MKUU wa Wilaya ya Rorya
Elias Goroi imeomba Wizara ya Maji kupitia kwa Naibu Waziri,Bilinith Mahenge
kuona uwezekano wa kuipatia kipaumbele Wilaya hiyo kutokana na upya wa
Wilaya hasa maeneo ya Ingri juu na Komuge yalipo makao Makuu ya Wilaya.
Alisema kuwa
Wilaya mpya ya Rorya inayo changamoto kubwa ya ukosefu wa maji ambapo tayari
Halmashauri imetuma maombi ya fedha Wizara ya maji kwa ajili ya miradi minane
ambapo bunge lilipitisha miradi mitano ambayo ni ya Michele, Ingri Juu,
Garimori. Komuge na Masonga.
Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa sekta ya
maji ina chanagamoto nyingi ikiwemo mwitikio duni wa uchangiaji huduma ya maji
kwa watumiaji wa maji,uchakavu wa miundo mbinu ya maji unaotokana na na miradi
mingi kupita umri (Design Period) na gharama kubwa za uendeshaji miradi ya
skimu za pampu inayotumia Dizeli ama umeme .
Aliongeza kuwa ukilinganisha na mapato
yanayatokana na malipo ya maduhuri ya maji inawalazimu kutumia fedha
nyingi za matumizi ya kawaida na kusababisha miradi mingi kusimama kutokana na
ukosefu wa fedha za kulipia huduma ya mafuta na umeme.
Aidha kati ya vijiji 80 vilivyo katika
Wilaya ya Rorya, Vijiji 25 ndivyo vyenye mifuko ya maji yenye thamani ya
Sh.27,863,388, visima 85 na Kati ya hivyo visima 60 vinafanya kazi,
malambo 19 na mabwawa sita.
Naye Naibu Waziri alipotembelea ujenzi wa
Bwawa la Nyambori lenye ukubwa wa mita za ujazo 236,910 lenye uwezo wa
kuhudumia wakazi wapatao 3,785 alishangazwa na ujenzi huo ambapo kwa sasa bwawa
hilo lina nyufa ambazo zinahatarisha kuwepo na uendelevu wa kudumu wa wananchi
kupata huduma hiyo muhimu.
Pia alishangazwa na wananchi kuteka maji
eneo la kunyeshea mifugo ambapo wananchi hao walilalamikia uongozi
uliopo ambao unahifadhi funguo za bomba la wananchi hali ambayo ilimlazimu
Naibu Waziri Mahenge kuagiza uongozi wa kijiji kumchagua mwanamke ambaye ndiye
mwangaikaji wa kutafuta maji ili aweze kuwa na funguo hizo.
Wizara ya Maji ilikabidhi bwawa hilo kwa
halmashauri ambapo ililikabidhi kwa halmashauri ya kijiji kwa ajili
ya usimamizi na uendeshaji.
Aidha akiwa Wilayani Tarime Naibu
waziri wa Maji, Dk.Eng. Binilith Mahenge aliagiza Mamlaka ya Maji safi na Taka
(MUWASA) kuhakikisha inafatilia madeni ya wateja wake ili iweze
kujiendesha yenyewe.
“Mimi nashangaa sana mnasubiri maagizo kutoka juu wakati
mkijua kabisa kuwa hayo ndiyo majukumu yenu,angalieni wenzenu wa Tanesco
wanavyojiendesha wenyewe bila hata kuambiwa wasubiri kukata umeme kwa
fulani,kwa nini nyie mnashindwa kufanya hivyo”Aliuliza Mahenge.
Alisema suala la kupanda kwa gharama za umeme
haliwezi kuepukika na kuhusu suala la uchakavu wa miundombinu
linawezekana pale tu watakapojua kujiendesha wenyewe na kuwataka kujifunza
kuwekeza kwenye maji kwani ni mtaji usiohitaji gharama kubwa na ni zaidi ya
Almasi.
Serikali imetoa kiasi cha Sh. B.17.3 ya
uboreshaji wa maji Mjini Tarime ambapo Wilaya hiyo ina jumla ya visima 207
vilivofugwa pampu za mkono,miradi ya maji ya kusambaza na mabomba ipatayo
mitano.
No comments:
Post a Comment