Wednesday, December 6, 2017
MBUNGE MATHAYO ATOA MILIONI 1.7 ZA KUONGEZA MITAJI KWA WAFANYABIASHARA.
MUSOMA.
WAKAZI wa kata ya Nyamatare wamemwomba Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini, Vedastus Mathayo kuhakikisha anawaletea maji katika soko la biashara la Nyamatare kwani wanatumia maji ya dimbwi la maji machafu yaliyochimbwa kwa ajili ya ujenzi wa Choo katika soko hilo.
Wameyasema hayo katika Mkutano wa hadhara wa kutambulisha viongozi wapya wa Wilaya hiyo waliochaguliwa katika chaguzi zilizopita wiki iliyopita.
Mkazi wa kata hiyo, Christina Mori ambaye ni mfanyabiashara katika soko hilo alisema kuwa kutokana na huduma duni ya maji iliyopo wanalazimika kuchota maji kwenye dimbwi la maji machafu kwa matumizi ya kuosha viazi vitamu ambavyo kwa kawaida huwa na udongo kutokana na kutokuwa na maji hali mbayo inahatarisha afya ya wananchi hao.
Changamoto zilizopo katika soko na kata hiyo kwa ujumla ni pamoja na huduma ya choo,uvujaji wa maji ovyo kutokana na ujenzi wa miundo mbinu ya barabara na mitaro.
Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Musoma, Magiri Maregesi ametoa wiki mbili kwa mamlaka ya maji safi na taka Manispaa ya Musoma, (MUWASA) ili wananchi waweze kupata huduma hiyo kwa ukakika kwani ulazaji wa mabomba ya maji umeishamalizika na uko mita kadhaa kuelekea katika soko hilo.
Naye Diwani wa kata hiyo, Masumbuko Magesa aliilalamikia Mamlaka hiyo kwa uzembe uliofanyika wa kutowasiliana kati ya mamlaka zote,na kusababisha mabomba ya maji kuwa ya ya mitaro ahali ambayo inahatarisha usalama wa mabomba ambayo yanaweza kuhujumiwa na ahata kuharibika.
Kwa upande wa vivuko vya barabara, Diwani huyo alilalamikia ucheleweshaji wa ujenzi wa vivuko ambao inawalazimu wananchi kupata hadha kubwa wakati wa matatizo yanapotokea hasa kwa upande wa huduma ya maziko ama panapotokea mgonjwa hali ambayo inawaletea hadha kubwa wananchi wa eneo hilo.
Akijibu hoja hiyo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma, Fidelica Muyovella alisema kuwa barabara ya Nyasho-Nyamatare-Majita inahitaji jumla ya vivuko 65 lakini vitajengwa vivuko 20.
Katika kuongeza mitaji kwa wanawake wajasiliamali, Mbunge huyo alitoa kiasi cha Sh. Milioni 1.7 akishirikiana na viongozi wapya waliochaguliwa ili kuinua uchumi wa mwanamke na kuahidi kuwajengea mabanda mengine,ikiwemo uzio na choo.
Thursday, November 30, 2017
MJUE MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CCM MKOA WA MARA (Musoma Mjini)
Mmiliki wa Blog hii akiingia katika ukumbi wa CCM Mkoa wa Mara, amechaguliwa kuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Mkoa wa Mara kutoka Wilaya ya Musoma, na alishinda kwa kishindo katika nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT Taifa, ikiwa ni Wilaya moja ya Musoma, ikiwa imeungana na Musoma Vijijini ambayo ni Wilaya kichama kwa sasa.
WAGOMBEA WAKIJINADI.
Wegesa Hassan Witimu akipiga magoti kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT Mkoa wa Mara, kuomba ridhaa ya kuwa Mwenyekiti,katika uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa CCM, Mkoa wa Mara, Wilaya ya Musoma Mjini.
WAJUE WAGOMBEA WA UWT MKOA WA MARA.
Wagombea wa nafasi ya kiti cha Umoja wa Wanawake(UWT) Mkoa wa Mara, wa kwanza ni Veronica Mwijarubi Kunenge(138), Mwajuma Hamisi Magoti(55) na Wegesa Witimu akishinda kwa kura 245.
Sunday, November 19, 2017
MAONESHO YA KILIMO MSETO MUSOMA-MARA
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adamu Kigoma Malima, akikagua mabanda ya maonesho katika viwanja vya VI- Agro forest,Bweri Musoma.
KILIMO MSETO-MUSOMA
MKUU wa Mkoa wa Mara,Adamu Malima, amesema kuwa ili kuendeleza kilimo cha mkataba cha pamba katika Mkoa wa Mara haina budi kushirikiana kwa dhati kwa vikundi vya wakulima kuwa pamoja na kuhakikisha kilimo cha pamba kinakuwa kwa kasi kwa maendeleo ya Mkoa wa Mara.
Akizungumza katika kilele cha maonesho ya kilimo mseto kwa niaba yake,yaliyomalizika jana Afisa kilimo Mkoa wa Mara, Dennis Nyakisinda alisema kuwa ili vikundi vya wakulima viweze kupata tija ya kilimo bora haina budi kituo cha sasa kilimo Mseto cha (Vi Agroforestry) cha na kanisa la AICT Dayosisi ya Mara na ukerewe kiwe kituo cha mafunzo ya kilimo mseto cha Mkoa wa Mara ambacho kitakuwa kitovu cha mafunzo ya kilimo bora na ufugaji.
‘’Kituo hiki kitakuwa kitakuwa bora cha mfano kwa masuala mbalimbali jinsi ya kupanda miti,kutambua majina ya miti, ufugaji, ukulima wa kisasa kwa ajili ya maendeleo ya mkoani hapo na nchini kwa ujumla’’Alisema Nyakisinda.
Aidha alitaka Shirika la viwanda vidogo vidogo(SIDO) Mkoa wa Mara kuhakikisha linawashaidia wajasiliamali ili wapate uwezo kwa kupata ujuzi ili waweze kuanzisha vyao wenyewe kwa ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Amesema ili kukabiliana na changamoto za tabia nchi hawana budi kuzingatia kilimo mseto ambacho ndicho kilimo pekee chenye tija.
Ameongeza kuwa wakati huu ni wakati wa mapinduzi ya viwanda na kwamba kilimo mseto ndiyo injini pekee ya maendeleo ya mapinduzi ya viwanda nchini na kwamba wakulima hawana budi kushirikiana na mashirika mbalimbali ili kuweza kufanikiwa katika kukuza uchumi wa viwanda na kuyataka madhehebu mengine kuiga mfano wa kanisa la AICT kwani bila kuwa na chakula hakuna ibada.
Amewashukuru wafadhili wa Shirika la Vi Agroforestry la nchini Sweden na Kanisa la AICT la Dayosisi ya Mara na Ukerewe kwa kuwa kipaumbele kwa kuchangia nguvu kubwa ya kupanda miti ili mkoa huo uwe na mandhari nzuri na kuzitaka na taasisi nyingine kuwaunga mkono.
Maonesho hayo ya kilimo cha mseto ya siku tatu alipambwa na mabanda ya maonesho ya bidhaa mbalimbali zikiwemo, utengenezaji wa mkaa wa udogo uliochanganywa na kinyesi cha Ng’ombe, ufugaji wa kuku wa kienyeji kwa njia ya kisasa,utengenezaji wa sabuni ya maji, mche na mbegu bora aina ya Mkombozi.
Wednesday, October 18, 2017
MWALIMU WA SEKONDARI AWA MWENYEKITI UVCCM MUSOMA VIJIJINI
Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Murangi, Martine Juma Chacha, akijieleza katika Ukumbi wa Kanisa Katoliki,kata ya Mugango, Wilaya ya Musoma Vijijini, wakati akiomba kura,aliibu mshindi kwa kupata kura 150, akifuatiwa na Jackson Nyakia kikomati ambaye alipata 124.
Thursday, June 8, 2017
Saturday, June 3, 2017
Makamu wa Rais awasili Mwitongo-Butiama
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan alipokelewa na Chifu wa kabila la Wazanaki, Chifu Japheti Wanzagi, mara baada ya kuwasili alasiri katika Kijiji cha Mwitongo,alipozaliwa na kuzikwa mwasisi wa Taifa la Tanzania mzaliwa wa Mkoa wa Mara, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
EWURA yawataka wazalishaji wa Gesi kupunguza gharama za mtungi.
BUTIAMA.
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imewataka wafanyabiashara wa mafuta ya gesi asilia kupunguza kiwango cha kununua gesi kwa watumiaji ili wananchi wa kipato cha chini waweze kuhimiri bei ya gesi na kuwasaidia katika kupunguza matumizi ya ukataji miti ovyo unosasabisha kutoweka kwa uoto wa asili ambapo kwa sasa watumiaji wa mkaa wanaongezeka na kusababisha mazingira kuharibika.
Akizungumza na waandishi wa habari katika banda la Mamlaka hiyo, kuwanja wa Mwenge-Mwitongo Wilaya ya Butiama, Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji ( EWURA) Kanda ya Ziwa,Nyirabu Musira,amesema kuwa upunguzaji wa bei utasababisha upungufu wa matumizi ya mkaa ambao ulikuwa ukitumiwa na wananchi.
Hii ni katika maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani ambayo kitaifa inafanyika kijijini Mwitongo Wilaya ya Butiama alipolelewa na kuzikwa hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Leo kuna kongamano la hifadhi ya Mazingira linaloendelea katika Ukumbi wa Romani Katoliki jirani na kanisa alilokuwa anasali Baba wa Taifa, ambapo Waziri wa Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba.
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imewataka wafanyabiashara wa mafuta ya gesi asilia kupunguza kiwango cha kununua gesi kwa watumiaji ili wananchi wa kipato cha chini waweze kuhimiri bei ya gesi na kuwasaidia katika kupunguza matumizi ya ukataji miti ovyo unosasabisha kutoweka kwa uoto wa asili ambapo kwa sasa watumiaji wa mkaa wanaongezeka na kusababisha mazingira kuharibika.
Akizungumza na waandishi wa habari katika banda la Mamlaka hiyo, kuwanja wa Mwenge-Mwitongo Wilaya ya Butiama, Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji ( EWURA) Kanda ya Ziwa,Nyirabu Musira,amesema kuwa upunguzaji wa bei utasababisha upungufu wa matumizi ya mkaa ambao ulikuwa ukitumiwa na wananchi.
Hii ni katika maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani ambayo kitaifa inafanyika kijijini Mwitongo Wilaya ya Butiama alipolelewa na kuzikwa hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Leo kuna kongamano la hifadhi ya Mazingira linaloendelea katika Ukumbi wa Romani Katoliki jirani na kanisa alilokuwa anasali Baba wa Taifa, ambapo Waziri wa Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba.
Gosol na mapambano dhidi ya Utunzaji wa Mazingira.
Mratibu wa mradi wa Shirika lisilo la kiserikali la Gosol la nchini
Finland,Heikki Lindfors kwa kushirikiana na Taasisi ya global Resource
Allience ya Madaraka Nyerere ya Mjini Musoma alitoa maelezo kwa
wananchi na waandishi wa habari waliofika katika banda la maonesho
nchini ambapo wamebuni mashine inayotumia mwanga wa jua kuoka mikate
itakayosaidia kupunguza uharibifu wa mazingira na itatoa mashine hiyo
kwa vikundi vya akina mama bure na kutoa mafunzo kwa vijana wapatao
watano ya kutengenezaji wa mashine hiyo ambayo hapo zitauzwa nchini.
Saturday, May 27, 2017
WAKALA WA VIPIMO MKOA WA MARA WACHACHAMAA
MUSOMA.
Wakala wa vipimo Mkoa wa Mara (WMA),umewataka wasafirishaji kutumia
mizani kwa mujibu wa Sheria ya vipimo sura nambari 340 pamoja na
marekebisho yake ya mwaka 2002 ambayo inamtaka kila msafirishaji
kupima mizigo inayosafarishwa.
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya vipimo duniani ,katika
ofisi za mabasi yaendayo Mikoani katika kata ya Bweri Manispaa ya
Musoma, Afisa vipimo Mwandamizi, Almachius Pastory alisema kuwa
wamiliki wa mabasi wanapaswa kuwa na mizani ili waweze kutumia vipimo
kwa manufaa yao kwa kuzingatia uzito wa gari na kuepuka ajali
sizizokuwa za lazima wawapo katika safari.
Wakizunugmza kwa nyakati tofauti baadhi ya wasafirishaji wenye mizani
wa kampuni ya Musoma express, Veronica Innocent ambaye ni Mhasibu
alisema kuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya wateja
kukataa kupimiwa mizigo yao na matokeo yakewa kupata hasara kwa
kupigwa faini katika mizani kwa kuzidisha uzito kwenye mabasi yao.
Alisema kuwa kuwa na mzani ni faida kwa wateja lakini wengi wao
wanaonekana kuwa hawana elimu ya faida ya kuwa na mzani ambayo endapo
utazidisha mzigo unasababisha uchakavu katika basi na kuwaomba
maafisa hao kutenga muda wao kwa ajili ya kutoa elimu kwa
wasafirishaji juu ya faida na hasara za kutokuwa na mzani.
Akitoa elimu kwa baadhi ya wasafirishaji katika stend ya mabasi
yaendayo Mikoani katika ofisi ya kampuni ya usafirishaji ya Ndiyo Mzee
Afisa Vipimo Mkoa wa Mara, Paulini Chilato alisema kuwa wakala wa
vipimo kazi yake ni kujua vipimo sahihi na endapo gari litazidi uzito
uliotakiwa unapaswa kupigwa faini na ili kuondoka na karaha hiyo ni
vyema uwe na mzani ili kujua kiwango sahihi kinachotakiwa cha kubeba
mzigo.
Naye Warioba Ngara wa kampuni ya usafirishaji ya Ndiyo Mzee alisema
kuwa atahakikisha kuwa na mzani huo kwani walikuwa wanafahamu mzani
unaotumika ni wa barabarani pekee na walikuwa wanatumia mzigo kwa
kuuangalia kwa macho na au kutumia uaminifu kwa mteja anapozungumza
kuwa gunia moja lenye nafaka lilijazwa mara mbili linachukua kilo
100 (lumbesa) na wanakubali kupakia katika basi.
‘’Nashukuru kupata elimu hii,nimepata ufahamu juu ya basi linapaswa
kuwa na ujazo wa kiwango kilichoandikwa kwa mujibu wa sheria,na
nimefahamu kuwa nikiwa njiani nasafiri salama nikiwa na uhakika wa
kufika salama na kuepuka faini zisizo za lazima’’Alisema Ngara.
Thursday, May 4, 2017
Banda la Monyesho-Solar Appropriate Technology-Mei Mosi
Mwalimu kutoka nchini Korea, Dk.Hong-Kyu Choi akitoa maelezo ya jinsi kifaa cha kutumia umeme wa jua na kuchaji simu kinachofanya kazi katika banda la umoja wa vijana wa Wilaya ya Serengeti waliohitimuu mafunzo ya kutengeneza kifaa hicho ambapo jumla ya vijana 91 wamehitimu,hao ni MKuu wa Magereza Mkoa wa Mara, ACP,Golleha Massunzu na Mkuu wa gereza Wilaya ya Srengeti,Masanja Maharangata.
Friday, April 28, 2017
MUSOMA YAWA YA KWANZA KUKAMILISHA MASTER PLAN.
MUSOMA
WAZIRI Wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi
amepiga marufuku ujenzi usio na utaratibu ulio nje ya mpango kazi
kabambe(Master Plan) wa 2015-2035 uliozinduliwa jana katika Manispaa
ya Musoma ambao utagharimu kiasi cha Sh. Bilioni 15 ikiwa na pamoja na
miundo mbinu.
Alisema pia kuwa ni marufuku wananchi kujenga bila kuwa na kibali cha
ujenzi kutoka katika halmashauri za miji, mji na Manispaa na kwamba
watavunjiwa nyumba zao bila kulipwa fidia yoyote.
Aidha aliagiza uongozi wa Manispaa, kitengo cha mipango miji
kuhakikisha inatumia mpango kazi huo na kutumia wataalamu wazalendo
kwa kuwapatia ushauri wa kitaalamu endapo kutakuwa na utata.
‘’Ni marufuku Wizara ya Ardhi kutumia wataalamu kutoka nje kutupangia
mji, zitumike kampuni za kizalendo,kwani tumetumia gharama kubwa
katika kupanga mji wa Mwanza na Arusha kwa kuweka kampuni za kizungu
kwa kiasi cha zaidi ya Bilioni 22, lakini katika kupanga Master Plan
ya halmashauri ya Manispaa ya Musoma kampuni ya kizalendo ya upimaji
CRM Land Consultant zimetumika Sh Milioni 288 na kazi ni nzuri na ni
kitaalamu.
Alisema kuwa serikali iko tayari kuwajengea uwezo kampuni za kizalendo
ili kuweza kupanua wigo wa wataalamu wa nchini ili kupunguza gharama
zisizo za lazima na kuongeza kazi ya urasimishaji ili mji ukae katika
Madhari nzuri.
Amewaagiza watendaji wa mitaa kusimamia kuendeleza miji kwani mji
umepangwa upya kwa kuweka masharti ya uendelezaji wa ujenzi na sio
kufanya kazi moja ya ukusanyaji wa mapato kwani rasilimali zilizopo
zikitumika zitasaidia kukuza uchumi na kutoa hati kwa wananchi ili
ziwasaidie kuchukua mikopo itakayowasaidia kufungua biashara kubwa
ambayoo itawaingizia halmashauri mapato.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Manipaa hiyo Joseph Masero alisema kuwa
Manipaa ya Mji wa Musoma ilipata hadhi ya kuwa Manipsaa mwaka 2005 na
mchakato wa kupata mpango kazi kabambe ulianza mwaka 2013 ambapo
Manispaa ndiyo ya kwanza nchini Tanzania kuwa na mpango kazi kabambe
(Master Plan).
Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Vicent Naano alisema kuwa mpango kazi huo
utasaidia kuondoa ujenzi holela ili Manispaa iweze kupata eneo la
ujenzi wa viwanda ili kutekeleza Ilani ya CCM na sera ya serikali ya
kuwa na kuwa na viwanda na kuondoa tatizo la ardhi.
Aidha Profesa John Lupala Mkurugenzi alisema kuwa mara baada ya
kurekebishwa kwa sheria mbalimbali za ardhi mipango ilianza kufanywa
kwa kuanza kuandaa mipango iliyoandaliwa ni 26 katika miji 18
lakini kati ya miji hiyo ni Manispaa ya Musoma pekee ndiyo
imekamilisha mpango kazi (Master Plan).
Mtaalamu Mshauri wa kampuni ya mpango kazi kabambe ya (CRM Land
Consultant),Clara Kweka Msale aliwapongeza wataalamu walioshirikiana
nae kuhakikisha wanapanga mji huo ambapo kazi hiyo ilishirikisha
wadau wote.
WAZIRI Wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi
amepiga marufuku ujenzi usio na utaratibu ulio nje ya mpango kazi
kabambe(Master Plan) wa 2015-2035 uliozinduliwa jana katika Manispaa
ya Musoma ambao utagharimu kiasi cha Sh. Bilioni 15 ikiwa na pamoja na
miundo mbinu.
Alisema pia kuwa ni marufuku wananchi kujenga bila kuwa na kibali cha
ujenzi kutoka katika halmashauri za miji, mji na Manispaa na kwamba
watavunjiwa nyumba zao bila kulipwa fidia yoyote.
Aidha aliagiza uongozi wa Manispaa, kitengo cha mipango miji
kuhakikisha inatumia mpango kazi huo na kutumia wataalamu wazalendo
kwa kuwapatia ushauri wa kitaalamu endapo kutakuwa na utata.
‘’Ni marufuku Wizara ya Ardhi kutumia wataalamu kutoka nje kutupangia
mji, zitumike kampuni za kizalendo,kwani tumetumia gharama kubwa
katika kupanga mji wa Mwanza na Arusha kwa kuweka kampuni za kizungu
kwa kiasi cha zaidi ya Bilioni 22, lakini katika kupanga Master Plan
ya halmashauri ya Manispaa ya Musoma kampuni ya kizalendo ya upimaji
CRM Land Consultant zimetumika Sh Milioni 288 na kazi ni nzuri na ni
kitaalamu.
Alisema kuwa serikali iko tayari kuwajengea uwezo kampuni za kizalendo
ili kuweza kupanua wigo wa wataalamu wa nchini ili kupunguza gharama
zisizo za lazima na kuongeza kazi ya urasimishaji ili mji ukae katika
Madhari nzuri.
Amewaagiza watendaji wa mitaa kusimamia kuendeleza miji kwani mji
umepangwa upya kwa kuweka masharti ya uendelezaji wa ujenzi na sio
kufanya kazi moja ya ukusanyaji wa mapato kwani rasilimali zilizopo
zikitumika zitasaidia kukuza uchumi na kutoa hati kwa wananchi ili
ziwasaidie kuchukua mikopo itakayowasaidia kufungua biashara kubwa
ambayoo itawaingizia halmashauri mapato.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Manipaa hiyo Joseph Masero alisema kuwa
Manipaa ya Mji wa Musoma ilipata hadhi ya kuwa Manipsaa mwaka 2005 na
mchakato wa kupata mpango kazi kabambe ulianza mwaka 2013 ambapo
Manispaa ndiyo ya kwanza nchini Tanzania kuwa na mpango kazi kabambe
(Master Plan).
Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Vicent Naano alisema kuwa mpango kazi huo
utasaidia kuondoa ujenzi holela ili Manispaa iweze kupata eneo la
ujenzi wa viwanda ili kutekeleza Ilani ya CCM na sera ya serikali ya
kuwa na kuwa na viwanda na kuondoa tatizo la ardhi.
Aidha Profesa John Lupala Mkurugenzi alisema kuwa mara baada ya
kurekebishwa kwa sheria mbalimbali za ardhi mipango ilianza kufanywa
kwa kuanza kuandaa mipango iliyoandaliwa ni 26 katika miji 18
lakini kati ya miji hiyo ni Manispaa ya Musoma pekee ndiyo
imekamilisha mpango kazi (Master Plan).
Mtaalamu Mshauri wa kampuni ya mpango kazi kabambe ya (CRM Land
Consultant),Clara Kweka Msale aliwapongeza wataalamu walioshirikiana
nae kuhakikisha wanapanga mji huo ambapo kazi hiyo ilishirikisha
wadau wote.
WAZIRI LUKUVI AGAWA HATI MILIKI
SIMIYU
WAZIRI Wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi
amewakabidhi wakazi wa mji mdogo wa Lamadi Wilaya Busega Mkoa wa
Simiyu hati miliki za viwanja na kuagiza kuvunjwa kwa nyumba
zitakazojengwa kiholela mara baada ya kukamilisha mpango kazi
kabambe(Master Plan) katika Wilaya hiyo.
Zoezi hilo lililofanyika katika viwanja vya mikutano vya stooni ,
Lamadi wilayani humo lililoshuhudiwa na wananchi, huku akitoa elimu
kwa wananchi walioonekana kuhamasika kuwa na makazi bora mara
watakapopata hati miliki ili waweze itakayowawezesha kukopa na
kufungua biashara zao na kuondokana na umasikini.
Alisema kuwa lengo la serikali la kufanya urasimishaji huo ni
kuwataka wananchi kuweza kupata hati zitakazowasaidia kukopesheka
kwenye mabenki ili kujikwamua kiuchumi .
‘’Rais ameniagiza kuja kurasimisha ili wananchi muweze kupata makazi
yaliyo bora na ili kuondokana na makazi holela na kupata hati miliki
za viwanja ili muweze kukopesheka,ukiwa na hati unakuwa umefunga ndoa
ya halali ambayo ni mkataba halali na serikali ambao utakuwa unalipia
kodi ya ardhi kila mwaka na bila kubugudhiwa na Mkuu wa Wilaya au
Mtendaji wa kata’’. Alisema Lukuvi.
Aidha amewataka wananchi kutumia fursa ya hofa ya punguzo ya kulipia
asilimia 2 iliyotolewa na Rais Dk. John Magufuli katika kufanya
urasimishaji wa mpango kazi kabambe(Master Plan ) ili kuendeleza mji
huo kuwa wa kibiashara ambayo kufikia Juni 30 mwaka huu ndio mwisho
na kuweza kupata hati miliki.
Aliongeza‘’Kuna nyumba nyingi ambazo zimejengwa kiholela lakini rais
ametoa hofa rasmi ambapo leo nimekuja kutoa hati 122 kwa atakae ipata
ndio dhamana itakayomwezesha aweze kukuza uchumi wake ambao ni mtaji
wa maendeleo na kuondokana na umaskini’’.
Akiongea kwa hisia kali alisisitiza‘’ Serikali haiwezi Kuja
kuhalalisha maovu tu kila siku na kurasimisha na kutoa hati kwa
makosa yanayofanyika hivyo tumieni hofa hiyo mliyopewa ili
kuhakikisha wananchi wote wa mji wa Lamadi mnafanya urasimishaji wa
kupata makazi yaliyo bora, ili mpima atakapokuja asilazimike kuvunja
nyumba ili uweze kujenga nyumba upya,lakini kwa hawa waliopata
hati,mpango kazi ukija na ikalazimika eneo lile aidha ni barabara
inapita,italazika alipwe,lakini kama hiyo nyumba utakuwa umejenga bila
kibali itavunjwa hata kama umejenga ghorofa.’’Alisisitiza Lukuvi.
Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Busega Anderson Mbiginya akisoma
taarifa ya maendeleo ya wilaya hiyo alisema katika kipindi cha
kuanzia oktoba 2016 hadi sasa halmashauri hiyo imefanya upimaji wa
awali wa miundombinu ikiwemo ya shule, zahanati, malambo, majosho na
mabanio ipatayo 102 kati 180 sawa na aslimia 56.67na kufanya
urasimishaji wa makazi yanayoendelezwa kiholela na kutambua miliki
imekamilika kwa kupata viwanja 5,223 na upimaji wa awali viwanja
4,950.
Alisema umilikishaji wa viwanja ulianza Aprili mwaka huu katika eneo
la Lamadi ambapo hadi sasa hati 138 zimeandaliwa na kati ya hizo 122
zimekamilika na zimekabidhiwa .
Alisema kuwa kupitia urasimishaji serikali imefanikiwa kuongeza
mapato yatokanayo na tuzo na huduma za ardhi kwani zaidi ya shilingi
milioni 22.3 zimekusanywa katika kipindi cha wiki mbili na inakadriwa
kuwa shilingi 315 .4 zitakusanywa ikiwa viwanjwa 1,934 vilivyokamilika
kupimwa vitamilikishwa.
Alisema kuwa licha kuwa na mafanikio hayo kuna changamoto
zinazowakabili ambazo ni umbali mrefu wa upatikanaji wa huduma ya
baraza la Ardhi wilaya ambapo kwa sasa wananchi wanapata huduma ya
baraza la ardhi wilaya ya Maswa ambako ni wastani wa km 150 na
darubini ya kupimia (Total Station).
Nao baadhi ya wakazi wa eneo hilo waliopata hati waliishukuru serikali
kwa kuwaletea huduma hiyo kikanda ambapo kwao ilikuwa ni ndoto.
Akizungumza na gazeti hili, Mkazi wa mji mdogo wa Lamadi, ambaye ni
mwanamke,Lyabubi Gatulwa Mkelebe ambaye alichukua hati 3 alisema hati
hizo atatumia kwa kuweza kukopa benki ili aweze kuongeza hekali 50 za
kulima mpunga kwa njia ya kisasa ambapo kwa sasa ana heka 13 za
mpunga.
Saturday, April 15, 2017
Profesa Muhongo awataka wananchi kuzingatia elimu
MUSOMA.
MBUNGE wa Jimbo la Musoma vijijii na Waziri wa Nishati na Madini Pro. Sospeter Muhongo amewaomba wananchi kuweka jitihada kubwa katika sekta ya elimu kwani ndio pekee itakayoleta manufaa katika kukuza uchumi wa familia na Taifa.
Ameyasema hayo jana katika kijiji cha Bugoji, Muhoji na Chumwi katika ziara yake ya kukgua ujenzi wa vyumba vya madarasa na kuongea na wananchi katika mikutano ya hadhara ambayo ilifanyika katika shule za msingi za Kanderema .
Aidha amewataka wananchi kutobakia kulalamika badala yake waongeze bidii katika utendaji wa shughuli za maendeleo ikwemo kilimo ili kuweza kuondokana na matatizo mbalimbali ya maisha.
Licha ya hayo akizungumzia juu ya mradi wa maji , aliwaeleza wananchi kuwa katika miradi mingine kama vile maji inasimamiwa na halmashauri na kwamba serikali inafanya kazi kwa mpangilio hivyo madiwani ndio wanapaswa kusimamia suala la maji kwa kuweka katika vikao vyao ili atakaposhughulikia suala hilo iwe rahisi.
Akizungumzia suala upungufu wa chakula amesema ni aibu sana kusema kuwa mna njaa huku mnazungukwa na ziwa,sisi ndo tungekuwa watu wa kwanza kusambaza chakula katika mikoa mingine, lakini kwa sasa ni tofauti, tunaomba chakula kutoka mikoa ya Mbeya,tubadilike kutoka kilimo cha kutegemea mvua na sasa tulime kilimo cha umwagiliaji, kwani shamba kama la Bugwema lipo na halitumiki’’ Alisema Muhongo.
Naye katibu wa Mbunge wa jimbo hilo Ramadhan Juma alisema Pro. Muhongo amekwishaleta vifaa vya ujenzi ambapo jumla ya mifuko ya saruji ipatayo 1269 na mabati 5120 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa shule za msingi 111 na sekondari 20 ambapo mgawanyo wa saruji katika ukanda wa Bukwaya shule 13 kati shule 18 ,ukanda wa mugango 13 kati ya 24, ukanda majita 40 kati ya shule 69.shule 4,majita shule 2.
Sunday, February 19, 2017
ANNE MAKINDA ASEMA MFUKO WA NHIF UTOE HUDUMA BORA.
MWENYEKITI wa Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa, Mheshimiwa Anne Makinda amesema kuwa endapo mfuko wa bima ya afya utatoa huduma nzuri watanzania watakuwa na afya bora,hivyo ni vyema kujenga mfuko huo kwa kutoa huduma bora zinazowaridhisha wateja kwani ndio mkombozi kwa watanzania na kumekuwapo na tabia za baadhi ya wauguzi na madaktari kuwa kikwazo pindi wanapotakiwa kuhudumia wagonjwa wanaotibiwa kwa mfuko huo hali inayowalazimu wananchama kwenda kupata huduma ya matibabu katika maeneo mengine na kuwataka watanzania kubadilika.
Amewataka watoa huduma kuwa na moyo wa unyenyekevu wakati wanapohudumia wagonjwa na sio kuwatolea matusi na kejeli na endapo atabainika atachuliwa hatua za kinidhamu kwani wakifanya hivyo nikuchafua mfuko wa Bima.
Aidha uongozi wa bodi hiyo pia umeonesha kusikitishwa na tabia za baadhi ya wauguzi na madaktari wanaouhudimia wagonjwa katika zahanati, vituo vya afya na hospitali za serikali kuwabagua, kuwanyanyasa na kuwajibu kwa lugha za matusi wagonjwa wanaopatiwa matibabu wanaofika kutibiwa kupitia mfumo wa kadi zinazotolewa na mfuko huo.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara, Dk. Charles Mlingwa aliwakemea vikali madaktari wa zahanati, vituo vya afya na hospitali zote za serikali na kuwataka kuzingatia usawa na maadili pindi wawapo katika majukumu yao na yeyote atakayeenda kinyume hatua za kinidhamu zitachukiliwa dhidi yao.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wadau wa mfuko wa bima ya afya wakalalamika upungufu wa watumishi katika vituo vya serikali na kumwomba mwenyekiti huyo alete watumishi katika vituo hivyo ili wananchi waweze kunufaika na mfuko wao.
Mchungaji Musa Marwa ambaye ni mtoa huduma alisema kuwa kuna tatizo kubwa katika kutoa huduma kutoka serikalini na kwamba wamebaki kulalamika kila siku lakini utekelezaji wake umekuwa mgumu kuwarekebisha wahudumu wa afya kwa kuwa wana lugha chafu katika kuwahudumia wagonjwa.
Naye Mkurugenzi wa halmashauri ya Musoma vijijini, Frola Yongolo amesema endapo kuna uwezekano wa kutoa mikopo kutoka katika mfuko huo ni vyema apewe mkopo wa kufanya ukarabati wa majengo katika eneo lake vikiwemo vitendea kazi na samani.
Kaimu Mkurugenzi wa Bima ya Afya (NHIF),Bernard Konga Changamoto huduma zisizorithisha kutoka kwa wananchi, msongamano mkubwa wa wagonjwa,unyapaa kwa wanachama wa bima ya afya,vituo vyingi vya serikali vina upungufu wa dawa katika vituo vya kutolea huduma,madai kutoka kwa watoa huduma kuwa na utata ambao umekuwa na udanganyifu ambalo si jambo zuri kwa mstabali wa mfuko wa bima hivyo ni vyema serikali ikawa na chombo cha uthibiti wa madawa kama EWURA walivyo.
Akijibu hoja za watoa huduma kuhusiano na dawa ambazo zinazosema hazipo kwenye bima amesema kuwa wao wanatoa kufuatia mwongozo wa serikali na juu ya suala la kadi za wanachama zitakuwa zinapatikana kikanda ambapo kanda za Mwanza, Mbeya, Arusha na Dodoma zimeundwa na kuhusu ya madai ya malipo ya watoa huduma taratibu zifanywa ili waweze kulipwa.
Saturday, February 18, 2017
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AMEUFUNGA MGODI WA DHAHABU WA BUHEMBA.
WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ameufunga mgodi wa dhahabu wa Buhemba kutokana na kutokithi vigezo vya uchimbaji wa madini kutokana na maafa ambayo huwa yanatokea katika mgodi huo mpaka pale taratibu za kisheria zitakapokamilika.
Akizungumza na wachimbaji wadogo wadogo wa madini katika eneo la Irasanilo kijiji cha Biatika kata ya Buhemba kitongoji cha Ikoma ‘B’ Wilaya Butiama Mkoani Mara alisema kuwa serikali inapata hasara kubwa katika kutoa misaada mbalimbali yanapotokea majanga.
Aidha ametoa agizo kwa Shirika la Madini Taifa (STAMICO) na Wizara ya Nishati na Madini kupima eneo ili kujua lina ukubwa kiasi gani sambamba na kuweka mipaka ya eneo hilo(Beacon) ili kuweza kuwakabidhi wachimbaji wadogo wadogo kuendesha kazi ya uchimbaji katika eneo hilo.
Kamishina wa madini, Lucas Mlekwa alisema kuwa STAMICO inafanya utaratibu wa kuwagawia eneo hilo wachimbaji hao na kwamba taratibu zinafuatwa ili kuwakabidhi eneo hilo na kuhakikisha wachimbaji wengine ambao hawana maeneo wanapata na sio kuwamilikisha wachimbaji wale wale.
Katika ajali ya iliyotokea februari 13 mwaka huu,Samrya Zablon ambaye ni mmilikiwa eneo hilo alimdhibitishia Waziri Muhongo kuwa jumla ya wachimbaji wapatao 18 walikuwemo katika shimo hilo na kati ya hao 17 walijorodhesha majina yao na mmoja hakujiorodhesha jina wakati anaingia, lakini alitambuliwa na kwamba watatu walipoteza maisha, akiwemo Joseph Salige,Babuu Okungu wa Wilaya ya Rorya ambao miili yao imepatikana na maziko yamefanyika na Peter James(31). ambaye amenaswa hajapatikana na jitihada za uokoaji zinaendelea.
Uokoaji katika mgodi huo unaendelea kufanyika kwa kushirikiana na mgodi wa North Mara ambao wameleta wataalamu na vifaa vya uokoaji, Jeshi za zimamoto, Msalaba mwekundu, Polisi, Mgambo na wachimbaji wa eneo hilo ambapo Baba mzazi wa marehemu huyo James Matiko alithibitisha kuwa mnamo februari 13 mwaka huu mwanae Peter James aliingia kwenye duara hilo lakini mpaka sasa hajaonekana ambapo aliiomba ushirikiano ili mwanae aweze kupatikana na taratibu za maziko zifanyike.
Thursday, January 19, 2017
MKOA WA MARA UNA UPUNGUFU WA CHAKULA
MUSOMA-MARA.
SERIKALI Mkoani Mara inawadhibitishia wananchi kuwa hakuna tatizo la ukosefu wa chakula kutokana na akiba iliyopo ya tani 461,000 ya ziada ya chakula iliyovunwa kwa mvua za vuli za mwaka 2015 /2016 pamoja na hayo Mkoa wa Mara una jumla ya idadi ya watu Milioni 1,700,000 na ifikapo Disemba inakadiliwa kuwa na watu Milioni 2, ambapo Mkoa unajitosheleza kwa tani 544,525 kwa mwaka mzima hivyo Mkoa una upungufu wa jumla ya tani 83,525.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana Mkuu wa mkoa wa Mara Dk. Charles Mlingwa amesema kuwa pamoja na hali ya mvua za vuli kutokuwa nzuri lakini jumla ya tani 953,000 zilivunwa baada ya kulima ekari asilimia 42.
Dk. Mlingwa amesema kuwa ziada ya chakula ya tani 461,000 zilizopo mkoani hapo zina uwezo wa kujilisha mwaka mzima kwa kufikia mwezi mei hadi Agosti mwaka huu maana hata mvua za masika za mwaka 2016 kwani katika wilaya za Tarime ,Rorya, Serengeti na Butiama ambapo jumla ya tani 953,000 zilivunwa.
Amesema kuwa kutokana na asili ya watu wa mkoa huo kutumia nafaka aina mahindi , Mhogo na Mtama wamekuwa na dhana kuwa kunapotokea upungufu wa nafaka hizo wanadai kuna njaa wakati wanao uwezo wa kutumia nafaka nyingine kama vile mchele kwa kusaga unga wake na kusonga ugali pamoja na vyakula vingine kama vile viazi mbatata ,ndizi na vinginevyo.
Aliongeza kuwa mkoa ulikuwa na lengo la kuzalisha tani milioni 1,864,900 lakini kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa lengo hilo halikuweza kufikiwa ambapo ekari 280,000 zilitarajiwa kulimwa na kuzalisha mavuno ya tani 760,000 kama hali ingekuwa ya hewa ingekuwa nzuri.
Mpango kabambe wa kuanzisha kilimo cha umwagiliaji umeandaliwa, ambapo kila halmashauri zimetakiwa kuandaa bajeti ya mradi huo kwa mwaka 2016/2017.
SERIKALI Mkoani Mara inawadhibitishia wananchi kuwa hakuna tatizo la ukosefu wa chakula kutokana na akiba iliyopo ya tani 461,000 ya ziada ya chakula iliyovunwa kwa mvua za vuli za mwaka 2015 /2016 pamoja na hayo Mkoa wa Mara una jumla ya idadi ya watu Milioni 1,700,000 na ifikapo Disemba inakadiliwa kuwa na watu Milioni 2, ambapo Mkoa unajitosheleza kwa tani 544,525 kwa mwaka mzima hivyo Mkoa una upungufu wa jumla ya tani 83,525.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana Mkuu wa mkoa wa Mara Dk. Charles Mlingwa amesema kuwa pamoja na hali ya mvua za vuli kutokuwa nzuri lakini jumla ya tani 953,000 zilivunwa baada ya kulima ekari asilimia 42.
Dk. Mlingwa amesema kuwa ziada ya chakula ya tani 461,000 zilizopo mkoani hapo zina uwezo wa kujilisha mwaka mzima kwa kufikia mwezi mei hadi Agosti mwaka huu maana hata mvua za masika za mwaka 2016 kwani katika wilaya za Tarime ,Rorya, Serengeti na Butiama ambapo jumla ya tani 953,000 zilivunwa.
Amesema kuwa kutokana na asili ya watu wa mkoa huo kutumia nafaka aina mahindi , Mhogo na Mtama wamekuwa na dhana kuwa kunapotokea upungufu wa nafaka hizo wanadai kuna njaa wakati wanao uwezo wa kutumia nafaka nyingine kama vile mchele kwa kusaga unga wake na kusonga ugali pamoja na vyakula vingine kama vile viazi mbatata ,ndizi na vinginevyo.
Aliongeza kuwa mkoa ulikuwa na lengo la kuzalisha tani milioni 1,864,900 lakini kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa lengo hilo halikuweza kufikiwa ambapo ekari 280,000 zilitarajiwa kulimwa na kuzalisha mavuno ya tani 760,000 kama hali ingekuwa ya hewa ingekuwa nzuri.
Mpango kabambe wa kuanzisha kilimo cha umwagiliaji umeandaliwa, ambapo kila halmashauri zimetakiwa kuandaa bajeti ya mradi huo kwa mwaka 2016/2017.
Sunday, January 1, 2017
TATIZO LA UVAMIZI WA TEMBO KUTOWEKA
SERENGETI.
SERIKALI kupitia wizara mbalimbali itaangalia upya uwezekano wa kutatua matatizo ya uvamizi wa wanyama aina ya Tembo wanaoharibu mazao ya wananchi.
Naibu Waziri wa Mali asili na Utalii, Mhandisi, Ramo Makani aliyasema hayo katika uwanja wa ndege wa Ikorongo baada ya kumaliza ziara yake katika Wilaya ya Serengeti, kutokana na hali asili aliyoina serikali kupitia Wizara zote nne itaangalia uwezekano wa kuangalia na kupitia upya na kuweka mikakati ya kuzuia wanyama hao wasiharibu mazao ya wananchi.
''Tuna Wizara zinazohusika na masuala mbalimbali, ikiwemo,ya Ardhi, Mifugo, Maliasili, na nyingine tutakaa kwa pamoja kuangalia changamoto zilizopo,nimeona kuna watu wanaishi kihalali na ni vijiji vilivyopo kwa mujibu wa sheria vinapakana sana na mapori ya akiba ya Ikorongo na Grumeti ambavyo kwa sasa vimekuwa vimekuwa vikivamiwa mara kwa mara’’Alisema Makani.
Akiwa katika kijiji cha Makundusi Wilaya ya Serengeti kinachopakana na mapori ya akiba alishuhudia wanyama hao walivyobomoa nyumba katika tukio lilitokea oktoba mwaka jana na kusababisha madhara makubwa ya kuhama kwa familia mbili ikiwemo ya Malimi Nyamuhanga yenye jumla ya wakazi 10 na nyingine ambapo wanyama hao walikula chakula chote kilichokuwa ndani ya nyumba.
Alisema kutokana na wananchi kuishi katika njia za mapitio ya wanyama(shoroba) na mabadiliko ya wanyama kwa kuvamia majumba ya watu na kula chakula na kuvamia mashamba ni jambo jipya ambalo linatizamwa kwa upana wake.
Akizungumza katika majumuisho ya ziara hiyo katika ofisi za pori la akiba la Ikorongo,Afisa wanyamapori Wilaya ya Serengeti, John Meitamei (DGO) alisema kuna ongezeko kubwa la wanyamapori aina ya Tembo,na wao kuwa na tabia ya kukumbuka walikotokea, mabadiliko ya tabia nchi, kumesababisha waingie katika maeneo ya wakazi na kusababisha madhara, hivyo wanaiomba serikali kunusuru wananchi wasipate matatizo.
Alisema kuwa wameweka mikakati mbalimbali ya kunusuru ikiwemo ya ujenzi wa uzio wa umeme ili wanyama hao wasiingie kwenye makazi ya watu pia wameiomba Wizara kuongeza vitendea kazi yakiwemo magari ya kuweza kufanya doria ya mara kwa mara ili wananchi waweze kuvuna mazao yao na kuunda kikosi kazi cha ulinzi kitakachoshirikiana na wananchi.
Akiwa katika kijiji cha Mugeta Wilaya ya Bunda katika mkutano wa hadhara, wananchi hao walimwomba Naibu Waziri huyo kuwasaidia chakula cha njaa haraka, ili kuwanusu na njaa kwani kwa sasa debe moja la mahindi linauzwa Sh.21,000 na kwamba endapo Serikali hatachukua hatua za makusudi debe la mahindi wiki ijayo litafikia sh.40,000.
Aliagiza kikosi dhidi Ujangili (KDU) na magari yaliyokuwa yakilinda mwaka wa juzi yaanza doria na vikundi vya ulinzi vya vijana viundwe na vitambuliwe na Serikali ili viendelee kulinda katika kijiji cha Maliwanda Wilayani humo ambapo alitoa tochi zipatazo 200 kwa ajili ya kufukuzia wanyama hao.
LADY DJ DEE KUTUMBUIZA DREAM GARDEN-MUSOMA.
MWANAMUZIKI mahili kutoka Mkoa wa Mara, Lady Jay De usiku huu anatoa Burudani kabambe katika Resort ya Dream garden iliyopo katika Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara ambapo atawaburudisha wakazi wa Mkoa wa Mara.
Hapa niko na Mkurugenzi wa Resort hiyo Abbas Chamba ambaye amesema kuwa huduma kubwa itatolewa katika bar hiyo ambayo kwake ameitaja kuwa ni ya aina yake katika Mkoa na Manispaa na yenye sifa kwa kuwa iliweza kujumuisha wagenii wa kitaifa katika Mkutano mkuu wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ALAT mwaka ulioisha ambapo tuzo ya kimataifa ya Tanzania Mayors Award ilifanyika katika ukumbi huu.
Mwaka mpya huu utawafurahisha wakazi wa Mkoa wa Mara waishioo nje na ndani ya nchi kupata burudani ya kipekee kwa kuwa watajumuika na mwimbaji wa kitaifa na kimataifa wa nyimbo za Kiswahili ambaye pia Mkoa wa Mara ndio makazi yake rasmi kwa kuwa ni mzaliwa wa Mkoa huu.
Lady Jay Dee atatumbuiza nyimbo zote alizoziiimba mwaka wa jana ukiwemo 'Ndi, Ndi, Ndi, ulio na washabiki wengi ncbi na nyingine za zamani.
Nao washabiki wa muziki wake bila kutaja majina wamesema kuwa ni mwanamziki anayefaa, na kumtaka achukue wanaziki wengine wenye uwezo ambao wapo katika Mkoa huu, akisemo mwimbaji mwenye sauti mithili ya Kasuku, Abdalla Ukwaju anayeibia bendi ya Magereza ya Mkoa wa Mara.
Subscribe to:
Posts (Atom)