Mwalimu Nyerere mwaka 1985 aliposema anang'atuka wengi walipatwa na wasiwasi na wengi walimwomba aendelee kutawala ila yeye alisema kuwa muda wake umefika kikomo wa kutawala.
Inabidi Tanzania tufike wakati tusione viongozi fulani ndio lazima wawepo madarakani bali sheria na sera zetu zimfanye kila kiongozi kuweza kuongoza. Nahili kamwe halitaletwa na kiongozi bali wapiga kura wanaoelewa nini maana ya kura zao. Kila anayechukua form ya kuwa kiongozi pamoja na yote ana malengo yake binafsi, na kutuletea maendeleo ni mpaka pale malengo yake yatakapo intersect na shida za wananchi la sivyo kalabagaho tutalia sana. Sio vizuri nchi au taasisi au chama au wananchi kuwekeza nguvu zake zote kwa mtu mmoja au kwa kikundi cha watu bali kwa mfumo imara. Hivi ndivyo nchi zilizoendelea zimefanya kwani sera na mifumo yao imekuwa ndio dira ya kila kiongozi na uelewa wa wananchi wao ndio nguzo ya utawala uelewa wa waandishi wa habari kuelimisha umma umeifanya serikali na bunge zao kuwa imara na kutokuyumbishwa na upepo upitao.
Naona swala la Kabwe kuamua kuachia ngazi liwe ni maamuzi yake. nani anajua kwamba akilazimishwa kuendelea ataweza kutimiza wajibu wake, ni hatari sana kumlazimisha mtu ambaye tayari amechoka kazi husika, kwani kumlazimisha kubaki utendaji wake huwa unakuwa hafifu, mfano Raisi angekubali kujiuzulu kwa Dr. Idrisa rashid mazila anayotupatia sasa hivi tusinge yapata, hii ni kwasababu ameona thamani yake iko juu na hakuna mtanzania mwingine wa kushika kazi yake, sasa anatutenda.
Ni vyema mtu akisema libeneke limemshinda anaachia ngazi tumshukuru na tumwage kwa amani kwani hatujui kichwani kwake ana nini. Tuwe tayari kwa mabadiliko yenye manufaa na salama.
Naona ingekuwa vyema tukamkubalia Zitto akaachia siasa na kufanya anachokipenda, kwani ukisoma mistari yake yeye mwenyewe anaonyesha siasa za Tanzania zimemchosha/kumshinda kwani mara ya kwanza kasema anaachia ubunge na kwenda shule na kusaidia kukijenga chama kuanzia shina. hapo hapo kasema hana uzoefu wa uongozi hivyo atatafuta kwanza kazi ili apate uzoefu. hapo hapo kasema akimaliza shule tayari kaanza mipango ya kazi sudani au somalia.
Utajengaje chama wakati utakuwa masomoni na baada ya masomo unakwenda somali/sudani.
Pili je ni lini utapata huo uzoefu na je ni elimu ya kiwango gani anakihitaji je second degree or PHd na kama ni second ni miaka takribani miwili na sudan/somalia sijui miaka mingapi na kama ni PHd unaongelea miaka zaidi ya minne na sudan/somalia.
Ukiangalia vizuri Zitto is done on politics yeye awaage tu wapiga kura wake na aseme wazi nini kimemkuta ili awasaidie watanzania wengi vijana wenye mwelekeo wa kuingia dodoma mapema na asizungushe mbuyu, akumbuke ana haki ya kuwa au kutokuwa mbunge sio lazima na atashukururiwa kwa muda aliowatumikia watu wa Kigoma.
No comments:
Post a Comment