“PRESS RELEASE”
TAREHE 09/09/2011
TAARIFA YA KIFO CHA MAREHEMU
RICHARD S/O MASATU
Mnamo tarehe 08/08/2011 majira ya saa nne na nusu ukiku huko Igoma (W) Nyamagana jijini Mwanza, RICHARD S/O MASATU, ambaye kwa sasa ni marehemu mika 39 Mjita na aliyekuwa Mkurugenzi wa gazeti la Kasi Mpya la Jijini Mwanza, mkazi wa Nyakato aliokotwa eneo la barabara kuu itokayo Mwanza kwenda Musoma akiwa na majeraha.
Majeruhi alikutwa hatua chache toka eneo la Namda bar/hotel barabara iendayo Musoma kutoka Mwanza.
Tumefanikiwa kupata na kuwahoji watu walioshuhudia tukio
Majeraha aliypata marehemu katika ajali hiyo ni
1. Michubuko kwenye mguu wa kushoto
2. Mvunjiko wa ndani mguu wa kushoto
3. Michubuko na majeraha upande wa kulia wa paji la uso
4. Michubuko katika mkono wa kulia na kushoto
5. Alipasuka bandama na pia alipata majeraha makubwa sehemu ya kichwa.
Kesi iliyobaki kwetu ni kuongeza juhudi za kuipata gari lililosababisha kifo hiki ili tuweze kumuhoji na kumfikisha mtuhumiwa mbele ya sheria.
RAI
Ninatoa wito kwa wananchi wenye mapenzi mema ambao wanaweza wakawa na taarifa za tukio hili lililopelekea kifo cha marehemu RICHARD S/O MASATU zikiwemo za gari lililomgonga. Pamoja na utalaamu wetu katika upelelezi, wananchi wanayo nafasi kubwa
(LIBERATUS BARLOW – ACP)
KAMANDA WA POLISI (M) MWANZA
kifo cha Mwandishi Masatu ni mauaji na si ajali.
ReplyDelete