Sunday, October 7, 2012

SHY-ROSE CHALI/MJASILIAMALI JUU!!! UWT MARA





MBUNG E wa Afrika Mashariki Shy-Rose Bhanji amebwagwa katika kinyang’anyiro cha Ujumbe Baraza Kuu la UWT Taifa, kuwakilisha kina Mama kutoka Mkoa wa Mara baada ya kushindwa na mjasiliamali mdogo, Agness Mathew alipata kura 274.


Shy-Rose ambaye pia ni  Mkuu wa kitengo cha Mahusiano na Jamii Benki ya NMB alipata kura 249, kati ya kura 526 zilizopigwa.


Awali akitangaza matokeo hayo Msimamizi wa uchaguzi, Jackson Msome alisema alimtangaza Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Mara kuwa ni Nancy Msafiri alipata kura za ndiyo 429 na kura 89 za hapana.


Aliwangaza wengine katika nafasi na kura zao zikiwa kwenye mabano kwa ya Mjumbe Mkutano Mkuu wa CCM Mkoa, alipata Stellah Manyonyi(312), Mkutano Mkuu CCM Taifa, Amina Masenza aliyepata kura (273), na  nafasi ya kuwakilisha Wazazi Mkoa, Mercy Mollel alipata kura 195 dhidi ya mpinzani wake wa karibu Rose Magoti, ambaye pia ni diwani wa viti Maalum (145),.


Nafasi ya uwakilishi vijana ilikwenda kwa  Victoria Chacha (271) na kumshinda Lina Lucas aliyepata kura (97) na katika nafasi mbili mbili kila Wilaya za Ujumbe wa Baraza la UWT Mkoa waliopita bila kupigwa kutoka Wilaya ya Bunda  ni Chausiku Luzama na Salome Lutoryo, Wilaya ya Rorya ni Marimu Odunga na Tamary Nashon


Waliopigiwa kura katika nafasi hiyo kutoka Wilaya ya Serengeti ni Maria Chacha(228) na  Dorice Kiraryo(129), katika Wilaya ya Butiama walioshinda ni Yustina Ngega(294) na Anna Bianda (186), Wilaya ya Tarime Kichena Chambiri alipigiwa kura akiwa amelazwa hospitalini baada ya kupat ajali akiwa njiani kuelekea kwenye uchaguzi huo kwa kupata kura (321) na Justina Mantago (245).


Awali akifungua kikao hicho cha Uchaguzi Mlezi wa UWT Mkoa wa Mara, Christopher Gachuma aliwaasa wachague viongozi walio bora na watakiokijengea Chama uwezo kwa kushinda katika uchaguzi ujao wa ngazi za vitongoji hadi Taifa.


Akizungumza mara baada ya kuchaguliwa Mwenyekiti wa UWT Mkoa, Nancy Msafiri aliwataka wabunge wa viti Maalumu kushiriki kikamilifu kuhakikisha  wanashiriki  katika Chaguzi zote.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Jackson Msome alitumia fursa hiyo kuomba kura kwa wajumbe kutoka Mkoa wa Mara watakamchagua Mjini Dodoma NEC  ya watu 10 kutoka Tanzania Bara.



No comments:

Post a Comment