Sunday, October 7, 2012

NI VYEMA KUWA NI WAPINZANI-CCM YASEMA

MUSOMA



MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Butiama, Yohana Mirumbe,amesema hataki kuona mpasuko unaotokana na makundi yta Uchaguzi kwa kuwa kazi hiyo imekwisha na kinachotakiwa ni kufanya kazi kwa bidii, Umoja na Mshikamano,

Alisema kuwa wajumbe hao wasimwone kuwa ni kijana na kwamba, atakayevurunda kazi katika utendaji wa Chama Wilayani humo, atafuata kanuni na katiba ili kurejesha maadili ya uongozi.

Aliyasema hayo juzi wakati akifungua kikao cha kwanza Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ambacho pia kilifanya  tathmin ya uchaguzi na kupendkeza kuwa wajumbe wawe wanapewa usafiri mzuri kuliko wa awali wa kubeba wajumbe kwenye malori.


Alisema  kuwa atafanya kazi kwa akushirikiana nao na kwamba viongozia mbao watakuwa wazembe ataanza na hao.

Kuhusu suala la wagombea wa CCM kunadiwa na vyama vya upinzani katika nafasi ya NEC, lililoonekana kwa baadhi ya wagombea wa NEC, Mirumbe alisema si jambo baya kwani wakiwa karibu nao watapata fursa ya kuwarudisha ndani ya Chama.

“Mimi sioni kama hilo ni tatizo uwenda wakiwa na sisi wanaweza kuvutiwa na sera zetu na kurejea katika Chama kwani walikuwa huku, kwa upande wangu ningependa kukaa nao na kubadilishana mawazo, unaweza kupata kitu kipya kutoka kwao na kuweza kufanya mabadilikoya haraka”Alisema Mirumbe.

Akizungumza na wajumbe hao, Mjumbe wa NEC, Wilaya ya Butiama, Christopher Siagi, alisema atashirikiana na wajumbe wote katika kuhakikisha wanapata maendeleo na kuhakikisha suala la usafiri mzuri kwa kipindi kijachao analivalia njuga.

Naye mgombea wa NEC ambaye kura zake hazikutosha Eva-Sweet Musiba, alitoa shukrani kwa wajumbe hao na kuwapatia barua za shukrani makatibu kata kwa kata 34 za Wilaya ya Butiama ikiwa  na ujumbe wa kutaka kufanya kazi kwa bidii na kukumbuka Kilimo ndicho kitakachowakomboa katika maisha yao na kuzingatia elimu kwa kusomesha watoto wao.


No comments:

Post a Comment