BUTIAMA.
WAKATI
Serikali inajitahidi kutoa huduma ya afya ya Mama Mjamzito na Mtoto kutotembea
mwendo mrefu kutafuta huduma ya afya,pikipiki za kusaidia huduma
hiyo(Ambulance) zilizoletwa katika Wilaya ya Butiama kuhudumia wananchi
zimeshindwa kusambazwa.
Pikipiki
hizo mpya zipatazo nne zimehifadhiwa katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri
ya Musoma,na zimeota Buibui na uwezi kuzitambua kuwa ni pikipiki zilizoletwa
kwa ajili ya kusaidia huduma ya haraka kwa wagonjwa wenye hali mbaya kutoka
kijiji fulani kwenda sehemu huska ambapo kikao cha Bodi ya hospitali
tayari kilishapitisha pikipiki hizo zinatakiwa kufanya huduma katika vjiji vya
Balaga, Nyegina na Masinono.
Akizungumzia
juu ya ukaguzi wa pikipiki za wagonjwa(Ambulance) kutokaguliwa na kusababisha
wagonjwa kukosa huduma hiyo,Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Reuben
Mataso alisema kuwa ameshindwa kufanya hivyo kutokana na pikipiki hizo kutokuwa
na usajili.
No comments:
Post a Comment