KAMANDA W A POLISI MKOA WA
MWANZA,KAMISHINA MSAIDIZI (ACP) LIBERATUS BARLOW ANAAGWA LEO KATIKA VIWANJA
VYA NYAMAGANA JIJINI MWANZA.
ACP BARLOW aliua usiku wa kuamkia oktoba 13 maeneo ya kitangiri na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi akitoka kumshindikiza mwanamke mmoja,Mwalimu wa Shule ya msingi Nyamagana aliyejulikana moja la Doroth Isasia Moses.
Kwa mara ya kwanza kutokea nchini Tanzania kufanyika mauaji ya Kamanda wa
Polisi.
Hii ni mara ya Kwanza kwa nchi yetu yenye
UPENDO,AMANI na UTULIVU kupatwa na simanzi na majonzi kwa mauji ya kikatili kwa
kiongozi wa ngazi ya juu, nchini Tanzania.
Mimi Eva-Sweet Musiba,nimesikitishwa sana na taarifa
hizi za mauaji ya Kamanda na nimepata simanzi kubwa kwa upande wangu na machozi
yanatiririka kila wakati nabaki
kujiuliza tunakwenda wapi na tumetoka wapi.
Dhana na polisi jamii iangaliwe kwa makini sana,
nadhani Kamanda Barlow alichukulia watu hao kuwa wana
Amani kumbe sivyo ndivyo,
alijua kuwa ni wenzake kumbe la!
Naomba jeshi la polisi kuwa makini sana,kwani kuna
baadhi ya askari hata Bastola hawana wakiwa katika doria.
Mh.Emmanuel Nchimbi,Waziri wa Mambo ya ndani, pole
kwa kupatwa na msiba mkubwa,jipange vyema ili kuboresha maisha ya askari wetu
ambao wafanya kazi kubwa na hatari sana katika maisha yao.
Natoa pole kwa familia ya marehemu,Wakazi wa Jiji la
Mwanza, Arusha na Watanzani wote kwa ujumla.
Baada ya mwili huo kuagwa Jijini Mwanza utasafirishwa kuelekea Jijini Dar Es Salaam eneo la Ukonga nyumbani kwa marehemu ambapo utaagwa na kuzikwa Oktoba 17 nyumbani kwao Marangu Moshi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz pokea kamanda na mpiganaji mwenzio.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA KILIMANJARO,ROBERT BOAZ
No comments:
Post a Comment