Sunday, October 14, 2012

MRADI WA MAJI WEGERO WACHAKACHULIWA






MRADI WA MAJI WEGERO WACHAKACHULIWA.
BUTIAMA/SERENGETI


MRADI wa Maji Wegero ulioko katika Wilaya ya Butiama unaolalamikia na wananchi sasa kupata ufumbuzi.
Mradi huo uliogharimu jumla ya Sh.Milioni 969 .9 ulikabidhiwa kwa halmashauri ya Musoma Vijijini Feb.27 mwaka huu ambapo mkandarasi wake alikuwa kampuni ya Mwanza ya Jassie ya Jijini Mwanza.

Akizungumza mara baada ya kukagua bwawa hilo, Naibu Waziri wa Maji, Dk. Eng. Binilith Mahenge alisema ataleta wataalamu kuhakikisha ubora wa ujenzi wa bwawa hilo na kwamba tayari amemwagiza Mkandarasi aliyejenga bwawa hilo kurekebisha mapungufu yaliyopo.

Akijibu hoja mbalimbali zilizoulizwa na wakazi wa kijiji hicho juu ya kutumia maji hayo kwa kuwa bwawa hilo halijakabidhiwa rasmi, alisema wananchi waendelee kuyatumia kwani hayana madhara yoyote.
Ujenzi wa Bwawa la Wegero lilisimamiwa chini ya Mtaalam Mshauri Kampuni ya  Netwas Tanzania Limited ya Jijini Dar es Salaam ambapo ujenzi wa bwawa hilo ulianza Mei Mosi 2009.
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Nimrode Mkono amekuwa akilalamikia ujenzi wa bwawa hilo kuwa halina kiwango na halikupaswa kukabidhiwa.




No comments:

Post a Comment