Tuesday, January 29, 2013

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI NA OPERESHEN


MUSOMA

JESHI la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara limefanikiwa kufanya ukaguzi wa tahadhari na kinga ya moto  katika Manispaa ya Musoma licha za zoezi hilo kuingiwa na dosari kwa baadhi ya wamiiliki wa maduka kukataa kukaguliwa na kulipia ada ya Ukaguzi.

 Akizungumza na Uhuru  ofisini kwake, Kaimu Kamishna Mkuu wa Kikosi cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara Don Mhally  alisema kuwa kwa upande wa Wilaya zingine zoezi hilo limefanikiwa kwa kiasi kikubwa lakini kwa Manispaa ya Musoma baadhi ya wamiliki walikataa kwa kile kinachodaiwa kuwa  utoaji wa fedha bila kupatiwa kifaa cha kuzimia moto.

Alisema kuwa  baadhi ya wamiliki wa maduka waliokaa kukaguliwa wameachukuliwa sheria ikiwa ni pamoja na kufikisha Mahakamani kwa kosa la kukiuka Sheria ya ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Na.14 ya mwaka 2007 pamoja na kanuni zake za mwaka 2008(Fire Safety Inspection and Certificate) na marekebisho yake ya mwaka 2012.


Jumla ya maduka ya kawaida zaidi ya 74 yamekaguliwa na kulipia gharama ya ukaguzi na cheti na makusanyo ilikuwa ni sh. 54,590,000,ambapo kutoka Julai-Novemba 2012 jumla ya maeneo 431 yamekaguliwa na zoezi hili ni la mwaka mzima wa fedha hadi Juni 30.

Aidha wametakiwa kuwa na kifaa cha kuzimia moto ambavyo vinapatikana kwa mawakala walioteuliwa, aliwataja kuwa ni Sodobhi Investment,Dawill Trading Agency(ZK) na Musoma Equipment Agency za Mjini hapa.
 

AMBULANCE ZA PIKIPIKI ZAOTA BUIBUI





BUTIAMA.

 WAKATI Serikali inajitahidi kutoa huduma ya afya ya Mama Mjamzito na Mtoto kutotembea mwendo mrefu kutafuta huduma ya afya,pikipiki za kusaidia huduma hiyo(Ambulance)  zilizoletwa katika Wilaya ya Butiama kuhudumia wananchi zimeshindwa kusambazwa.


Pikipiki hizo mpya zipatazo nne zimehifadhiwa katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Musoma,na zimeota Buibui na uwezi kuzitambua kuwa ni pikipiki zilizoletwa kwa ajili ya kusaidia huduma ya haraka kwa wagonjwa wenye hali mbaya kutoka kijiji fulani kwenda sehemu huska ambapo kikao cha  Bodi ya hospitali tayari kilishapitisha pikipiki hizo zinatakiwa kufanya huduma katika vjiji vya Balaga, Nyegina na Masinono.


Mganga Mkuu wa Musoma,Dk.Genchwele Makenge amesema kuwa Pikipiki hizo zimeshindwa kufanya kazi kutokana na kutosajiliwa kazi ambayo ni ya Wizara ya Ujenzi pia ukaguzi kutoka kwa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Mkoani hapa.



Aidha kwa sasa gari la wagonjwa katika kituo cha afya cha Murangi limeharibika ambapo kwa sasa Wilaya ina Magari mawili ambayo hayatoshelezi kufanya huduma ya haraka kwa wagonjwa ambao hali zao zinakuwa mbaya.Wilaya ya Butiama ina vijiji 120,kata 34,Tarafa 3 na  Zahanati 59,ambapo pia alitoa wito kwa wananchi kujiunga na mfuko wa afya ambapo watalipa Sh.10,000 kwa mwaka itakayowawezesha kutoa huduma bora ambayo itasaidia kupunguza gharama kwa mgonjwa.

Akizungumzia juu ya ukaguzi wa pikipiki za wagonjwa(Ambulance) kutokaguliwa na kusababisha wagonjwa kukosa huduma hiyo,Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Reuben Mataso alisema kuwa ameshindwa kufanya hivyo kutokana na pikipiki hizo kutokuwa na usajili.


UBADHILIFU MKUBWA HOSPITAL YA RUFAA YA MUSOMA.

MUSOMA.



ZIARA ya Mwenyekiti wa Bodi ya Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Mara,Askofu wa Kanisa la Menonite kanda ya kati Amos Muhagachi imeibua mambo mengi yakiwemo wizi wa kupindukia wa fedha za kuchangia huduma ya afya, fedha  za manunuzi ya vifaa vya hospitali upande wa Ugavi (Procurement).

Mara baada ya kuteuliwa, Mwenyekiti huyo akiwa na wajumbe walipata fursa ya kutembelea wodi na sehemu ya kuhifadhia miili ya Marehemu (Mochwari) na maabara  na kubaini kasoro nyingi zikiwemo pia za uchakavu wa mabomba ya kupitisha maji taka ambayo yamezagaa ovyo na kuhatarisha maisha ya wagonjwa katika wodi namba 7.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wagonjwa waliokuwa wamelazwa katika wodi mbalimbali walilalamika uongozi uliopo kwa kutokuwa makini na kuzingatia usafi,ambapo katika wodi namba tatu na saba wagonjwa hujisaidia haja kubwa kwenye ndoo zao na kumwaga nje asububi hali ambayo imekuwa ikiibua milipuko ya wagonjwa mengine.

Aidha watumishi wa hospitali hiyo pia walipata fursa ya kutoa dukuduku zao ambapo wameiomba bodi hiyo kumfukuza Katibu wa Hospital hiyo,Faustin Bigambo,Mhasibu na Afisa Ugavi kwa kuwa wazembe na kuvuja fedha za Serikali huku wakiwa hawawajali wauguzi.

Akilalamikia fedha za kipindupindu ambazo zililetwa na Wizara ya Afya na kuliwa,Afisa Muuguzi,Musa Jackson alisema kuwa Jumla ya Sh. Milioni 78 hazijulikani zilipo tangu mwaka 2008  kwa ajili ya watumishi kuhudumia wagonjwa wa kipindupindu na kwamba mpaka sasa hawajalipwa fedha hizo.

Aidha Wizara ya Afya utoa kila mwezi jumla ya Sh. Milioni 26 kwa ajili ya uendeshaji(0c).

Naye Muuguzi Hawa Albert alitoa ombi kwa Mwenyekiti huyo kuwanusuru wafanyakazi hao kwa kuwa wamechoka kulalamika na kwani kuna malimbikizo mengi ya fedha zao zikwemo posho za wenye zamu za usiku,motisha na mashono ya nguo za wafanyakazi na makato kutoka PSPF.

Bodi hiyo ni jumla ya wajumbe 15 ambao waneteuliwa kutoka sekta mbalimbali zikiwemo,viongozi wa madhehebu ya dini,(Maaskofu na Mashehe), madaktari, wanasheria, wafanyabiashara, wanasiasa na wenye taaluma ya afya,elimu na Madaktari kati ya hao wanawake ni watatu.


OSWARD MANG'OMBE HIGH SCHOOL


                           
OSWARD Mang'ombe High School,ni shule ya Kisasa Afrika Mashariki na Kati,iliyojengwa kwa hisani ya Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini,Nimrode Elirehema Mkono.

Monday, January 21, 2013

TRA MUSOMA WAKOSA MAPATO-BUSEKELA


MUSOMA VIJIJINI


Mamlaka ya Mapato( TRA) Mkoa wa Mara hukosa mapato kutokana na makusanyo ya samaki aina zote ambapo samaki ya aina dagaa wanasafirishwa kwenda nchi  jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya watu wa kongo,kenya, Uganda,Zaire,Msumbiji na uarabuni.  



Zaidi ya tani 10,000 za samaki aina ya dagaa usafirishwa kila siku wakati wa msimu wa dagaa ukifika,kutoka kwa mfanyabiashara mwenye asili ya uarabuni ambapo amekuwa akiwatumia wakazi wa hapo kuwasafisha na kutumia chanja maalumu ya kuanika na kupakia samaki hao kwenye malori tayari kwa kusafirishwa.
 
Diwani wa kata ya Bukumi,Chomya Ndege pamoja na wananchi wa kijiji cha Busekela walishindwa kusema juu ya tatizo hilo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa alipofanya ziara yake ya kikazi na kufanya Mkutano wa hadhara katika viwanja vya Shule ya Msingi Busekela huku Diwani huyo akilalamikia mambo mengine yakiwemo ya ukahaba uliopo katika kisiwa hicho,ujambazi na uvuvi haramu.