (50HDPE PN 10), 1422m long (from 3 boreholes to  the booster station) and distribution network consisting of 7,375m pipe 15 water points double tapped.
v) Supply materials and construction of a storage tank of capacity 90m3 on ground level and 8 hand pumps for drilling and development
vi) Rain water harvesting systems construction(5m3 ferro cement tank, 1m3 water jar) and Pour Flush toilets with 2 Sim Tanks(3m3) for rain water harvesting
Surveying, drilling, test pumping and development of one (1) additional borehole.




CRB Class V and above (Civil)
Bidders are required to bid for all items and quantities in each phase and may bid both Lots in separate envelop.
                        
4. Bidding will be conducted through the National competitive Bidding (NCB) procedures specified in the Public Procurement Act, 2004 and the Public Procurement (Goods, Works, Non Consultancy Service and Disposal of Public Assets by Tender) Regulations, 2005 – Government Notice No. 97 and are open to all eligible bidders.

5. Interested eligible Bidders may obtain further information from and inspect the Bidding Documents at the office of the Secretary of the Tender Board, Rorya District Council, P.O Box 250, Tarime – Rorya District, TANZANIA, from 8:00 am to 3:30 pm Monday to Friday inclusive except on public holidays.

6.  A complete set of Bidding Documents in English, in hard copy and additional sets may be purchased by interested Bidders on the submission of a written application to the address given  above and upon payment of a non-