Wednesday, October 10, 2012

ZIARA ya Naibu Waziri wa Maji yavumbua mengi.




MUSOMA.


Ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Dr.Eng. Binilith Mahenge imevumbua mengi yakiwemo madeni ya muda mrefu kwa wafanyakazi , wadeni, uchakavu wa mitambo ya maji Wilaya ya za Musoma na Butiama.

Akizungumza na wafanyakazi wa Mamlaka ya Maji safi na  taka katika ofisi za Mamlaka hiyo  Wilaya ya Musoma, wafanyakazi hao walipata fursa ya kutoa maoni na dukuduku zinazoikabili Mamlaka hiyo.


Akielezea tatizo la ulimbikizwaji wa madeni hasa kwa Taasisi za Kiserikali, Mhasibu wa (MUWASA) Richard Chisimbili alisema kuwa jeshi la polisi linadaiwa jumla ya Sh. Milioni 98 ambapo pamoja na kutuma taarifa kwa IGP Said Mwema deni hilo halijalipwa na kwamba ni la muda mrefu sasa hali ambayo inasababisha uendeshwaji wa Mamlaka hiyo kuwa mgumu.


Naye  Gantala  Said alimwelezea Naibu Waziri  kuwa makusanyo ya mapato ya maji kwa mwezi ni Sh.Milioni  105 hadi Milioni 110, malipo ya gharama za umeme kwa mwezi ni Sh. M.50, mishahara na makato ni Sh.Milioni 46, usomaji mita ni Sh M.6, madawa ya kuweka kwenye maji ni Sh. M. 5 hali  ambayo inasababisha watumishi kulipwa mishahara ama kucheleweshewa mishahara yao hadi kupungua kutoa Sh. M.46 hadi Sh. M.26.



Akizungumzia upotevu wa maji  katika Manispaa ya Musoma, Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo (MUWASA), Genes Kaduri alisema kuwa Mamlaka inapotez afedha nyingi kutokana na wateja wengi kutokuwa n a mita za maji, hali ambayo kwa sasa wanalipa kwa kukadilia matumizi ya mwananchi, pia baadhi ya viwanda kutumia maji ya moja kwa moja kutoka ziwani bila kulipia kutoka kwenye Mamlaka hiyo.

Akitoa  ombi  kwa Naibu Waziri, Naye Edson Mwambene alisema kutokana  na tarifu ya umeme kuwa kubwa, aniomba Wizara kuangalia suala la kuondoa  VAT kwenye umeme na madawa ya maji ili mamlaka hiyo ipate angalau unafuu kidogo.

Akijibu hoja hizo Naibu Waziri alisema kuwa atawasiliana na wadeni hao ili walipe madeni yao, pia suala la VAT amelipokea na litafanyiwa kazi.

Naibu Waziri Dr.Eng. Binilith Mahenge alisema kuwa Serikali tayari imetoa Sh. Milioni 40 kwa ajili ua mradi wa Maji Manispaa ya Musoma na kutoa wito kwa wafnyakzi na watumishi wafanye jitihada za makusudi ili kuboresha maji katika Manispaa,kwani maji ya sasa ni machafu kutoka na kuwa na chujio chakavu,hali ambayo inahatarisha maisha ya wakazi wake.


Akisoma taarifa kwa Naibu Waziri, Meneja Mradi wa Maji, Mugango/Kibakari/Butiama, Merchades Anaclet  alisema kuwa mpaka mwishoni mwa  mwezi Septemba 2012 jeshi la la wananchi kikosi cha kiabakari(253KJ) linadaiwa jumla ya Sh.57,905,918 za umeme na mitambo.

Naibu Waziri Mahenge yuko Mkoa Mara kwa ziara ya kutembelea miradi ya Maji ambapo amekwenda katika mradi wa maji wa Mugango/Kiabakari/Butiama na amezulu kaburi la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na kumsalimia  Mjane wa Mwalimu Maria Nyerere ambaye ambaye aliwasili muda mfupi akitokea  Jijini Dar es Salaam.



No comments:

Post a Comment