DODOMA.
Mlemavu wa Ngozi Fatma Jumbe Mwalimu amejitokeza kugombea
Ujumbe NEC viti 6 na Baraza kuu Taifa
viti vitano Bara
Akiwa katika ofisi za Makao Makuu ya Chama Mjini Dodoma
alipokuwa akijinadi kwa wapiga kura kutoka Mkoa wa Mara,Mbeya na Kigoma mara
walipowasili kutoka Mikoa hiyo
Alisema kuwa atasimamia maslahi ya vijana kwenye
vikao husika,kuipa UVCCM nguvu ya kiuchumi na kimaamuzi na kuimarisha jumuiya
na kuhakikisha ushindi wa kishindo ifikapo 2015 katika uchaguzi Mkuu.
Fatma
ameongeza kuwa vijana ndiyo nguvu ya Chama na kwamba na kwamba msingi wa
maendeleo ya vijana ni vijana wenyewe.
Katika
uzoefu ndani ya Chama ni Mjumbe wa kamati ya utekelezaji UVCCM UDSM,Mjumbe Baraza
la vijana Mkoa wa Ruvuma, Mjumbe Baraza la UWT Mkoa wa Ruvuma, Katibu Mkuu
Jumuiya ya walemavu UDSM (DUAH),Naibu Waziri Maji na Mazingira UDSM, na Afisa
afya na mazingira kata ya Ubungo.
Kwa upande
wa elimu ana Shahada ya ualimu aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
na sasa ni Mwalimu shule ya Sekondari ya wasichana Songea.
Wengine
waliokuwa wanajinadi na kutoa vipeperushi vyao ni Beatrice Omolo anayegombea
NEC, Nadra Rashid NEC,Edna Kwilasa NEC nafasi 6 Bara,Fadhila Nassor Abdi NEC
viti 4 Sango Kasera NEC Zanzibar,Lulu Abdallah NEC viti 4 Zanzibar,Neema
Nyangalilo Mgombea NEC,Anthony Mavunde mgombea NEC,Jerry Silaa Mgombea NEC Hassan
Chamshama NEC viti sita Bara,Neema Mwandabila NEC nafasi 6 Bara
Esther Sato Makune
na Zainabu Katimba wanaogombea Baraza Kuu Taifa nafasi tano,
Wengine
niliopata nafasi ya kuzungumza nao na kwamba wako imara na kuhakikisha Chama
kinaendelea kushika dola ni Mwanawewe Ussi Yahaya anayegombea BarazaKuu Taifa nafasi tano Zanzibar ,Rashid
Gewa na Asha Abdalla anayegombea Nafasi
ya Halmashauri Kuu kupitia UVCCM viti vinne Zanzibar.
Aidha vijana
Makao Makuu hapa Dodoma wamepamba Moto zaidi kwa Mgombea wa nafasi ya Makamu
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Paul Makonda ambapo baadhi ya wajumbe wamekuwa wakibeba
bago lako likiwa na maandishi ya heshima, uwezo na utu wa mgombea upimwe kwa
mchango wake katika jamii wala sio kundi au fedha alizonazo.
No comments:
Post a Comment