MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Mara nayemaliza muda wake, Makongoro Nyerere amesema kuwa jambo la posho ni jambo jema kwa
wanachama lakini limeingia vibaya ndani ya chama kwani limefanya wajumbe
kutochagua kiongozi bora na kujali wenye fedha zao.
Akizungumza na wajumbe wa halmashauri kuu ya wilaya kwenye kikao cha kwanza cha tathmini za
uchaguzi uliofanyika kilichofanyika hivi karibuni alilalamika jambo la posho.
“Posho ni jambo jema lakini limeingia vibaya katika CCM
limefanya watu wetu kusema kuwa kama hutoi
posho hutakiwi kuonekana sura
yako.”Alisisitiza Makongoro.
‘Tatizo chama chetu hakina mradi wowote wa kuzalisha tunapaswa tutafute mradi ili
tuweze kujiwekea akiba tunapota shughuli mbalimbali kama
hizi ziweze kutusaidia badala ya kutegemea mgombea kuja kuwawezesha wajumbe.”,aliongeza.
Makongoro alisema
kuwa kila mjumbe anayo haki ya kulipwa posho kama
wanavyolipwa wajumbe wa Kitaifa kwani bila wao wajumbeo hao wa kitaifa
wasingekuwepo.
Alisema kuwa kuna baadhi ya wanachama ambao hawana fedha na
wenye fedha hawapewie nafasi bila kwa
sababu zisizo za msingi.
Makongoro Nyerere aliowaomba wajumbe hao waweze kumpigia
kura katika uchaguzi utakaofayika oktoba 13 mwaka huu .
Wagombbea katika nafasi hiyo ni Enock Chambiri na Christopher Sanya.
No comments:
Post a Comment