MWANZA.
NI wiki Moja baada ya
ya maziko ya yaliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa
Polisi (ACP ) liberatus Barlow,Jeshi la Polisi limewataja watuhumiwa wa mauaji
yake.
Kamanda Barlow
aliuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi usiku wa
kumakia Oktoba 13, mwaka huu.
Barlow mwenye Umri wa Miaka 52 aliuawa usiku wa
manane eneo la Kitangiri, Wilaya ya
Ilemela, Mkoa wa Mwanza, baada ya kutoka kwenye kikao cha harusi,
alipokwenda kumshusha Mwalimu Doroth Moses, aliyekuwa amempa lifti.
Mkuu wa Jeshi la
Polisi.IGP Said Mwema, akizungumza na
vyombo la habari amesema polisi inawashikilia watu 10 wakituhumiwa kuhusika na
mauaji yake.
IGP aliwataja kuwa ni Muganyizi Peter mwenye umri wa miaka (36)
aliyemkamatwa Jijini Dar es Salaam kuwa anadaiwa kuwa ndiye aliyempiga risasi kamanda Barlow.
Wengine waliokamatwa
Jijini Dar Es Salaam ni Chacha Mwita
(50), Majinge Marwa (48), Edward Kusoka( na Bhoke Marwa (42).
Kwa Mujibu wa IGP Mwema watuhumiwa hao
walipatikana an bunduki mbili, ikiwemo Shotgun Greenner iliyokatwa kitako,
inyaodaiwa ilitumika katika mauaji hayo.
Walikamatwa pia na
silaha aina ya Pump Action na simu ya upepo
ya kamanda Barlow.
Amesema watuhumiwa wengine waliokamatwa jijini Mwanza ni Mwalimu
Doroth(42), Felix Felician (50), Fumo Felician (40), Bahati Lazaro (28) na Amos
Bwire Bonge (30).
Kwa mujibu wa IGP Mwema, watuhumiwa hao wapo katika
mtandao wa ujambazi na wamekiri kuhusika katika matukio mengine matatu ya
ujambazi Mkoani Mwanza, kabla ya wenzao kukimbilia Jijini Dar es Salaam, baada
ya mauaji ya Kamanda Barlow kufanyika.
IGP SAID MWEMA,
amesema kukamatwa kwa watuhumiwa hao ni kunatokana
na simu ya Mwalimu Doroth waliyokuwa wakitumia baada ya mauaji.
Watuhumiwa wawili
waliokimbia Jijini Dar wanasakwa.
Hongera jeshi la
polisi kwa kazi nzuri mliyoifanya, pia hongera TCRA kwa ufuatiliaji kwa njia
mtandao.
Vitendo hivi
vithibitiwe si kwa kamanda tu bali kwa mauji mengine ya raia pia.