Wednesday, August 18, 2010






Katibu wa CCM Mkoa wa Mara, Ndeng’aso Ndekubali akimkabidhi na kumtambulisha kwa viongozi wa CCM wa Wilaya ya Tarime,Mgombea Ubunge Mteule wa Wilaya ya hiyo, Nyambari Chacha Nyangwine mara baada ya kuteuliwa na NEC,kabla ya kuanza kwa kikao cha Chama kilichofanyika katika ukumbi wa CCM Wilayani hapo jana.
Picha na Eva-Sweet Musiba.


Wagombea Ubunge wateule wa CCM wa Wilaya za Rorya na Tarime wakisikiliza kwa makini maagizo kutoka kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Mara, Ndeng’aso Ndekubali hayupo pichani wakati wa kikao cha Viongozi wa CCM wa Wilaya hizo wa kuwatambulisha viongozi waliopitishwa kuipeperesha vyema bendera ya CCM wa Ubunge, Udiwani na Udiwani wa viti Maalum katika hafla fupi iliyofanyiaka katika ukumbi wa CCM Wilaya ya Tarime jana.


Katibu wa CCM Wilaya ya Rorya, Abubakar Ghati akimpokea Mgombea Ubunge Mteule wa Wilaya ya Rorya Lamek Airo,wakati wa utambulisho wa viongozi wateule wa Ubunge,Udiwani na Udiwani wa Viti Maalum Wilaya ya Tarime yaliyofanyika jana katika Ukumbi wa Wilaya katika yao ni Katibu wa CCM Mkoa wa Mara,Ndeng’aso Ndekubali.
Picha na Eva-Sweet Musiba.

Picha.Katibu Kikaoni.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mara, Ndeng’aso Ndekubali akisitiza jambo katika kikao cha Viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM,kilichofanyika jana katika Ukumbi wa CCM Wilaya ya Tarime,kulia kwake ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya hiyo ,Rashid Mbogomba
Picha na Eva-Sweet Musiba.

Baadhi ya Madiwani wateule wataopambana na vyama vya upinzani kupeperusha bendera ya CCM Wilayani Tarime katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31 mwaka huu.
Picha na Eva-Sweet Musiba.

Viongozi wa CCM Mkoa wa Mara wakisali,baada ya Katibu wa CCM Mkoa wa Mara,Ndeng’aso Ndekubali kutangaza kifo cha Mume wa aliyekuwa Naibu Waziri wa Elimu,Gaudentia Mgosi Kabaka na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, kilichotokea ghafla jana.

No comments:

Post a Comment