TUJIKUMBUSHE 2010:

Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM,Jakaya Kikwete alipokutana na waandishi wa habari akinadi sera na kuzungumzia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2005/2010 ilivyotekelezwa katika kipindi alipokuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ucheshi wake Rais hautasahaulika kamwe! aliweza kuchati na wapiga kura wake kwa mtindo wa kidali po!! alitamani kuwashika watu wote mikono lakini alishindwa,waliobahatika kushika mkono wake wasema hawawezi kunawa Mkono huo ulioshikwa na Rais bali,watakula chakula bila kunawa,hii iliwahi kutokea katika kijiji cha Busekela Jimbo la Uchaguzi la Musoma Vijijini ambapo ilikuwa ni mara ya kwanza kufika hapo.
Mwenyekiti Mstaafu,wa CCM na Rais wa awamu ya Tatu,Mh. Benjamin Mkapa akipeana Mkono na Mjumbe wa Halmashauri Kuu NEC,kwa sasa ndiye Makamu wa Rais, Dk.Mohamed Gharibu Bilal anayetabasamu katikati ni Rais Mstaafu wa awamu ya pili,Ally Haji Ally Hassan Mwinyi (Mzee Ruksa) kabla ya kuanza kwa kampeni Jagwani jijini Dar es Salaam.
Mgombea akinadi sera,katika tukio ambalo halitasahaulika katika kurasa za ubongo wa Mtanzania ni pale mgombea huyo alipoanguka,katika Uwanja huu wa jagwani, kwa kile kilichodaiwa kuwa ni uchovu pia mfungo,mgombea alikuwa amefunga, kipindi hiki kilikuwa kigumu kwa watanzania walio wengi kipenzi chao kuanguka ghafla.Pamoja na misukosuko yote kesho yake aliweza kuendelea na kampeni na afya yake ilikuwa njema.
No comments:
Post a Comment